eddy king
JF-Expert Member
- Apr 1, 2016
- 556
- 1,210
Nzuri, nimeipenda. Hapo ni Mungu alikua afanya njia bila ya wewe kujuaMimi tulikutana kwenye daladala tukiwa tunaenda interview basi la mwenge posta lilipofika moroco basi likaharibika na condakta akakimbia kurudisha nauli ilikuwa nipande likaharibikia kituoni.
Huyo kijana Akawa analia kuwa anaenda interview kule kule Mimi nlikuwa naenda kufanya interview hana nauli ingine nikambwambia usijali na mimi naenda nitakulipia. Kweli ikaja UDA tukapanda nikalipa
Tukafika posta tukashuka akasema nisubiri nakuja Toa photocopy za vyeti nipe nikatoa nikampa sikujali sababu muda wa interview ulikuwa bado sana na japo simjui sikujali sababu hakuchukua vyeti original
Baada ya muda akaja na mtu mzima pale nilikuwa akasema twende pembeni akaniambia maswali yote yatakayoulizwa interview na majibu
Kuingia nikamkuta nikajikausha kama simjui maswali yote nikakuta yaleyale nikayajibu vilevile nikapata kazi kumbe alikuwa mjomba wake
Hadi leo yeye simhesabu kama best friend bali ndugu