Ukweli wa Kiini cha Mgogoro wa Waisrael/Wayahudi na Wapalestina

Haya mambo yenu yanachanganya tu. Mwingine mara anadai waisrael ni weusi, wengine Israel taifa teule. Pambaf watu weusi!

Hayo ma vitu yenu huwa siyaamini. Ninachoamini Mungu yupo na amewapa neema wengine kama mtihani tu kama watashukuru au watakufuru. Kwa maneno mengine naweza ku-declare Israelis ni watu so intelligent na wana play part kubwa kwenye historia ya ulimwengu lakini hiyo haimaanishi wao ni bora kuliko wengine. Hiyo ni mitihani ya Mungu kwa wanaadamu.
Nimependa post yako mkuu
 
Mahangaiko ya bure tu haya. Hutaokoka kwa kuipenda Israel au kuichukia, bali utaokoka kwa matendo yako. Pia kumbuka Israel wanavopewa nchi ya Kanaan sio kwamba ilikuwa empty, kuna watu walikuwa wakiishi ambao mm na ww hatuwajui. Kwann Mwenyezi MUNGU aliwapeleka hapo wakati palikuwa na watu, hilo ni suala ambalo Mwenyezi MUNGU mwenyewe ana makusudi, Mwenyezi MUNGU akitaka kutimiza kusudi lake hufanya atakavyo. Suala la wayahudi kumkataa Yesu sio lako ni la kwao na Mwenyezi MUNGU, na wanaendelea kumuabudu MUNGU yuleyule waliyemuabudu tangu enzi na enzi bali ww ndio unaabudi tofauti na wao. Ni vyema ukajifunza kumcha Mwenyezi MUNGU acha kuhangaika na dini.
Kama ni mjadala wa historia na siyo kiimani tafakari yafuatayo;
1. Torati kitabu cha wayahudi ndiyo kumbukumbu ya kwanza ya Mungu wa Ibrahim. Biblia ya kikristo, hasa agano la kale, imetokana na Torati.
2. Koran ya Waislamu, ambao ulikuja miaka 600 baada ya Kristu, ina maandiko mengi ambayo yanashabihiana na Biblia na Torati,

Je, haiwezekani kuwa waandishi wa nyuma.walikuwa wanaazima au kunakili kutoka kwa waliowatangulia?
Ndg yangu GuDume, nimeifwatilia hili andiko lako na kugundua ni andiko lililokosa ukweli wa kikamilifu na limejaa uwongo na uzushi na hii si kwa koza lako la makusudi bali ni kwa sababu hatujawai ilezwa na kutafiti ukweli.

Kwanza naanza kukuonyesha uzushi na uwongo wa andiko lako: Mosi, WAYAHUDI ni kabila la YUDA kati ya makabila 12 ya wana wa ISRAEL (IS-RA-EL) ambao hio ardhi haikuwa yao: kukuonyesha ardhi haikuwa ya kwao tunasoma KITABU CHA MWANZO sura ya 10: SUMMARY YA MATAIFA WAKATI WA NUHU:View attachment 381386
View attachment 381388
View attachment 381389

Hivyo ile ardhi kutokana na maandiko ya kitabu cha mwanzo na kitabu cha Jubilees (ambao wengi hawakijui kama ni kitabu kimoja wapo cha biblia) kinaeleza ardhi hio ya Afrika ya Kaskazini Mashariki ni ya WAKANAANI ambae alikuwa mtoto wa HAM na si SHAMU.

Pili: KITU MUHIMU CHA KUKIFAHAMU NI KWAMBA, WAYAHUDI WALIKUWA WEUSI na WATABAKIA KUWA WEUSI TU. NA NDIVYO WALIVYO KWA WAARABU, WAISRAELI (WAEBRANIA, WAYEMEN, WAYAHUDI). ILI KUJUA HAWA WATU WALIKUWA WEUSI, TUNASOMA CHANZO CHETU CHA BIBLIA wewe mwanzilishi wa maada hii umekitumia, tusome Nimrod ambae alikuwa mwanzilishi wa falme ya babel ambae ni utukuu wa NUHU Ujukuu wa HAMU na mtoto wa KUSHI, katika kitabu cha mwanzo sura ya 10, mstari wa 9-14, inamuelezea huyu NIMROD ambae katika historia NIMROD alimuajiri baba wa ABRA-HAMU kuwa mshauri wa mambo ya Kiroho kwakuwa alikuwa ni kati ya ndugu kwa babu yake mkubwa SHAMU. kwahio HIMAYA ZOTE DUNIANI ZILIJENGWA NA KIZAZI CHA HAMU KWANZA. REJEA KUSHITIC EMPIRE, EGYPTION EMPIRE, PERSIAN EMPIRE, BABYLONIA EMPIRE (NINEVAH, LAND OF ACCAD and SHINAR).

