Ulipataje kazi yako

Ulipataje kazi yako

sijui kama utakaa uitwe kwenye interview kwa kukaa tu home na kusubiria .tafuta watu wakuunganishe au tafuta waajiru wenyewe live.
hicho chuo ulichomaliza kawaone pia maadmin wa hapo live
Yaan ungejua,,yaan kwanza kipindi hiki cha shida nawasoma watu wa ukweli na fake..
Hao ma secretary wa ma HR walivo na nyodo jamn..
Nitajaribu ya kupita vyuoni mwenyew..thank u fr the alert.
 
haha anaota nilitafutiwa na na bibie mmoja niliyefanyanaye kazi japo huko nyuma tulikorofishana lakini akanisaidia baada ya kuona nimepigika ,,,,,,,,,, katika kampuni yoyote ninayofanya kazi sitoi uchi... ni chanzo cha kunyanyaswa na kufukuzwa muda wowotw wanaotaka



by the wway anayenila mzigo yumo humu humu jf hahaha

Yaani siku zote najua wewe ni Mwanaume.
 
Mimi nina uzoefu mwingi katika swala zima la kutafuta Ajira, mbinu nyingine ni za kawaida/haki zingine ni za haramu. Na kuna wengi nimewasaidia either kwa ushauri tu kwa kuzingatia ABCD nilizowapa. Currently, mbinu ninayotumia kupata Kazi ni kuonana na mtoa kazi/bosi/mwajiri....sio CV, Portfolio, Uzoefu au Barua ndefu...changamoto yake ni Mapokezi/Reception/Walinzi, wengi watakuzuia ati hadu uwe na appointment na mtu unayetaka kumuona...

.lakini nikishavukaga hicho kipengele, ole mwajiri nimtie machoni na nishushe madini....HANIACHI NA KESHO YAKE HUWA NAANZA KAZI. Kwahiyo mbinu hii huwa naiita ni Siraha ya Kisaikolojia, Saikolojia ambayo nimeivuna kwa miaka kama 4 hivi ya utafutaji kazi. Yaani siku hizi hata huwa sisomi maswali mapya ambayo HR huwa wanagoogle na kuniandalia, au kubabaika na walivyojipanga....yaani kabla hajamaliza swali, tayari jibu ninalo ambalo litamoderate swali lake la pili!!!! patamu hapo.....so kazi nyingi huwa nazikosa either kwasababu ya formality tu, yaani tayari wana mtu wao lakini ukiondoam watasemezana " dah...hiki kichwa kilistahili kuwa hapa sema ndo ivyo mtoto wa bosi hana kazi!"

Pamoja mbinu hiyo, huwa nina hakikisha document zote zipo ready, yaani CV, barua, vyeti, recommendation letters, referrees (ambao mara nyingi huwa ni washkaji zangu ambao nimeshawalisha madini. maana ndugu au waajiri waliopita wameshachoka kila siku kusumbuliwa). Marafiki huwa nina wapanga "eb bhana ee, ni aje ninja wangu, utapigiwa simu na HR, mwambie Nyankunde namjua ni mchapa kazi, mpeni kazi...siwezi kuongea sana kwa sasa maana nipo kwenye Kikao!" mchezo kwisha.

Njia ya tatu ni haramu, but nani ambae sio haramu kwasasa?? NANI???....kila kitu ni feki. Nina dokta rafiki yangu na hata juzi alionekana kwa TV akinadi product zake, sasa nilipokuwa namfanyia kazi yake akasema" hivi km mkuu wa mkoa an vyeti vyeki lakini ameweza kuwa mkuu wa mkoa, kwanini mm nishindwe kuwa dokta??!!.....nilicheka sana, na nilitafakari kwa jicho la 3.

Nnjia hii inapita kwenye uvuvio huohuo niliouchanganua hapo juu japo sifa yake kubwa ni "Confidence", yaani ni sawa sawa na kufanya kosa lakini bado ujione mwenye haki na unastahili...yaani kile kitu kinaitwa dhambi/uongo/guilty/karma uone ni kama miradi ya wapiga dili tu lakini hizo vitu havipo (thi is my current mentality of course). Njia hii ni VYETI FEKI. yaani unamktuta mtu ana uzoefu na kazi flani, au graduate wa form six mwenye uwezo kabisa wa kufundisha watoto wa Secondary kwenye International School....ila kwakuwa hana vyeti vya ngazi za juu, mavyeti ya recognition, recommendation letters n.k., ataishia kupauka tu.

Sasa mimi nilisolve swala hilo kwa kujifunza Graphic Design/Digital Imaging, nikiri tu wazi hadi sasa kuna watu wapo kwenye ajira na wananizidi hela kwasababu nilispend the whole night to just get that IFM Certificate right just like the original one! na ndio wanaoniweka mjini maana nina siri zao. Sasa utaniuliza; vipi kuhusu NECTA, coz jina lazima liwe kwenye sytem yao n.k.....au vyeti vya siku hizi vinatoka na passport size....!! Hii siri siitoi, madude mengine ntashusha siku ingine.

