Umasikini wetu ni akili sio mali wala fedha

Umasikini wetu ni akili sio mali wala fedha

Hivi FF Nyerere alikufanya kitu gani? Kama alivunja ndoa ya wazazi wako basi naamini ilikuwa ni kwa manufaa ya umma. Mimi sioni uhusiano wa sisi kutokuwa na utamaduni wa kujitegemea na Nyerere. Nafikiri siasa ya ujamaa na kujitegemea hukuielewa vyema. Na kuhusu akili, nafikiri hata sasa huna na ndio maana miaka kadhaa baada ya utawala wa Nyerere kuondoka bado umeweka masaburi chini ukimlaumu badala ya kuwajibika.

Naomba unitumie kamfano kadogo tu kanakoonesha kuwa Nyerere alikuwa OMBA-OMBA kama Mh.Dokta. Manake nahisi una jambo binafsi na Nyerere
 
Aisee una akili wewe.......... hata mimi nimekuwa nikigombana na wenzangu kazini kila nikiwambia umasikini tulio nao tumejitakia........ watu wanachanga milioni hadi 20 kwa harusi lakini kuna ndugu wa muoaji au muolewaji wameshindwa kuendelelea na masomo kwa sababu ya ada.............. hivi kama tuna uwezo wa kuwa na ndugu na marafiki au jamaa wenye uwezo wa kukusanya milioni 20 kwa sherehe ya harusi ya siku moja tu, tunashindwaje kuwashawishi watuchangie ili kuwawezesha ndugu zetu kuendelea na elimu ya juu kwa ustawi wa nchi yetu? kwa wagonjwa ndio usiseme.......... unaweza kushangaa marehemu anapanda ndege kwa mara ya kwanza kwenda kuzikwa lakini kifo chake kilitokana na kukosa dawa au huduma zilizo bora.................
 
Mfano mwingine, watanzania wengi tu mtu hana kazi maana lakini ana simu mbili..matumizi mabaya ya pesa

siyo hivyo 2 Topical, mtu asubuh na mapema anaamka anakaa kwenye kochi anatazama tv. Program yenyewe music, nusu saa badae ananunua vocha elfu tatu elfu mbili, bdo hajala, na pengne hana kaz, unadhan huyu tutamwita maskin asiye na fedha. Akil ndo kila kitu.
 
Unaweza kumulza mtu, we ni maskin akajbu ndiyo, ukimulza kwa nin atakujib hana hela, ukimulza ukimpa hela km milion tatu ataifanyia nin il kesho asiseme tena yeye ni maskin hataweza kukujibu. Hiyo ni kwa sababu hana akil ya kuweka malengo, hana mpanglio wa maisha yeye anaish mrad kunakucha na kunakuchwa bas. Umaskin cyo kutokuwa na mali na hela hata hao wenye mal na fedha ni maskin tena sana na ndo mana wanaishia kutumia madaraka vbaya.
 
Hivi hiyo akili tumeipata lini? Wakati miaka zaidi ya 20 ya mwanzo tuligubikwa kwa kuaminishwa kuwa mwenye akili ni mmoja tu. Tuliwekwa ndondocha.

hv dada yangu kazi huwa unafanya sa ngapi? Au mmeo unakaa nae saangapi, kwa7bu kwenye karibu kila thread nakukuta.
 
nimejaribu kuchunguza mambo hasa katika field ya afya na nimeona tatizo linalotusumbua sio fedha bali ni akili au utashi wa kufanya mambo muhimu.nikichukulia mfano wa mama mjamzito anapokwenda kujifungua bila kubeba pamba,mipira(gloves) au cord clamp kisa kaambiwa huduma ya kujifungua ni bure!ukipiga mahesabu vifaa hivi vinaweza kugharimu sh.10000 tu.lakini mama huyo huyo ataletwa hospitali na tax(10000) huku akiwa amebeba kanga na vitenge vipya vinavyogharimu sh 35000+,halafu akijifungua atafanyiwa party inayogharimu zaidi ya sh 60000.sasa hapa utajiuliza kipaumbele ni nini!
wamarekani(USAID) wanajichukulia umaarufu katika kuchangia huduma hizi za afya na hela hizi huchangwa na watu(wananchi) wa marekani.je kwa nini wananchi wa Tanzania wasitoe michango yao(fund rising) na kusaidia watanzania wengine?tunasaidiwa fedha ambazo tunaweza kuzikusanya wenyewe kama tukiamua.hivi tuna shida gani upstairs?


Ni kweli kabisa ulisemalo na linahitaji hatua za makusudi kujirekebisha.Lakini kumbuka ndugu Viongozi wetu ni vipofu na vilaza walio wengi na wanawaongoza vipofu wenzao ni nani aanze kurekebisha hili wakati hata Rais wako hajui kwa nini Nchi yake ni maskini?Mashine za Muhimbili(Xray,utrasound,za kusafishia damu n.k) ni mbovu na hakuna anayeuliza kulikoni na wakati huo huo tumetumia zaidi ya 64billioni achana na za kila wizara ktk sherehe za uhuru wa hapa Dar maana wa Mikoani hawakuona.Jimbo mmoja tu la uchaguzi mfano la Igunga serikali imetumia si chini ya 10billioni maandalizi tu achana na za vyama husika ktk kampeni zao,na linakuja hili la kafulila ni zaidi ya 10bilioni nyingine zitatumika bila sababu za msingi.
Na wakati huohuo Serikali inakwambia haina pesa za kununua vifaa vya Hospitali,kujenga barabara na maendeleo mengineni ujinga na akili finyu kukubali dhana hiyo ya kijinga.Kama hatutabadili mwendo huu wa siasa mbovu za bongo hata raia kuwabadili ni ngumu.
 