Tatu: kuhusu jinsi ulivyochambua juu ya jina la ardhi hiyo kama sio ya wapalestina (Philistinites), pamoja na majina kubadilishwa mara kwa mara, bado uhalali wa kuwa mwenye ardhi ni MKANAANI maana WAFILIPI ni wajukuu wa Kanaani, rejea biblia. Na kwa ushahidi huu MYAHUDI NI MTU MWEUSI ambao ni labda wamerika weusi, wewe ama na mimi kwa sababu kwa sababu wengi waliuwawa na wengine walikimbia kuishi AFRIKA na baadae kupelekwa Utumwani. STILL WE ARE SCATTERED, WALIOKO PALE NI IMPOSTORS JEWS AU ISRAELIS(WAYAHUDI WA UWONGO) ingawaje wachache walibaki majangwani, na wengine wanarudi taratibu hasa wanaishi Monna, soma ufunuo wa Yohana Sura ya 2.9, 3.9.

USHAHIDI NI HUU:







NITAENDELEA...........


Hawa sio WAISRAELI ASILI (BIOLOGICAL ISRAELITES) NI ESRAELIS BY FAITH. HAWA NI WAKAIZARIA KUTOKA KHAZAR'S EMPIRE (GEORGIA, UKRAINE NA ROMANIA). Ni Vipandikizi vya wazungu wote maana ULAYA hawakutakia ndipo wakaamua kuwadampu Ardhi ya Wakanaani.
 
Kama ni mjadala wa historia na siyo kiimani tafakari yafuatayo;
1. Torati kitabu cha wayahudi ndiyo kumbukumbu ya kwanza ya Mungu wa Ibrahim. Biblia ya kikristo, hasa agano la kale, imetokana na Torati.
2. Koran ya Waislamu, ambao ulikuja miaka 600 baada ya Kristu, ina maandiko mengi ambayo yanashabihiana na Biblia na Torati,

Je, haiwezekani kuwa waandishi wa nyuma.walikuwa wanaazima au kunakili kutoka kwa waliowatangulia?
Mim binafsi sina tatizo na torati, Injili, zaburi wala Quran. Titizo ni jinsi tunatafsiri neno hilo kwa mahaba yetu binafsi ya kidini hadi tunasahau hata maandiko yenyewe yalikuwa na lengo gani. Lengo halikuwa kuwagawa watu bali ni kuwaongoza ktk njia iliyo sawa. Suala la mitume na manabii, kiukweli wote walikuja na ujumbe mmoja tu wa kuonya watu wasiabudu vitu wasivyovijua na pia walifundisha sheria zitakazo wafanya watu waishi kwa amani. Mitume wengi hawakuja na jipya bali walikuja kukumbushia ujumbe ambao wenzao walishauleta ila umepuuzwa. Mapya yalikuwa machache na mengi ni yaleyale.
 
Naomba tujadili kwa facts za kweli na sio hisia zako juu ya jambo fulani.
Nazani wengi hawajui kuwa mitume na manabii walikuja na ujumbe mmoja/sawa kuanza Adamu hadi Mohammad(s.w.a) kuabudi Mungu mmoja tu.Pia tujue kuwa vitabu vyote vilikuwa na ujumbe unaofanana,lkn pia tujue kuwa vitabu vilitokana na Mungu mmoja.
qoran ni mchanganyiko wa vitabu vinne kama sijakosea mtanirekebisha
1)zaburi nabii daudi
2)Torati nabii mussa(a.s
3)injili(issa bin maryam (a.s
4)qoran muhammadi(s.a.w.
hebu angalia aya hii
qoran 2:87 Na hakika tulimpa mussa kitabu na tukafuatisha baada yake mitume wengine na tukampa issa mwana wa mariamu,hoja zilizo waziwazi na tukamtia nguvu kwa roho mtakatifu.Basi kila walipowafikieni mitume kwa yale ambayo hayapendwi na nafsi zenu mlijivuna----
surat al bakarah2:89 Na kilipo wajia kitabu kitokacho kwa Mwenyezi mungu kinachothibitisha waliyonayo na wao walikuwa wakitafutia ushindi kuwashinda.Yalipo wajia yale waliyokuwa wakiyajua waliyakanusha.
mtazamo wangu.waislael au ban islael ni watu walitajwa sana ktk qoran sura mblmbl ni kweli hawa jamaa walibarikiwa sana na Mungu ila walikanusha ishara hvyo walilaniwa.qoran 2:111 Na walisema hataingia peponi ila aliyekuwa myahudi au mkristo.Hayo ni matamanio yao Sema leteni ushahidi kama nyinyi ni wasema kweli.
soma qpran 2:121-122 Wale tuliowapa kitabu wakakisoma kama ipasavyo kusomwa hao ndio kweli wanakiamini na wanaokikataa basi hao ndio wenye kukhasiri.Enyi wana wa israeli!Kumbukeni neema yangu niliyokuneemesheni,na hakika Mimi nikakufadhilisheni kuliko wengine wote.
nakuomba kma unajubu jiubu kwa hoja zilizo wazi sio maneno matupu.
 
