Umejua dhumuni lako la kuwepo?

Umejua dhumuni lako la kuwepo?

de Gunner

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2021
Posts
11,090
Reaction score
21,978
We live in the same existence but share different realities

Wewe ulijuaje dhumuni lako la kuwepo hapa duniani?

Tukachana na dhana za nature eti kuzaliwa, kuzaliana na kufa.. Kuna kitu ndani yako kinacho kufanya uamke kila siku uka hustle ni kina msukimo wa nini haswa?

Na uligunduaje ya kuwa hicho ndo kitu pekee kinacho kufanya ufanye unalo fanya.

Tupac shakur alisha wahi kusema,
"I may not change the world, but I may spark the minds that will do"

Anyways blue Monday hiyoo, wale wa kwenda kufanya jambo lile lile kwa miaka 50 straight tuamke.
 
Wito namba mbili ni kumpenda Mwenyezi Mungu kwa akili zite, nguvu zote na kwa moyo wote. Pia kumpenda jirani kama niipendavyo nafsi yangu.

Wote tukiweza kuyafanya haya kikamilifu, hakika dunia itakuwa ni Paradiso chini ya jua.
Sawa sawa.
Hivi kumbe Paradiso ni dhana tu, ila ni hapa hapa duniani?
 
Binafsi mimi naamini kuwa nipo duniani, nahishi ili nitimize kusudi la Mungu (ambaye naamini ndiye aliyeniumba).

Lakini kutokana na mfumo wa maisha, kutokana na dhana ya kwamba mwanadamu ameumbwa kwa mfano wa Mungu. Kila binadamu amepewa fikira, uwezo, nguvu, muda, utashi nk vinavyomsaidia kufanya jambo lolote.

Hivyo mwanadamu hutengeneza au kufanya jambo ambalo linamsaidia kulipa maana kusudi la kuhishi kwake kwa vitendo.
 
Lakini kutokana na mfumo wa maisha, kutokana na dhana ya kwamba mwanadamu ameumbwa kwa mfano wa Mungu. Kila binadamu amepewa fikira, uwezo, nguvu, muda, utashi nk vinavyomsaidia kufanya jambo lolote.

Hivyo mwanadamu hutengeneza au kufanya jambo ambalo linamsaidia kulipa maana kusudi la kuhishi kwake kwa vitendo.
Kwa hiyo mwizi au malaya nae anaishi kusudi lake?
 
Kwa hiyo mwizi au malaya nae anaishi kusudi lake?
Sasa yeye kama ameona hiyo ndio mission yake. Kwa watu wanaoamini kwa Mungu wa Israel tutakwambia, hapana. Huyo haishi katik akusudi lake bali amelikiuka agano. Lakini hiyo ni kwa mujibu wa imani ya upande wetu. Huenda labda kuna upande mwingine wanaamini kwa kufanya hivyo wanahishi katika kusudi.
 
Sasa yeye kama ameona hiyo ndio mission yake. Kwa watu wanaoamini kwa Mungu wa Israel tutakwambia, hapana. Huyo haishi katik akusudi lake bali amelikiuka agano. Lakini hiyo ni kwa mujibu wa imani ya upande wetu. Huenda labda kuna upande mwingine wanaamini kwa kufanya hivyo wanahishi katika kusudi.
Inafikirisha sana mkuu
 
As long as kuna watu wanategemea huduma yake yawezekana hilo ndilo kusudi lake.
Tofautisha, kuna kusudi la Mungu la kuwepo kwa mwanadamu hapa duniani pia kuna kusudi la mwanadamu mwenyewe.

Nimejibu kwa mujibu wa swali lako.
Ok mkuu
So kumbe kuna kusudi la Mungu na la mwanadamu...

Sasa je, hilo la umalaya ni kusudi la haki mbele za Mungu aliye kuleta?
 
Back
Top Bottom