THE SPIRIT THINKER
JF-Expert Member
- Sep 9, 2019
- 392
- 555
WATAALAMU wa anga hufurahia sana kupiga dunia picha wanapoiona ikiwa kubwa kupitia dirisha la chombo cha angani. “Huo ndio mwono bora zaidi unapokuwa angani,” akasema mmoja wao. Lakini dunia yetu huonekana kuwa ndogo sana ilinganishwapo na mfumo wa jua na sayari zake. Dunia zipatazo milioni moja zinaweza kutoshea ndani ya jua, na bado nafasi ibaki! Lakini, je, mambo hayo juu ya ulimwengu yanahusu maisha yako na maana yake?
Ebu tuelekeze uangalifu wetu kifupi katika anga na kuona uhusiano uliopo kati ya dunia na jua. Jua letu ni mojawapo tu ya nyota nyingi sana zenye kutazamisha zilizo sehemu ya kundi la nyota linaloitwa Kilimia (Milky Way), ambalo nalo ni sehemu ndogo sana ya ulimwengu. Kwa macho, inawezekana kuona madoa machache ya nuru ambayo kumbe ni makundi mengineyo ya nyota, kama vile kundi kubwa la nyota lililo maridadi linaloitwa Andromeda. Kilimia, Andromeda, na makundi mengine yapatayo 20 ya
nyota, yameshikamanishwa pamoja kwa nguvu za uvutano na kufanyiza fungu la makundi ya nyota, yote hayo yakiwa sehemu ndogo tu ya mkusanyo mkubwa wa mafungu ya makundi ya nyota. Ulimwengu una mikusanyo mingi sana kama hiyo, na mambo bado.Mafungu ya makundi ya nyota hayana mpangilio wenye utaratibu angani. Yakipanuliwa, yanafanana na tando nyembamba na mapovu makubwa yaliyo matupu yenye nyuzinyuzi zinazotokezea pande zote.
Huenda hilo likashangaza wengi wanaofikiri kwamba ulimwengu ulijitokeza wenyewe tu katika mlipuko mkubwa. “Kadiri tuwezavyo kuona kwa uwazi zaidi ulimwengu ukiwa na mambo mengi matukufu,” akata kauli mwandishi mmoja mkuu wa Scientific American, “ndivyo inavyozidi kuwa vigumu kueleza kirahisi tu jinsi ulimwengu ulivyopata kuwa hivyo.”
NITAENDELEA KUELEZEA HADI MWISHO LAKINI MNARUHUSIWA KUJADILI.
UFAFANUZI WA KUNDI LA NYOTA
(Milky Way)
Inachukua kilometa kwintilioni moja kuvuka Kilimia, yaani kilometa 1,000,000,000,000,000,000! Inachukua nuru miaka 100,000 kulivuka, na kundi hili moja la nyota lina nyota zaidi ya bilioni 100
Ebu tuelekeze uangalifu wetu kifupi katika anga na kuona uhusiano uliopo kati ya dunia na jua. Jua letu ni mojawapo tu ya nyota nyingi sana zenye kutazamisha zilizo sehemu ya kundi la nyota linaloitwa Kilimia (Milky Way), ambalo nalo ni sehemu ndogo sana ya ulimwengu. Kwa macho, inawezekana kuona madoa machache ya nuru ambayo kumbe ni makundi mengineyo ya nyota, kama vile kundi kubwa la nyota lililo maridadi linaloitwa Andromeda. Kilimia, Andromeda, na makundi mengine yapatayo 20 ya
nyota, yameshikamanishwa pamoja kwa nguvu za uvutano na kufanyiza fungu la makundi ya nyota, yote hayo yakiwa sehemu ndogo tu ya mkusanyo mkubwa wa mafungu ya makundi ya nyota. Ulimwengu una mikusanyo mingi sana kama hiyo, na mambo bado.Mafungu ya makundi ya nyota hayana mpangilio wenye utaratibu angani. Yakipanuliwa, yanafanana na tando nyembamba na mapovu makubwa yaliyo matupu yenye nyuzinyuzi zinazotokezea pande zote.
Huenda hilo likashangaza wengi wanaofikiri kwamba ulimwengu ulijitokeza wenyewe tu katika mlipuko mkubwa. “Kadiri tuwezavyo kuona kwa uwazi zaidi ulimwengu ukiwa na mambo mengi matukufu,” akata kauli mwandishi mmoja mkuu wa Scientific American, “ndivyo inavyozidi kuwa vigumu kueleza kirahisi tu jinsi ulimwengu ulivyopata kuwa hivyo.”
NITAENDELEA KUELEZEA HADI MWISHO LAKINI MNARUHUSIWA KUJADILI.
UFAFANUZI WA KUNDI LA NYOTA
(Milky Way)
Inachukua kilometa kwintilioni moja kuvuka Kilimia, yaani kilometa 1,000,000,000,000,000,000! Inachukua nuru miaka 100,000 kulivuka, na kundi hili moja la nyota lina nyota zaidi ya bilioni 100