Ulijuaje mpenzi wako anaku-cheat, na kwanini?

Ulijuaje mpenzi wako anaku-cheat, na kwanini?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,406
Reaction score
19,361
Binafsi nakumbuka nlikuwa na girl friend ambae tulidumu, Nlizani nimepata kumbe nimepatikana (kwa sauti ya msanii 20% 😁).

Enzi hizo nlikuwa nasoma chuo cha uhasibu pale Arusha (I.A.A) mitaa ya Njiro huko kwa matajiri wa Arusha.

Nlikuwa mtu wa watu sana, washkaji kama wote na hiki ndicho kilinisaidia, marafiki zangu wa kike wakaanza kuniambia huyu dem wako tunamuonaga mida ya jioni anachukuliwa na gari, mi nikawapuuza na kuwaona wananizushia tu wana wivu japo trust yangu kwa huyu manze ilishuka.

Basi baada ya siku 3 nilitumiwa picha kibao za huyu ex wangu akiwa kiwanja flani akimpa burudani mwenye pesa zake, hizo picha moja kwa moja ziliashiria nshaibiwa inabidi nitulie ni move on.

Sikumwambia hii ishu ila tulipokutana nlimwangalia machoni na kumwambia kwanini anani cheat, alikataa kata kata na hapa ndipo nilipojua kwamba moyo wa mtu ni msitu.

Nilipomuonyesha zile picha hizo dharau za kunijibu kwa kujiamini ziliyeyuka, hakuwa na cha kusema zaidi ya michozi kumtoka, mda huo nlikuwa na hasira sana yani nmesalitiwa na bado nikadanganywa 😠😠, kila nkimwambia kwanini umenicheat kimya, nikamfukuza atoke.

Baada ya wiki ndio akaanza kuja chuo japo alikuwa ananikwepa sana, nilimcheki usiku na kuuliza swali lile lile, kwanini ulinicheat basi ndo akanipa makavu kwamba yote aliingia tamaa ya pesa kwasababu alikuwa anadaiwa ada na nyumbani kwao pesa hawana, hata boom nililozani analo aliniambia ukweli kwamba hakuwa na boom ila aliniambia hivi ili nisimuone mzigo.

Anyway tangu hapo huyu dem ndio ikawa tabia yake na akawa mdangaji sana kadri siku zinavoenda na bado hadi sasa anaendelea kudanga, kiukweli namuombea abadilike maana ashakuwa mraibu wa haya mambo yeye ni pesa tu.

Hii kitu iliniumiza sana, anyway nilipata cha kujifunza na ku move on maisha yakaendelea nikampata mpenzi mwengine ambae watu wake wa karibu wengi nilijuana nao.

Fundisho: Jaribu uwe na urafiki na watu wa karibu au wanaoishi na mpenzi wako, hii inasaidia sana, ningekuwa sina connection za marafiki zangu hao waliokuwa wanaishi na huyo ex wangu nisingegundua kabisa haya mambo ama ningechelewa.
 
Nikiwa kwenye mahusiano na mdangaji hata yeye lazima atakua anajua kua naijua tabia yake vizuri tu.
Kwahiyo nitamchukulia kama danga tu na mimi, na sita muacha danga wangu.. labda kwa sababu zingine tu..
Labda nimepata mwingine.

Kahaba unaendelea nae tu ila unatakiwa kumtumia kiakili, maana kuna magonjwa siku hizi.
 
Nikiwa kwenye mahusiano na mdangaji hata yeye lazima atakua anajua kua naijua tabia yake vizuri tu.
Kwahiyo nitamchukulia kama danga tu na mimi, na sita muacha danga wangu.. labda kwa sababu zingine tu..
Labda nimepata mwingine.

Kahaba unaendelea nae tu ila unatakiwa kumtumia kiakili, maana kuna magonjwa siku hizi.
Tatizo sie wengine kondom zinatubana mkuu huwa tunabutua hivyo hivyo
 
Sawa moyo una chaka kubwa hatujakataa!

Mimi hata kuwa na mshkaji tuu at first time huwa nimeshafahamu baadhi ya tabia zake 80% kupitia non verbal comm...movt + facial expression

siku zote zingatia ni kwa jinsi gani mtu anasema na sio kile anachokisema
 
Alikuambukiza gono, au klamedia au kisonono, maana hapo ndo dr alipokuthibitishia..!!
Hapana , ninatabia ya kwenda hosp moja tuu kila ninapoumwa labda niwe nje ya mji kwaajili ya records kipi niliumwa na kwa interval ipi, basi ikawa file langu ukiangalia kila baada ya miezi 2 au 3 nina U.t.i imagine kumeza antibiotica 30 kila baada miezi 2.
Dr kila siku ananipa somo la usafi na ninanazingatia usafi lkn tatzo liko palepale
Dr ndio akaniambia kati yenu kuna mmoja anauza mechi
 
Duh niliwahi achwa na nilipoteza 9 kilos ndani ya mwezi tuu
Haya mapenzi Haya
Pole,halafu unakuta wakati unaugulia mwenzio alishakufuta hata hakuwazi,najua maumivu ya aina hiyo,ubongo ungekuwa ni kama computer once mtu anakutenda una delete tu na kusonga mbele,ingekuwa rahisi sana,lakini kawaida huwa inachukua muda mpaka moyo ukate tamaa kabisa...
 
Back
Top Bottom