Ulimwengu wa 3D na 4D

Imeharibu hata ladha ya JF

 
Tukubali tusikubali ... watu wengi ni wavivu wa kufuatilia mambo. Kikundi kidogo tu cha watu ndo wanafuatilia mambo na hao wanajua mengi zaidi na zaidi .. waliobaki wanakuwa bendera fuata upepo tu.
Hata wewe unayesoma hapa uliwahi kujiuliza swali hili ... "mkono kwa ajili ya kulia chakula ni mkono wa kulia" nani aliweka utaratibu huo?
 
Kila kitu kimegota na kusimama kwenye hiyo meyiiiiii meyiiiii.kw hiyo hata km utafuata hayo maelekezo mengine lkn ukakosea kwenye hiyo meyiiiii meyiiiii.hutafanya lolote.hivyo meyiii meyiiii ndio kila kitu.
Sometimes huwa nikisoma post nyingine nacheka hata nikiwa peke yangu .... ebu ijaribu hiyo Meyiiiiiii uone kama ina madhara yoyote.
 
Chochote kile unachokijua ni kwa sababu ulijifunza, hii inamaanisha kuwa ulichozaliwa nacho ni uwezo wa kujifunza tu. Tatizo uwezo huo unaendelea kupungua pale unapoendelea kuwa na umri mkubwa.
Mtoto mdogo uwezo wake wa kujifunza ni mkubwa sana kwa sababu kichwani kwake hana mrundikano wa mambo mengi. Wewe hapo kutokana na mrundikano wa mambo mengi ndiyo maana unakomaa na kubishia vitu vya ukweli eti mpaka upate evidence ... evidence ipi kwa vitu visivyoonekana kwa macho ya kimwili lakini vipo?
Wewe unayebishia hii kitu nakufananisha na mshamba mmoja anayeamini kuwa kwenye computer mambo yote ni keyboard tu eti kwa sababu ndo inayotumika saidi kwenye kuingiza data.
 
Hiyo Hollywood wanatengeneza picha zilizopo katika ulimwengu unaoonekana kwa macho na usioonekana kwa macho.
 
Hapa kila Mkristo anaamini kabisa kwamba Yesu alifunga siku 40 usiku na mchana pasipo kula kitu chochote. Ukimuuliza iliwezekanaje? anasema huyo alikuwa mwana wa Mungu; binadamu wa kawaida hawezi.

Huyo huyo utamsikia akiimba pambio eti ..
"Wote waliompokea aliwapa uwezo kuwa wana"
 
Sometimes huwa nikisoma post nyingine nacheka hata nikiwa peke yangu .... ebu ijaribu hiyo Meyiiiiiii uone kama ina madhara yoyote.
Sisemi kuwa ina madhara yoyote.ila nataka nijue huyoo meyiii meyiii ni nani ktk umimwengu huuu?,!! Na ana mamlaka yapi ktk ulimwengu huu mpk jina lake litumike kufungua mlango wa jicho la tatu?!!
 
Kwanza bro ungeyataja hayo mambo unayosema una anza kuyaona ili tuyajadili moja baada ya jingine tujue ukweli wake.

Pili,nini maana ya MEYIIIII na kwanini MEYIIIII ?

Ukishajibu nitakuja kukupa faida kubwa sana juu ya mambo hayo.

Kwa ufupi huo ni USHIRIKINA na unakupelekea katika upotevu.........

Narudi bro...... Elimu sahihi ni nuru na Ujinga ni giza.
 
Unapenda ku jibu nusu nusu ili uulizwe au...si ueleze kitu umalize
 
Asante Zurri kwa kuja nadhani tutajua mengi kuhusu huu Uzi
 
Jaribu kwanza ..
Unajua nashangaa kwa nini usijiulize kwa nini A inaitwa hivyo na wala sio Z
Hujajibu swali langu mkuu, ni bora utuambie maana ya maneno hayo kwanza kabla ya kuyatumia. Mimi naamini hayo maneno yana maana, siyo bure tu, na kama hayana maana basi inawezekana kabisa hilo likawa "jina" la kitu fulani au kiumbe fulani. Kama hujui maana yake basi usiwaambie watu wayatumie, inaweza kuwa hatari zaidi kuliko unavyofikiri wewe.

Fahamu kwamba ulimwengu wa "roho" umegawanyika mara mbili, kuna "Roho njema", na roho "wachafu", hizi roho chafu ni kama sumu, na sumu haijaribiwi kwa kuionja, utakufa. Itakuwa vipi kama hayo maneno(MEYIII) ni jina la roho mchafu na huyo roho akawaingia hao watakaomuita???
 
Aisee kweli nilitaka kujaribu labda ningeweza kuuambia mbuyu hama ukajipande baharini na ingekuwa kumbe fix wamarekani duh
 
kiongozi hakuna kitu kama hii.
sema "Meyiii" all day long hakuna kitakacho kukuta.
Hizi ni imani potofu. Na imani husababisha Brain ku react. ukiamini Nazi iliotupwa njia panda inadhuru na ukaikanyaga au kuiruka huenda ukadhurika Psychologically lkn kama huamini hii kitu hata wakikuwekea nazi Lori zima hakuna kitakachokukuta.

Imani ina athari kubwa sana ktk Ubongo.
na Ubongo ndio inayo control mwili wako wote. ukiathirika basi kila kiungo kinaathirika.

kuna watu through imani tu wanaweza kupona maradhi mengi kwa kunywa maji ya kawaida tu. kikubwa waaminishwe kuwa yale maji ni dawa KUU yenye kuponyesha hicho wanacho ugua.
 
Hayo madudu ya ajabu ajabu utakayoyaona nn faida yake mkuu
 
Kama mtu anapata kuwa na jicho la jini au la mzimu haumdanganyi kwa lolote labda wale matapeli tu.
 
Yote sawa! hata mimi nilikuwa mbishi kama wewe!
Hehehe alafu sasa hivi una third eye?
Nakushauri ukamuone daktari wa magonjwa ya akili aliyekaribu na eneo lako.
 
Kama mtu anapata kuwa na jicho la jini au la mzimu haumdanganyi kwa lolote labda wale matapeli tu.
hakuna kitu kama hii.
nani mwenye Jicho la tatu? nitajie mmoja tu.
manake Serikali yetu inahitaji watu kama hawa wakatuonyeshe majambazi wote na wizi wote mahala walipo tuwaondoe kabisa nchini ili askari nao wapumzike kidogo na sisi tupate kuishi bila wsws.

Hizo ni Holywood Movies my good friend.
hakuna mwenye uwezo wa kuona kinachokuja wala kilicho jificha. Na akidai ana uwezo huo huyo ni Tapeli tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…