Mpaka tutakapo tambua kuwa dawa zinazotibu magonjwa 40 zinazofanya mti wa muorobaini Ni za kuutibu Mti Huo na si zakumtibu mwanadamu ndipo tutambua maana ya KUJITEGEMEA!

Uasili wa mti wa mwarobaini ungefanya mzaha Kizazi cha mti huo ungefutika duniani ... so it was to work hard for its survival!

Uasili wa mwanadamu ambao ni Utu na Akili yake ... ungelazimika vilevile .. kupambana na mazingira na kujitegenezea dawa zake na sio kukopa toka nje yake ... ndio! Kama Miti na wanyama PORINI wanapona wenyewe ... Iweje mwandamu ..asiwe na uwezo huo?

Na uwezo huo ambao ndio maana yake kujitegemea ..ungemfanya mwandadamu ajitegemea .. Kielimu, kiuchumi, kifaya nk..

Tatizo ni Kudharau UNDANI wake MWENYWE! ...yaani AKILI, UFAHAMU, UTU NA HISIA ZAKE!!

Jibu la kweli la Matatizo ya Mwanadamu haliko nje yake ... NI NDANI YAKE ...!

Mwanadamu akibanwa kidogo ...akabanwa tena na tena ... Undani wake UTAAMKA!!

Na niswala la muda tu!! ... Atatokea Mtu anapona Mwenyewe kama tumbili wa mwituni na hondo hondo agani!

Kama mafuta ya Simba ni dawa .. ni dawa kwa huyo simba sio kwa mwandamu ... Simba ajitegemee na mwandamu ajitegemee...

Hakuna majibu kuleee mbali ... Mwanadamu anvyozidi kwenda mbali na yeye mwenyewe ... ni dhibitisho na wendawazimu wake ...

Bora kuamua kujirudi ...kujichunguza ... na kujitambua ... na kutambua kuwa siri ya mafanikio yote ..yamejikita kwenye uasili wake .. ambao sio unyama ..ni UTU wake ... akili zake... UAFAHAMU wake ...hivyo vifanyiwea kazi hadi ...UKOMBOZI UFIKIWE!!!
 
hainingii akilini ni kwa vipi mama mjamzito anasaidiwa iwapo anajifungulia njiani kuelekea kituo cha afya.nashangaa mwanasiasa anapomwambia mama huyu asibebe mipira au pamba anapoenda kituo cha afya?huu ni umasikini wa akili na sio fedha.
 
tujifunze kujitegemea,hii aibu ya kutembeza kibakuli mpaka lini?
 
Umasikini hauanzii mfukoni, bali unaanzia kwenye akili.

Aina ya fikra ulizonazo ndio zitaendelea kukumbatia umasikini au kuufukuza na kuingia kwenye utajiri.

Na hii ndio kazi ngumu sana maana jamii inayokuzunguka inakulazimisha uwe na fikra za kimasikini, uone matajiri ni wabaya na masikini wana haki zaidi.

Mfano.
Nyumba ya tajiri inataka kubomolewa, jamii nzima safi sana.

Nyumba ya masikini inataka kubomolewa, jamiii nzima ni uonevu huo.

Unahitaji kuondokana na fikra hizi haraka sana, kama hutaki kufa masikini.
#shared
 
Last edited by a moderator:
Mi nadhani watu wanafurahia kubomolewa nyumba ya tajiri iwapo wanaona tajiri mwenyewe Kuna namna anadhulumu wanyonge. Lakini ukiwa na mkwanja wako Safi bila dhuluma.. Mbona hamna mtu Ana shida na wewe.
 
Mi nadhani watu wanafurahia kubomolewa nyumba ya tajiri iwapo wanaona tajiri mwenyewe Kuna namna anadhulumu wanyonge. Lakini ukiwa na mkwanja wako Safi bila dhuluma.. Mbona hamna mtu Ana shida na wewe.
Na utajiri wa wabongo wengi ni wa dhuluma haposasa hata ndugu wenyewe wanadhulumiana.
 
Amani ya bwana iwe nanyi watu wa jukwaa hili kuna vitu nilikua navisikiaga zaman lakin sikuweza kuamini leo ndo nimeamini

Bora uwe masikin wa fedha na nguo lakin siyo kuwa masikini wa hakili alichokifanya manji na mchungaji gwajima ni umasikin wa hakili wamefanya mtihan lakin hawajafata maelekezo ndo maana wamekoseshwa na hawajasahishwa kabisa

Wakae wakijua hii ni awamu ya tano kwahiyo wasitake kujifanya kwamba wako juu ya sheria
Hakuna aliye juu ya sheria kwa awamu hii ya tano mi nawapa pole sana pole yao

Na kuna uwezekano hata kesho hawata achiwa kwa sababu wamefanya zalau sana sana ya kumupangia mkuu wa mkoa mda wa kuonana naye wakati naye ana ratiba zake

Mtu kavimbeya anakuja na jopo la mawakili utakazan anaakuja kwenye kesi hii sio kesi haya ni mahojiano tu

Mpaka wanyoke ccm mbele kwa mbele
 
Hakili =Akili
Mubaya=Mbaya
Zalau =Dharau
Kumupangia =kumpangia
Sasa tuje kwenye hoja!!
Ukishaambiwa unahitajika kituo cha polisi unaweza ripoti muda wowote ili mradi siku uliyoambiwa isipite, mkuu wa mkoa kwako unamuona mungu Eeh! Jinga kabisa na ushamba wako wa kisukuma!!! Umlaze manji ndani kwa lipi!! Mwenzake yuko kwake wewe umebaki na kisimu chako cha kugongea huko maswa unaandika ujinga tu
 
Back
Top Bottom