Kufoji vyeti sipendi ila ni njaa tu wandugu, ila kwasasa nimeridhika na ajira niliyonayo. Ila WARNING KWA WANAFUNZI WA VYUO: acheni kusccan vyeti vyenu kwenye stationary zilizo karibu na Vyuo vyenu, watu huwa tunakuja na vifrash vyetu tulivyoagiza kutoka India, nikiingia pale nanyonya data za Stationary nzima *****....nikrudi gheto najichagulia jina zuri hahahaha!....hii ni mojawapo tu ya mbinu ya watu KASOMEA JINA HILI, KAAJIRIWA KWA JINA HILI...kumbe aliwaona wataalamu hahahah!

Pia nyie NECTA na viportal vyenu vya kuverify nyaraka, zuieni Mirroring za Portal zenu.

#I'mOut
Hii ya kuchukua docs za stationary, nakumbuka kuna wanafunzi nimewafanyia kazi ya kufoji vyeti pale SJUIT dom, pamoja na slips za malipo ya ada..naadae nikakuta wananifata hadi home usiku wa manane, nikaachaga hiyo kazi.. Ilaa ni shida
 
kila siku nilikuwa nanunua gazeti la daily news ili kutafuta kazi .siku moja nikakuta kijarida cha ppra kimeandikwa matender waliyoaward kwa watu mbalimbali
nikaangalia kampuni ambayo ilikuwa imepewa tender kubwa nikaona moja ina bilion kadhaa. nikaingia mtandaoni nikatafuta contact zao
bahati nzuri kwenye website yao wameweka namba ya simu ya mkurugenzi .nikakuta kumbe yupo whatsup nikamtext akaniambia yupo nje ya nchi akija atanitafuta.siku moja akaniambia yupo dar ila anatafuta siku anitumie nauli .sikusubiria nauli nikaja dar nikamwambia nipo dar mzee.
akaniambia basi njoo jmosi tutakuwa wote mgt njoo saa tano.
nikaenda jmosi ile wakaniinterview saa saba akaniambia jtatu mapema uje kazini .
Mungu ni mwema nipo nae hapa sasa hivi tunaishi vizuri sana kweli tajiri hana roho mbaya .nampenda sana huyu mzee.

Kweli miss natafuta Bosi wa Kampuni anataka kukutumia nauli uje Dar akupe kazi??...yaani huu utaratibu wa bosi kutuma nauli huu!!!! Yaani anazama mfukoni anatoa nauli anakutumia!!!!!..dada zetu nyie aagh basi yaishe bana
 
kila siku nilikuwa nanunua gazeti la daily news ili kutafuta kazi .siku moja nikakuta kijarida cha ppra kimeandikwa matender waliyoaward kwa watu mbalimbali
nikaangalia kampuni ambayo ilikuwa imepewa tender kubwa nikaona moja ina bilion kadhaa. nikaingia mtandaoni nikatafuta contact zao
bahati nzuri kwenye website yao wameweka namba ya simu ya mkurugenzi .nikakuta kumbe yupo whatsup nikamtext akaniambia yupo nje ya nchi akija atanitafuta.siku moja akaniambia yupo dar ila anatafuta siku anitumie nauli .sikusubiria nauli nikaja dar nikamwambia nipo dar mzee.
akaniambia basi njoo jmosi tutakuwa wote mgt njoo saa tano.
nikaenda jmosi ile wakaniinterview saa saba akaniambia jtatu mapema uje kazini .
Mungu ni mwema nipo nae hapa sasa hivi tunaishi vizuri sana kweli tajiri hana roho mbaya .nampenda sana huyu mzee.
Hapa papuchi ilitumika kama collateral
 
Hii ya kuchukua docs za stationary, nakumbuka kuna wanafunzi nimewafanyia kazi ya kufoji vyeti pale SJUIT dom, pamoja na slips za malipo ya ada..naadae nikakuta wananifata hadi home usiku wa manane, nikaachaga hiyo kazi.. Ilaa ni shida
SJUIT ulimaanisha SJUT? Auu..by the way wote uliowafojia slip nilizozikuta niliwakamata na nikawarudisha mwaka wa pili na wakwanza
 
Mhh, unasema kweli?. SJUT ya camp David. Wapo waliorudi kunishukuru kwamba zilikubaliwa hivyo ada wakazila....wengine hawakurudi...kumbe ni wewe mhusika humu!. Habari sana
Nakuhakikishia ni kweli kabisa niliwakamata wengi saana, na kweli ada walikua wamekula..nikakuta wengine mpaka wamemaliza lakini walileta ada wakati wanaclear niliwakamata.
 
Nakuhakikishia ni kweli kabisa niliwakamata wengi saana, na kweli ada walikua wamekula..nikakuta wengine mpaka wamemaliza lakini walileta ada wakati wanaclear niliwakamata.
Heee, hatari. Mimi zangu nilikula nilizokuwa nawachaji. Sijui tukionana nao mtaani watanielewaje, hahahaaa!
 
Back
Top Bottom