Umasikini sio hatma ya Wachina wala Waafrika

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG111350897178.jpg

Baraza la serikali ya China limetoa waraka wenye kichwa “Safari ya China kutoka umasikini hadi kwenye neema” ukitaja maendeleo yaliyopatikana nchini China kuanzia mwaka 1952, hadi mwaka 2020. Baadhi ya takwimu zilizotajwa kwenye waraka huo, ni kuwa katika kipindi hicho pato la taifa la China limeongezeka kutoka dola milioni 10 za kimarekani kwa mwaka 1952 hadi dola trilioni 15.5 kwa mwaka, wakati pato la mtu mmoja moja limeongezeka kutoka dola 100 za kimarekani kwa mwaka hadi dola elfu 10.

Maendeleo yaliyopatikana nchini China bila shaka ni habari kubwa ya karne, na imeonyesha kuwa hakuna watu walioandikiwa na Mungu kuwa wao watakuwa maskini. Katika kipindi kifupi katika historia ya binadamu, China chini ya uongozi wa chama cha kikomunisti imeweza kutokomeza matatizo ya njaa na umaskini kwa watu wake, na kuweza kujenga uchumi imara ambao pia unatoa mchango kwa maendeleo ya wengine duniani.

Lakini tukubali kuwa maendeleo ya China bila shaka hayajapokelewa vizuri na baadhi ya nchi. Katika muda mrefu uliopita, neema ilionekana kuwa ni haki ya kundi la nchi fulani, na taabu ilionekana kuwa ni stahili ya kundi la nchi fulani. Maendeleo ya China yamethibitisha kuwa huu si ukweli, na hakuna mahali ilipotajwa kuwa neema ni haki ya watu fulani, na taabu ni stahili ya watu fulani. Kutokana na uongozi wenye maono, kujiamini, na juhudi endelevu na bila kuogopa taabu vinaweza kubadilisha jamii yoyote kutoka hali duni na kuwa na neema.

Maendeleo ya China yametoa mfano bora kwa nchi nyingi za dunia ya tatu, na kuna mengi ya kujifunza kutoka kwa China. Tukiangalia hali ya nchi nyingi za Afrika kwa sasa tunaweza kuona kuwa bado kuna changamoto nyingi kama vile njaa na umaskini. Vilevile tunaweza kuona dalili za neema. Mambo ambayo zamani yaliaminika kuwa ni haki ya wazungu wa Ulaya na Marekani au Japan, sasa polepole yanaonekana kwenye baadhi ya nchi za Afrika. Pamoja na kuwa safari bado ni ndefu, lakini mfano umeoneshwa na China kuwa inawezekana, na pia mazingira wezeshi pia yanaonekana.

Bara la Afrika lina nguvu kazi kubwa ya vijana, lina soko kubwa, na lina raslimali nyingi. Vyote hivi ni msingi mzuri wa kuhimiza maendeleo. Uzuri wa dunia ya sasa ni kuwa teknolojia nyingi zinazoweza kutumika kujiendeleza zinazoweza kupatikana kwa kununua au kutoka kwa nchi rafiki. Uzuri ni kuwa ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika, katika miaka ya hivi karibuni umeweza kuzisaidia nchi za Afrika kupata teknolojia za kuhimiza maendeleo. Kuimarishwa kwa ushirikiano katika maeneo yatakayochochea maendeleo kwa nchi za Afrika, kunaweza kutoa msukumo mkubwa wa maendeleo kwa nchi za Afrika.

Ni bahati mbaya sana kuona baadhi ya nchi za magharibi hazina furaha kuona China inakwenda juu na kufuta ile imani ya zamani, kwamba kuwa juu na kuwa na neema ni haki ya watu wa magharibi. Lakini pia ushirikiano kati ya China na nchi za Afrika pia umepunguza sana utegemezi wa nchi za Afrika nchi za Afrika kwa nchi za magharibi, kwa hiyo inawezekana kuwa baadhi wanapenda kuona Afrika inaendelea kuwa nyuma kila siku. Lakini ukweli umethibitisha kuwa, umaskini sio hatma ya kundi fulani la watu.
 
Mkuu ni Kweli kabisa. China imeweza ku transform hata uchumi wa Africa na third world country hata wale wenye kipato cha chini Ulaya na America wananufaika na ukuaji wa China,Viva China!
 
Back
Top Bottom