Ulokole wa facebook

Ulokole wa facebook

Binti Magufuli

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2011
Posts
7,479
Reaction score
5,160
Salamu kwenu waungwana wa jukwaa hili.

Salamu pia ziwaendee wale walokole wa mitandaoni wakati nje ya mitandao wanajijua wenyewe vile waishivyo.

Binafsi ni mdau mzuri wa facebook (hasa kipande ya usomaji zaidi wa kile wadau wengine wanachopost). Kwa ufupi kule watu walio wengi ni wema sana, full kuposti mistari ya biblia na kukemea uovu yani kule unaweza kujiona wewe ndio shetani peke yako duniani. Wnawake wengi walio single (hasa wale walioko kwenye 30's na hakijaeleweka) ndio usiseme kwa injili. Yani ni kama dozi (asubuhi mchana na jioni). Wakati mwingine hata inakuwa ngumu kwetu sie kuishi maisha yetu ya ukweli manake wahukumu ni wengi sana.
Sasa mie nilishangaa mmoja wa walokole hao maarufu kwa kuposti mistari ambae awali alikuwa anaishi kinyumba na njemba moja alipokuwa na mimba siku ya ndoa yake (na njemba nyingine).Sasa ulokole na mimba kabla ya ndoa wapi na wapi?

Wanawake wengi wameamua kuutumia ulokole km gia ya kuwanasa wakaka wengi wa karne ya 21 ambao wanaziogopa ndoa
km ukoma. Ule ulokole kwa asilimia kubwa ni fake (Sio kwa wote lakini). Mtu amekula dunia wee hadi dunia imemchoka, mtaani alishachakaza sasa anaona usiku unakaribia suluhisho ni mwendo wa kuposti verse tu ili awanase walio wengi. Zinduka but that is none of my business
 
#but thatsnoneofmybusiness
salamu ziwaendee ma madam woooteeee waliokula dunia na wanaendela kula dunia ila facebook na mitandaoni ni full ulokole. ishi maisha yako usiwe mtumwa wa maisha ambayo huyaishi
 
Wanawake wengi wameamua kuutumia ulokole km gia ya kuwanasa wakaka wengi wa karne ya 21

hapo nimekusoma lkn ulokole sio kama wanavofikiria
 
True story! Wadada wa fb sina ham nao na ulokole wao fake.
 
Nilishatishiwa maisha na walokole. Ni baada ya kuwahoji maswali walioshindwa kuyajibu.
 
Back
Top Bottom