Mkuu kuhusu waisrael kuletwa Uganda ni Mungu alisema au mwanadamu?Kama mleta mada alivyoshauri kama si mkristo walau soma biblia kama kitabu cha historia unaweza pata kitu.Nchi ya ahadi baba zao walimiliki na Israel wakaonywa wasipotii watatawanywa katikati ya mataifa,hicho kikatpokea.Then Mungu akawakusanya kutoka huko walikokuwa kurudi nyumbani kwao kwenye nchi ya ahadi.
Umesema Isarel inechukuiwa na dunia nzima that is generalization,lakini wewe unadhani kwanini Israel iwe ni habari dunia.Wamefanya mangapi mabaya kama watu wanavyosema lakini mbona taifa hilo teule bado lipo?Iran analiita ni uvimbe unaweza tumbuliwa muda wowote lakini bado lipo,tena kwa taarifa yako Isael wote wangempokea Yesu na kuenenda katika njia za Mungu lingekuwa ni taifa linalotisha duniani.Sasa hivi kama hujui hata marekani wako close na Wayahudi kwa ni hujui sababu ni nini?amelaaniwa atakayeilaani Israel,si uwaangalie wanao ichukia Israel wako katika kipindi gani sasa hivi.Open your eyes and see.
Hapo sawa kabisa mkuu... Umenena
 
Mungu anatoa amri Binadamu aue Binadamu wenzake at the same time kuna amri ya usiue kwenye amri zake 10?
Mkuu unaelewa maana ya agano ni nini?Unajua kuna agano la kale na agano jipya?Unjaua Yesu alivyokuja alisema hakuja kuitengua torati bali .....Kasome biblia vizuri agano la kale na jipya.
 
sikuja kutengua torati bali kutimiliza.Agano la kale ndio lilikuwa sahihi ila jipya linamapungufu mengi xn
 
Mahangaiko ya bure tu haya. Hutaokoka kwa kuipenda Israel au kuichukia, bali utaokoka kwa matendo yako. Pia kumbuka Israel wanavopewa nchi ya Kanaan sio kwamba ilikuwa empty, kuna watu walikuwa wakiishi ambao mm na ww hatuwajui. Kwann Mwenyezi MUNGU aliwapeleka hapo wakati palikuwa na watu, hilo ni suala ambalo Mwenyezi MUNGU mwenyewe ana makusudi, Mwenyezi MUNGU akitaka kutimiza kusudi lake hufanya atakavyo. Suala la wayahudi kumkataa Yesu sio lako ni la kwao na Mwenyezi MUNGU, na wanaendelea kumuabudu MUNGU yuleyule waliyemuabudu tangu enzi na enzi bali ww ndio unaabudi tofauti na wao. Ni vyema ukajifunza kumcha Mwenyezi MUNGU acha kuhangaika na dini.
Mkuu naona kama umeharakisha sana,ungekuwa unasoma my previous posts ungejua mimi ni mtu wa aina gani.Mimi si mtu wa dini kama unavyoniwazia wala sijasema naweza okoka kwa kuipenda isarel.Learn to read between lines,wala sijasema wayahudi kumkataa Yesu ni swala langu naona kuna mambo unaongeza sijui unayatoa wapi.Mimi nimeelezea kilicho katika biblia,wayahudi walimkataa Yesu kama ni messiah kwa sababu wao waliona kuna vigezo hakuvikamilisha.

Kama mtu humjui soma post zake walau upate some clue siyo unakuja out of a blue unaanza kuandika unayoyawaza juu yake.Ni uhuru wako siwezi kukuzuia kuandika kilicho ndani ya moyo wako ,in a nutshell you got me wrong.
 
Ndg naona mnaogelea bahari kuu wakati kiwango cha maarifa yenu ni vidimbwi. Taifa la waisraeli bado halijajengwa. Maana vita ya Ammagedon bado haijatokea. LILE SIO TAIFA LILILOONGELEWA KWENYE BIBLIA BALI NI SYNAGOGUE LA SHETANI, SOMA UFUNUO WA YOHANA 2:9 AMA 3:9.

WAISRAEL HALISI WAPO WACHACHE SANNA PALE NA HAWANA SOCIAL POWER, WAISRAEL WENGI BADO WAKO NJE YA PALE. Watu weusi wenye nywele za pilipili (kinky, nappi, whorl hair) yaani mim na wewe na wengineo.

Wale wanalindwa na Marekani na Ulaya yote maana ndio iliowaweka pale kwa maslahi yao ya pamoja kuhadaa ulimwengu.

Hawana legitimate ya ardhi ya pale. Wenye ardhi ni wale weusi wasio na mamlala ya kiutawala na wengine hawapo kabisa. Hawakuwapo mwanzo na hawatakuwapo mwisho.

Soma Kumbukumbu la torati sura ya 28:68.... ujue musa aliwaeleza nini true israelites kitakachowatokea, ndipo utafahamu nani anafit maandiko hayo.
REJEA PIA ZABURI YA 83:1-18 NI NANI WALIJADILI KUWATAWANYA WAISRAELI WASIJEKUKUMBUKWA KAMA NI TAIFA LILILOKAWEPO DUNIANI. CHECK BERLIN CONFEENCE NA VATIKAN WAMEWAFANYIA NIN WATU WEUSI.

