Ulevi wa mume unaelekea kuniharibia kazi

Ulevi wa mume unaelekea kuniharibia kazi

gilldenu

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2015
Posts
2,914
Reaction score
3,022
Wapendwa habarini,

Mimi ni mwanamke ila sasa nakutana na changamoto kwenye ndoa. Mwanaume hana kazi wala kipato chochote kile anachoingiza ila ulevi wa pombe ni January hadi December.

Ninachokipata kazini tunagawana ila ndo hivyo pombe lakini hilo halina shida bora alewe kwa starehe zake lakini swala linakuja ananiharibia hadi kazini kwangu.

Inafika kipindi ananifuata kazini kwangu na kutukana staff wenzangu kitu ambacho naona kitaniharibia kazi muda sio mrefu.

Naomba kama kuna msaada naweza pata mahali ili nilinde kibarua changu maana ndo kinachotuweka mjini. Naombeni msaada wenu na ukizingatia kibarua chenyewe nafanyia kanisani na kanisa na hayo mambo ni tofauti.
 
Kuna wanaume wa hovyo jaman, pole sana dada. Waweke tu wazi hapo kazini tabia za jamaa, ukiweza hama home halafu nenda kituoni.

Hauna Kaka au ndugu wa kukusakdia ku deal na Jamaa? Siwezi kubali Dada yangu ateseke hivyo, kama una Kaka au vipi hemu ongea nao wakusaidie.

Upo mkoa gani?
 
Mumeo ana shida kiroho na kimwili, tafuta msaada wa maombi na cancelling kwake
Usimchoke huyo ni mume wako!
Hakikaa manabii wataendelea kutajirika kwa akili kama hizi. Atafute msaada wa maombi! Kwanini yeye asiombe mwenyewe? BTW shida kama hizi kuzileta hapa hutapata ushauri mzuri kwani watu hawajui undani wenu na wamesikiliza upande mmoja. Kwanini unaogopa kuitisha kikao cha familia? Nina wasiwasi huko kanisani una uhusiano na ''mtume'' ndiyo maana mumewe anakwenda kutukana huko na wewe unaogopa kumshtaki kwa wazee.
 
Kuna wanaume wa hovyo jaman, pole sana dada. Waweke tu wazi hapo kazini tabia za jamaa, ukiweza hama home halafu nenda kituoni.

Hauna Kaka au ndugu wa kukusakdia ku deal na Jamaa? Siwezi kubali Dada yangu ateseke hivyo, kama una Kaka au vipi hemu ongea nao wakusaidie.

Upo mkoa gani?
Hapa umesikiliza maneno ya upande mmoja. Pengine hadithi ni tofauti kabisa kama utasikia maelezo ya mumewe. Na pengine mumewe amegeuka kuwa mlevi kwa sababu yake. Na pengine anakwenda mpaka kazini kutukana kwa sababu kuna mwanamme wake! Haya ni mawazo yangu tu lakini....
 
Hii stori ni ya upande mmoja. Wanawake sio wa kuwaamini sana na hizi stori za kusikia upande wao.

Kuna uwezekano jamaa now hana kazi, unamsumbua na hata kazini amekuja kuchenchia sababu ya uhusiano wako na wanaume wengine.

Naona umemkomalia kuhusu ulevi wake yeye kutokua na kazi. I believe there is more to this story
 
Hakikaa manabii wataendelea kutajirika kwa akili kama hizi. Atafute msaada wa maombi! Kwanini yeye asiombe mwenyewe? BTW shida kama hizi kuzileta hapa hutapata ushauri mzuri kwani watu hawajui undani wenu na wamesikiliza upande mmoja. Kwanini unaogopa kuitisha kikao cha familia? Nina wasiwasi huko kanisani una uhusiano na ''mtume'' ndiyo maana mumewe anakwenda kutukana huko na wewe unaogopa kumshtaki kwa wazee.
Makanisa ya katoliki, sabato, pentecoste, anglicana kote wanatoa msaada wa maombi,
"Unataka aombe mwenyewe" sio kila mtu ana kipaji cha kuomba, muda mwingine msaada ni muhimu.
 
Hapa umesikiliza maneno ya upande mmoja. Pengine hadithi ni tofauti kabisa kama utasikia maelezo ya mumewe. Na pengine mumewe amegeuka kuwa mlevi kwa sababu yake. Na pengine anakwenda mpaka kazini kutukana kwa sababu kuna mwanamme wake! Haya ni mawazo yangu tu lakini....


Mpaka mumewe naye atokee ninaamini maneno yake.
 
Hii stori ni ya upande mmoja. Wanawake sio wa kuwaamini sana na hizi stori za kusikia upande wao.

Kuna uwezekano jamaa now hana kazi, unamsumbua na hata kazini amekuja kuchenchia sababu ya uhusiano wako na wanaume wengine.

Naona umemkomalia kuhusu ulevi wake yeye kutokua na kazi. I believe there is more to this story
Kweli mkuu,...mwanaFA alisema "usimwamini mwanamke hata kama unamtania"...
 
Inaonekana pia kuna ka manyanyaso fulani anapitia toka kwako,kwaio wewe tumeshakusikiliza aje nayeye tupate ya upande wa pili,ili tatizo lisuluhishwe ukiona mwanaume yuko hivyo ujue kuna shida mahali,na pia kukosa kipato ndio kuna mfanya awe hivyo maana pia hajiamini lazima atakua mkorofi mkorofi....pambana nae mfungue kamradi asimamie atatulia tu,halafu mwamini MUNGU
 
Back
Top Bottom