Umasikini si kilema angalia potentials za mtu

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Kuna dada alinihadithia alivyokutana na mume wake. Walisoma wote shule ya msingi enzi zile za ujamaa hakuna English Medium wote tulikuwa St Kayumba. Mume wake alikuwa anakuja shule na deli la Ice cream, nyumbani hali haikuwa nzuri sana na kila mtu alichangia alivyoweza. Mama aliuza maandazi na watoto wengine walipewa karanga.

Enzi hizo dada anashushwa shule na STG na akitoka shule inamsubiri. Hawakuwahi kuzoeana. Walikutana chuo kikuu, wakati huo kijana nae ana boom. Walikumbukana na wakaanza kupiga stori. Kutokana na maisha aliyopitia kijana alikuwa mshauri mzuri kwa bi dada.

Walianza kuwa wapenzi wakiahidiana kufunga ndoa. Bidada alipomkaribisha kwao kijana alikosa kabisa amani ya kumpeleka kwa mama yake ambae ni single mother wa watoto watatu, wamepangisha vyumba viwili.

Dada alielewa hali walikubaliana kufanya harusi ndogo tu ya katikati ya wiki mradi kijana atoe posa kwao. Madada wakubwa wa msichana walimshauri aachane na kijana masikini atabeba mtatizo ya ukoo. Huyu dada anasema si mapenzi tu,?heshima aliyopewa na kijana alikua hataipata kwa mwanaume yeyote yule mwingine.

Walifunga ndoa na kuanza maisha. Mama walimjengea nyumba, mama mwenyewe ni muelewaji wa hali anajiongeza sana. Anauza maji mtaani kwake wala si wakuomba pesa ya kula.

Dada ana amani na ndoa yake, mume wake ameahidi kumpeleka ofisini asubuhi na kumchukua jioni kama ile STG ilivyo mhudumia wakiwa shulevya msingi.
 
Kuna dada alinihadithia alivyokutana na mume wake. Walisoma wote shule ya msingi enzi zile za ujamaa hakuna English Medium wote tulikuwa St Kayumba. Mume wake alikuwa anakuja shule na feki la Ice cream, nyumbani hali haikuwa nzuri sana na kila mtu alichangia alivyoweza. Mama aliuza maandazi na watoto wengine walipewa karanga.

Enzi hizo dada anashushwa shule na STG na akitoka shule inamsubiri. Hawakuwahi kuzoeana. Walikutana chuo kikuu, wakati huo kijana nae ana boom. Walikumbukana na wakaanza kupiga stori. Kutokana na maisha aliyopitia kijana alikuwa mshauri mzuri kwa bi dada.

Walianza kuwa wapenzi wakiahidiana kufunga ndoa. Bidada alipomkatibisha kwao kijana alikosa kabisa amani ya kumpeleka kwa mama yake ambae ni single mother wa watoto watatu, wamepangisha vyumba viwili.

Dada alielewa hali walikubaliana kufanya harusi ndogo tu ya katikati ya wiki mradi kijana atoe posa kwao. Madada wakubwa wa msichana walimshauri aachane na kijana masikini atabeba mtatizo ya ukiona. Huyu dada anasema si mapenzi tu,?heshima aliyopewa na kijana alikua hataipata kwa mwanaume yeyote yule mwingine.

Walifunga ndoa na kuanza maisha. Mama walimjengea nyumba, mama mwenyewe ni muelewaji wa hali anajiongeza sana. Anauza maji mtaani kwake wala hao ni pesa ya kula.

Dada ana amani na ndoa yake, mume wake ameahidi kumpeleka ofisini asubuhi na kumchukua jioni kama ile STG ilivyo mhudumia wakiwa shulevya msingi.
Ndoa ni upendo sio mali. Tatizo wazazi wengine wenye uwezo hawapendi watoto wao waolewe na wanaume malofa, hawajui kuwa maisha hayana kanuni.
 
wanawake wa aina hiyo ni wachache sana, wadada mpitie uzi huu kujifunza ili muache tamaa za kijinga hadi mkawaacha watu sahh katika maisha yenu.
 
Hiyo imetokea kwa Zuhura na Heri
Hivyo hivyo kasoro wao hawana magari
 
Back
Top Bottom