YESU ALISEMA ISHARA OJA WAPO YA KUJA KWAKE KAMA NI KWELI NI PALE UTAKAPOONA MTI ULIOKAUKA UNAANZA KUCHIPUA NA UJUE NDIO UFSLME WA MBINGU UNAKARIBIA.

TUJADILI HILI: KAMA WAO NDIE WAISRAEL WA KWELI MBONA WAMEJIKUSANYA WAO NA SII MUNGU NA WAKAUNDA TAIFA LAO MBONA YESU HAJAJA? HUU NI UNABII WA UONGO. REJEA UFUNUO WA YOHANA SURA YA 2:9

NITAENDELEA......
Mkuu ningependa nijifunze kutoka kwako angalia sentensi zako nilizo weka red,
Unamanisha taifa la Israel litajengwa kabla au wakati wa vita vya Armageddon?Je unaweza tueleza vita vya Armageddon ni vita vya aina gani au vitapiganwa wakati gani kibiblia?
Katika zaburi 83:1-18,pale imetajwa nchi ya Ashuri?Je unajua Ashuri ni nchi gani kwa sasa?Na kama unaijua hiyo Ashuri mahusiano yake na Isarel yako katika ulimwengu huu?
Naomba ufunguke kidogo kuhusu ishara ya kuja kwa Yesu alipose "mtakapoona mti uliokauka unaanza kuchipua" hapa najua ni fumbo,ebu funguka alimanisha nini .
 
Mkuu ningependa nijifunze kutoka kwako angalia sentensi zako nilizo weka red,
Unamanisha taifa la Israel litajengwa kabla au wakati wa vita vya Armageddon?Je unaweza tueleza vita vya Armageddon ni vita vya aina gani au vitapiganwa wakati gani kibiblia?
Katika zaburi 83:1-18,pale imetajwa nchi ya Ashuri?Je unajua Ashuri ni nchi gani kwa sasa?Na kama unaijua hiyo Ashuri mahusiano yake na Isarel yako katika ulimwengu huu?
Naomba ufunguke kidogo kuhusu ishara ya kuja kwa Yesu alipose "mtakapoona mti uliokauka unaanza kuchipua" hapa najua ni fumbo,ebu funguka alimanisha nini .
Mkuu ningependa nijifunze kutoka kwako angalia sentensi zako nilizo weka red,
Unamanisha taifa la Israel litajengwa kabla au wakati wa vita vya Armageddon?Je unaweza tueleza vita vya Armageddon ni vita vya aina gani au vitapiganwa wakati gani kibiblia?
Katika zaburi 83:1-18,pale imetajwa nchi ya Ashuri?Je unajua Ashuri ni nchi gani kwa sasa?Na kama unaijua hiyo Ashuri mahusiano yake na Isarel yako katika ulimwengu huu?
Naomba ufunguke kidogo kuhusu ishara ya kuja kwa Yesu alipose "mtakapoona mti uliokauka unaanza kuchipua" hapa najua ni fumbo,ebu funguka alimanisha nini .

Ndg, kwanza kabla sijakuhabarisha, napenda unifahamu kwamba MIMI SI MUUMINI WA DINI YEYOTE. MIMI NI MWASILIA (TRADITIONALIST) AMBAE HUISHI KWA KUFWATA AFRIKAN UNBROKEN SPIRIT WAYS OF LIFE (LIVING), I AM THE SPIRITUAL BEING, AND NOT A RELIGIOUS BEING.
Tukirejea juu ya vita ya Armageddon: Hii ni vita ya mwisho ya utawala wa kishetani duniani (kisiasa na kidini) dhidi ya wateule wa Mungu. Vita hii itakayoongozwa na Yesu Mwenyewe na Jeshi la Malaika pamoja na Wateule wa Mungu wa Majeshi dhidi ya majeshi ya mataifa wanaomti shetan mkuu watakapojikusanya kufanya vita kwa lengo la kuangamiza wateule wa Mungu wa Majeshi.

Hapa ndipo anguko la utawala dhalimu na ovu (kisiasa na kidini) na kuwekwa kwa utawala wa kiroho hapa duniani (ndipo dunia ile ya zamani itapita na kuzaliwa upya na ufalme wa mbingu kuwa hapa duniani. Taifa litakaloundwa chini ya utawala wa kiroho ni taifa la IS-RA-EL. SOMA ZABURI 2:2, DANIEL 2:44, UFUNUO WA YOHANA 16:14-1, 19:7-21, EZEKIEL 39:7.

ISHARA YA KUJA KWA UFALME WA MBINGU NI PALE UTAKAPOONA MTI ULIOKAUKA UKICHIPUA. HII NI KWAMBA, TAIFA LA WANA WA IS-RA-EL LILIPOPOKUTISHWA, NIKAMA TAIFA LILILOKUFA NA WATU WAKE NI KAMA MIFUPA ILIOKAUKA. SOMA EZEKIEL 37:1-14
KUCHIPUA NI PALE WATU WALIOKUFA NA MIFUPA YAO ILIOKAUKA KATIKA BONDE LENYE MIFUPA MIKAVU, WATAANZA KUAMSHWA KWA KUJITAMBUA, KUJIFAHAMUMUHIMU WA UWEPO WAO NA WAJIBU WAO WAKULETA UTAWALA WA MBINGU HAPA DUNIANI.

