Mkwaruzo
JF-Expert Member
- Feb 21, 2011
- 563
- 98
Usiku mmoja mume na mke wake wakiwa wamelala. Mke akiwa ndani ya ndoto akanza kusema "kimbia mume wangu anakuja... kimbia mume wangu anakuja..." Hafla mume akashtuka na kuanza kukimbia lakini akagundua kuwa yupo kwake ikabidi arudi. Lakini wakati anakimbia mke naye alishtuka na kumuona mume wake anakimbia. Akamuuliza mume wake "unakimbia nini?" Mume hakujibu ila naye kwa ukali akamuuliza ni nani huyo uliyekuwa unamuambia akimbie?