SONGOKA
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 1,836
- 1,845
nachukia watu wanaoandika bila kuwa na statistics , toka lini mapato ya utalii Kenya yakawa makubwa kuliko Tanzania???Masikini Tanzania!, tunashindwa kuchangamkia hizi fursa, kwa sababu kwa mujibu wa kanuni za kimataifa za usafiiri wa anga, ni nchi husika tuu ndio yenye uhusa kurusha direct flight kutoka nchi moja hadi nchi nyingine!.
Right yetu ya kutua UK ilichukuliwa na Alliance Air, kampuni hii ilikuwa ni ubia kati ya serikali ya Tanzania na shirika la ndege la Afrika Kusini SAA, ushirikiano ulipovunjwa, route yetu ikamilikiwa na SAA kwa vile hatukuwa na ndege wala uwezo wa kurusha ndege kwenda UK!. Ila sasa hata Tanzania ikipata uwezo wa kurusha ndege yetu kupeleka UK, bado tutakumbwa na tatizo la ng'ombe wa masikini hazai!, maana ndege hiyo itakamatwa mara tuu itakapotua London as an attachment ya kufidia kuikamata ile meli meli ya samaki wa Magufuli, na kushikiliwa hadi tulipe fidia ya meli ile iliyoozea Bandai ya Dar!.
Wakati haya yakiendelea, wenzetu Kenya, wanajenga uwanja wa ndege wa kimataifa kwenye kingo za Mlima Kilimanjao upande wa Kenya pale Holili!, kutoka hapo ni 30 minutes drive mpaka sehemu ya kupandia mlima Kilimanjaro pale Marangu, ambao unapandwa kwa upande wa Tanzania tuu!. Kutoka KIA hadi Marangu pale pa kupandia mlima Kilimanjaro ni 1 hr drive, hivyo uwanja wa Kenya ukikamilika, watalii wanaopitia Kenya, watapanda kwa haraka zaidi mlima Kilimanjaro kuliko wanaopitia Tanzania!, by then Nchi za Afrika Mashariki tutakuwa nchi moja!, hivyo visa ni moja tuu!, what chances do we stand?!
Hapa tulipo tuu, Tanzania ndio ina vivutio vingi vya utalii kuliko Kenya, lakini Kenya ndio inayoongoza kwa pato la utalii!, wengi wa watalii wanaokuja Tanzania, wanakuja kwa kupitia Kenya, na wanawajibika kulipia double visa kuingia Tanzania!, sasa just imagine kwa sasa kuingia Tanzania ni kwa visa lakini watalii wengi wanapitia Kenya, jee visa zikiondolewa hali itakuwaje?!.
Usafiri wa anga na uhamasishaji utalii ni changamoto kwa serikali ya JPM!.
Pasco
2013 Kenya total receipt 1.1 billion USD
2013 Tanzania total receipt 1.9 billion USD
2014 Kenya total receipt 1.5 Billion USD
2014 Tanzania total receipt 2.0 Billion USD
average expenditure per day per tourist Kenya 204 USD
Tanzania 317 USD per day
GDP contribution Kenya 4.8 %
Tanzania 17%
Pasco nakuheshimu, jifunze kuandika kwa kutumia data
Kenya wanachotuzidi ni idadi ya watalii ambapo wanapata average ya 1.7 million tourists annually wakati Tanzania tunapata 1.2 million annually (2014 stats). na hii inasababishwa na policy yetu ya "low volume high yield"
wakenya policy yao ni "mass tourism"