HAPA UAMSHO WA WATU HAWA UTAKUWA KIKWAZO KWA WATAWALA WA KISIASA NA KIDINI KTK DUNIA HII AMBAO KADRI YA ZABURI 83 WALISEMEZANA KULIFUTA TAIFA HILO NA KUJITWALIA MAHALI PAO PATAKATIFU (UKRISTO NA UISLAMU= VATIKANI NA MAKKA, BADALA YA YERUSALEMU), REJEA BERLIN CONFERENCE NA KUSAMBARATISHWA KWA HIMAYA NYINGI ZA WATU WEUSI AFRIKA NA BIASHARA YA UTUMWA ILIOTABIRIWA KUMBUKUMBU LA TORATI 28:68......


Rejea Zephaniah 3:10, From beyond the rivers of Ethiopia my suppliants, even the daughter of my dispersed, shall bring mine offering.
Psalm 68:31
Envoys will come out of Egypt; Ethiopia will quickly stretch out her hands to God.
Isaiah 19:19
In that day there will be an altar to the LORD in the midst of the land of Egypt, and a pillar to the LORD near its border.

Isaiah 19:21
Thus the LORD will make Himself known to Egypt, and the Egyptians will know the LORD in that day. They will even worship with sacrifice and offering, and will make a vow to the LORD and perform it.

Isaiah 45:14
Thus says the LORD, "The products of Egypt and the merchandise of Cush And the Sabeans, men of stature, Will come over to you and will be yours; They will walk behind you, they will come over in chains And will bow down to you; They will make supplication to you: 'Surely, God is with you, and there is none else, No other God.'"

KUHUSU ASSUR/ ASSHUR HILI NI TAIFA AMA DOLA YA SYRIA. NI DOLA ILIOKAWA KATIKA ENEO LA LEO IRAQ, KUWAIT NA SYRIA. KUMBUKA HILI ENEO LILIKUWA LINAKALIWA NA MAKABILA MENGI LAKINI YA WATU WEUSI TUPU. HIVYO HAYA MAKABILA YALIOKUWA YANAKAA KTK DOLA YA ASSUR WALIWASAIDIA PIA WAANA WA LUTU NA GOMER KUWATAWANYA WANA WA IS-RA-EL.




NITAENDELEA........
 
Mnepa sikuwa nimesoma andiko lako jingine nilipouliza maswali yangu.

Unaonekana unaelewa historia kiasi fulani ktk Biblia. Lakini kwa makusudi umeshindwa kuconnect historia ya waisrael na Canaani kwa mujibu wa Biblia. Je unajua nini kuhusu Musa na Joshua in connection with Caanan/Palestina na Waisrael?

Ninapenda kukujuza kwanza mim sio muumini wa dini hizi tatu ambazo huitwa Ibrahimic religions or religions of ibrahimic faith.
Ila ninafahamu kwa kiina sana historia za kitafiti za dunia yetu na umuhimu wa ufahamu wa historia inavyoakisi maisha yetu siku zote kama WATU WEUSI KOTE DUNIANI (WALIOKO KATIKA PEMBE ZOTE NNE).

KUHUSU HISTORIA YA MUSA NA HARUNI, HAWA KAMA WALIKUWAPO, WAWEZA KUWA NI KATI YA KOO ZETU ZA KIAFRIKA HIZI ZA SASA. KWANINI NASEMA HIVI, KWA SABABU MUSA NA HARUNI WALIKUWA WEUSI KAMA SISI NA MUSA ALIOA MMIDIAN OR MKUSHI PIA (KUTOKA ETHIOPIA). MIRIAM AMBAE DADA WA MUSA ALILAANIWA NA MUNGU KWA KUPEWA UKOMA SABABU YA HUYO MWANAMKE HUYU MKUSHI (MUETHIOPIA) OR MMEDIAN.

MAHUSIANO YAO NA WAKAANAANI NI KUWA HAWA NI FAMILIA ILIOKASAMBAA NA KUKUA KATIKA KOO NA MATAIFA MBALIMBALI AMBAYO DAIMA YALIKUWA NA SOCIAL AND LAND CONFLICTS. NI FAMILIA PANA AMBAYO WALIKUWA WANAOLEANA KWA KUJUA NYUMBA HII NI YA NDUGU YANGU.
KUMBUKA ABRAHAMU ALIPOTOKA MISRI NA LUTU ALINUNUA ARDHI KWA NDUDU YAKE MKANAANI KWA AJILI YA FAMILA YAKE.

KITABU CHA BIBLIA KIMEANDIKWA NA MABABU ZETU WEUSI KUELEZEA JAMII ZAO ZA KALE KWA FAIDA YETU KWA MAANA WALIJUA KITAKACHOTOKEA KWETU NDIO MAANA KULIKUWA NA UNABII (FORESEEN THINGS AND EVENTS TO HAPPEN).
UKIENDA MISRI AMBAPO JINA LENYEWE LIMETOKANA NA MTOTO WA HAMU ALIEKIITWA MISRIAM, KWENYE MAPIRAMIDI HADITHI NYINGI YA TAWALA NA MAMLAKA YA HIMAYA MBALIMBALI ZA WEUSI ZIMEONYESHWA ZILIKUWA ZINAPIGANA WENYEWE KWA WENYEWE.

HIVYO HUWEZI WATENGANISHA WAKANAANI NA WAEBRANIA, WA KUSHI, WA ASSURI NA WA MISRI, WAAJEMI NA WABABELI NI FAMILIA ILIOKASAMBAA NA KUWA MATAIFA.

HAWA WALIEKO KTK NCHI HIZI ZA AFRIKA KASKAZINI MASHARIKI SI WAESRAEL HALISI NI WA IMPOSTORS KAMA VILE WALIVYO WAARABU IMPOSTORS. MAANAA WAARABU HALISI NI WABEDUI AMBAO NI WEUSI NA BROWN.

ULE ULIMWENGU PALE UMEVAMIWA KAMA WALIVYOVYAMIA MISRI, LIBYA, TUNISIA, MOROKO , ALGERIA NA SUDAN (SO-YUDA-N=LAND-OF YUDANITES=WAYAHUDI).

WAKAJIMILIKISHA HERITAGE ZISIZOWAHUSU NA WENYE URITHI ULE NI BANTUS (BANTHUEL) AMBAO KWA MAVITA YA MARA KWA MARA WAKALAZIMIKA KUYAHAMA NA KUJA D0WN SOUTHERN SAHARA.
 
ukitaka kuielewa vizuri historia hii weka imani yako pembeni. ukija na imani,itikadi,chuki na msongo huwezi ukaelewa. kama ukiweza kunambia nlichopotosha ntashukuru sana. Ukija ukasema tu kuwa nmepotosha ntashindwa kukuelewa. IBRAHIM Alikuwa kabila gani? Kaanani ni nchi gani?mussa ni kabila gani? na aliwatoa waisrael misri akawapeleka wapi? mi nimetumia vitabu kadhaa kikiwepo Biblia mabacho nadhani ukilinganisha na kuran Biblia ni ya zamani zaidi. na Muhamadi mwenyewe alisema pia wafuasi wake wapate elimu kwa Wayahudi so sijajua kwa nini ndugu yangu umekuja na hasira hivi.
 
Pia mimi rangi hainipi shida sana. huwa sioni sababu ya kugombea rangi ya Yesu,rangi ya Wayahudi au akina nani ni nini...huwa hainipi shida kabisa. Ukiona mtu analazimisha rangi flan iwe watu flan maarufu au wenye nguvu flan ujue ni kwa sababu tu anajisikia inferior. mi hata ukinambia Yesu alikuwa wa Blue haina shida.
 
Mgogoro wa Israel na Wapalestina Chimbuko na Ukweli wake.

Je Wayahudi wana haki ya kuishi eneo la Mashariki ya Kati? Je hakukuwepo Kundi la wenyeji waliofahamika kwa jina la Wapalestina toka mwanzo? Je Wayahudi si kwamba walifika mara baada ya Vita ya Pili ya Dunia na kuchukua Ardhi hiyo toka mikononi mwa Wapalestina?

Haya ni maswali mengi ambayo watu wamekuwa wakiuliza nap engine kuamini mambo flan kuhusiana na maswali haya. WAYAHUDI waliishi nchi ile toka siku za Musa na ndio inayofahamika kama nchi ya ahadi pale Musa alipowatoa Waisraeli/Wayahudi toka Utumwani Huko Misri.Pamoja na kuwa walipata wakati mgumu wakati mwingine kupigana na Wasiria na Wababiloni ila kwa miaka yote hiyo ilibaki kuwa ni nchi ya Wayahudi mpaka walipokuja Warumi na kuwasambalatisha. Tito mtoto wa Mfalme aliliharibu Hekalu mwaka 70 Baada Ya Kristo na baadaye karne ya Pili Mtawala Hadrian alizima Uasi wa Wayahudi. Kipindi hiki Wayahudi wengi sana walifukuzwa na wengine wakachukuliwa Utumwani na Warumi.

Idadi ndogo ya Wayahudi walibaki katika ardhi hiyo mpaka ilipofika karne ya 20. Hata hivyo Jina la nchi hii lilibadilishwa kwa kuwa Hadrian alidhamilia kufuta kabisa uwepo au utambulisho wa Wayahudi. Na Hivyo akaiita hii nchi kuwa ni Syria-Palestinia” Palestinian i neno la Kilatini likimaanisha Philistine au kwa jina Maarufu Wafilisti hawa ambao tunakumbuka mara nyingi walipigana sana na Waisrael na kama umewahi kusikia kisa cha Daudi na Goliathi ambaye alikuwa ni Mfilisti au Samsoni na Delila. Hawa walikuwa ni maadui wakubwa wa Waisrael. Ukitaka zaidi vifungu vipo kwenye Biblia.leo nimeleta habari hizi Kihistoria si Kiimani au kufuata Biblia. Kwa hiyo Hadrian kwa makusudi kabisa aliamua kuwaudhi na kuwatukana Wayahudi.

Hivyo hakukuwa na nchi iliyokuwa ikiitwa Palestina. Hili lilikuwa jina la Utani kwa nchi Takatifu lililotolewa na Warumi. Watu wanaojiita leo hii kuwa ni Wapalestina ni Waarabu na siku zote walikuwa wakijitambulisha kuwa wao ni Waarabu mpaka Walipokuja kuitwa kuwa wao ni Wapalestina na Mwanzilishi wa PLO Yassir Arafat (Mungu aiweke roho yake panapostahili amen) Mwaka 1964.

Hata tungesema ni Kweli kuwa Waarab walishi Katika ardhi ile kwa Karne nyingi

Kwa miaka mingi waarabu wamekuwa wakipatikana sehemu nyingi nyinginezo lakini hawakuwah kuwa katika ardhi takatifu kwa kiasi kinachoeleweka Mpaka wakati Muhamad alipokuja kueneza Uislamu. Na waislamu walifanikiwa kuiteka ardhi yaw a bizantina ambao walikuwa ni Kanisa la mabaki ya Himaya ya Kirumi.

Kwa miaka mingi wakipigana vita vya kidini na vita mbalimbali nchi ikawa inakua chini ya tawala tofaut tofaut chini ya Kanisa la Katoliki na Waislamu. Yaani wakibadilishana kutegemeana na matokeo ya vita hivyo. Mwishowe iliangukia chini ya Himaya nyingine y kiislamu iliyokuwa ikifahamika kama Himaya ya Ottoman au (Ottoman Empire) Baada ya Himaya ya Ottoman kushindwa katika vita ya Kwanza ya Dunia Mashariki ya Kati iliangukia chini ya Utawala wa Uingereza Kuu( Great Britain). Hata hivyo Mashariki ya kati ikawa ni kama Zawadi ya Himaya ya Uingereza. Uingereza haikuwa na Nia wala uwezo wa kulishikiria eneo hilo milele.

Kwa sababu hiyo walianza kuunda states mbalimbali ambazo walishirikisha Waarabu waliowasaidia katika vile vita(kulikuwa na waaarabu ambao waliunga mkono upande wa Uingereza katika vile vita) walipewa states hizi waendeshe mambo yao wenyewe.. neno Arabia lilikuwa tayari limekuwa likitumika kuelezea sehemu kubwa ya eneo hili. Mashariki ya kati hii tunayoifahamu leo haikuwa huru mpaka Uingereza ilipojiondoa katika mambo ya kiutawala ya eneo hili.

Wakati waingereza wakiunda state mbalimbali. Kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa enzi hizo (League of Nations) wakatoa tamko kuwa watatoa nafasi kwa Wayahudi walio sehemu mbalimbali Duniani kurudi katika nchi yao. Na mwaliko au nafasi hii iliitwa Tamko la Balfour. Hivyo Wayahudi wengi waliamua kurudi toka huko walipokuwepo nchini mwao ambako walifukuzwa miaka mingi sana na Utawala wa Kirumi. Hivyo wana hawa wa Ibrahimu wakajikusanya toka Urusi,Ulaya Magharibi na maeneo mbalimbali kurudi nchini kwao kujumuika na wenzao Wakristo na Waislamu waliokuwa katika nchi hiyo ambayo nao waliiona kuwa ni nchi Takatifu.

Wayahudi wengi walipofika walinunua Ardhi kutoka kwa wamiliki Wakiarabu waliokuwepo wakati huo ambayo haikuwa nzuri,ilikuwa ni yenye madimbwi na taratibu wakaanza kuigeuza kuwa ni ardhi nzuri kwa kilimo na kupanda miti kila sehemu. Uchumi ukakua na wakaligeuza eneo hili kuwa zuri hata maeneo yaliyokuwa makame au majangwa.Wakageuza eneo hili kuwa la kuchumi na kazi zikawa zinapatikana kwa wingi Waaabu wengi wakaja wakiona kama ni sehemu yenye fursa. Wakulima na Wafanyabiashara wa Kiyahudi ndio walioweza kugeuza eneno hili kuwa lenye manufaa.

1. SWALI MUHIMU “ NI NANI MWENYE HAKI NA ARDHI/NCHI HII”
Naomba sasa niwaletee chimbuko la ugomvi huu kuanzia miaka ya nyuma kabisa kabla ya Uislamu na ukristo.
Naomba sasa niwaletee chimbuko la ugomvi huu kuanzia miaka ya nyuma kabisa kabla ya Uislamu na ukristo.

MADAI YA HUU MGOGORO
Israel ambayo ina wananchi wa kutoa jamii na makundi mbalimbali ya dini kwa kikubwa ni nchi ambayo inatawaliwa Wayahudi. Ina wakazi wapatao Mil 6.5 na zaidi ya Mil 5.ni wenye asili ya Kiyahudi. Wayahudi duniani kote hudai wao ndiyo wakazi halisi wa eneo hili. Na wao histori yao inarudi nyuma miaka 4000 kipindi cha Ibrahim, Isaka na Yakobo ambao ni wazazi wa Kwanza kabisa kuanza kuishi Nchini hapo. Na hapa tunaona au tunapata Kumbukumbu zao kwnye Kitabu kiitwacho Biblia.

Wapalestina pia wao wanadai kuwa wana uhusiano mkubwa na eneo hilo. Wanasema kuwa waarabu pia walitokana na Uzao wa Ibrahim ambaye alimzaa Ishmael, Esau na wengineo. Wao kiasili ni Wapwa wa Wayahudi. Na hawa wengi wao wanaishi maeneo ya Ukanda wa Magharibi na pia Gaza wakisema wana haki sawa na wayahudi kwa sababu ya uzao huo.

Uwepo wa Wayahudi na Waarabu.
Hebu tuangalie kwa kifupi matukio yaliyopelekea hali iliyopo . inabidi kurudi nyuma mbali zaidi ya mwaka 1948 au 1967. Na hivyo kurudi miaka mingi zaidi kipindi cha waanzilishi wa Makabila haya ya Kiyahudi na Kiarabu. Hebu kwa sasa tuangalie miaka 2000 iliyopita.

Haina ubishi kuhusiana na ukweli kuwa mwanzoni mwa karne ya kwanza 1st C. AD. Kipindi cha Yesu Kristo eneo la Palestina lilianza kukaliwa na Wayahudi. Eneo Kipindi hiki lilikuwa chini ya Utawala wa Kirumi. Hata hivyo Wayahudi waliasi kiasi kwamba Warumi waliuzingira mji wa Yerusalem . mwaka 70 B.K (70AD.) Yaani BAADA ya Kristo. hekali lilibomolewa

Wayahudi wengi waliangamizwa na wengine walifukuzwa katika Huo Mji wa Yerusalem. Na wengi walitawanyika sehemu mbalimbali duniani wakikimbia utawala wa Kirumi uliokuwa katili sana.

Hata hivyo kuna Wayahudi ambao walibaki katika ardhi hiyo hasa hasa sehemu za Galileya na kuendelea na maisha yao ya Kiyahudi.Karne nyingi zikapita weng zaidi wakawa wanarudi kwenye Miji Mikuu ya Uyuda ambayo ni Yerusalem, Hebrofeni,Tiberia na Safed. Huko kulikuwa na makazi ya Kiyahudi toka enzi za Kibiblia. Na kule mwanzo nlisema toka Karne 1 hadi ya 19 hakukuwa na Taifa lililoitwa Palestina. Waarabu na Wayahudi waliishi pamoja kwa amani kabisa.

Kwa mtizamo wa mgogoro ulipo kwa sasa ulichocehwa sana na Imani ya Uislam na Uyahudi. Na hapa tunajiuliza nini athari za kuibuka kwa |Dini ya Kiislamu? Mpaka Karne ya 7 B.K Wayahudi walikuwa wakiishi vizuri pasipo Ugomvi na Waarabu. Na Wayahudi wengi waliishi sehemu mbalimbali za Kiarabu ikiwepo Arabia. Na baadaye akaja Muhamad akasema kuwa haiwezekani kwa DINI MBILI KUKAA SEHEM MOJA katika peninsula ya Waarab. Na kuna sehemu katika quran inayowataka Waislamu kuwachukia au kuwapinga Wayahudi(sitoiweka hapa si lengo langu kuzungumzia dini,ila mtu akitaka naweza weka. Naepuka kuingiza UDINI katika historia) hata hivyo kwa zaidi ya miaka 1300 Wayahudi na Waarabu waliishi kwa kuvumiliana huko Mashariki ya kati.na Hapa lazima pia mjue baadaye Wayahudi pia walikuja Kupata shida sana na kuteswa na Wakristo wakati wa Vita Takatifu.

UZAYUNI NA KURUDI KWA WAYAHUDI.
Karne ya 19 Wayahudi walianza kurudi Nchi Takatifu.na mwisho wa Karne hiyo tuliona mwanzo wa kuanza Uzayuni mapak mwanzo mwa karne ya 20 Waingereza walipoamua kushikiria na kusimamia suala la Wayahudi kurudi Israel kupitia Azimio la Balfrour. Tuliona kule mwanzo kuwa baada ya vita ya kwanza ya Dunia Umoja wa Mataifa uliikabidhi Uingereza kuisimamia Palestina kwa kwa neno Palestina hapa hatumaanishi Jordan peke yake ila mpaka Bahari ya Mediteraniani,Arabia mpaka kwenye eneo la Iraq ya leo. Na pia kuanzia Misri,Lebanoni na Syria. Hata hivyo Mwaka 1921 katika hali ya kujenga imani kwa Waarab wakatoa sehemu ya Jordan Mashariki(Trasnjordan) kwa Sheikh Abdulllah. Na Hii ikawa Ufalme wa Jordan na wakapata mpaka Ukanda wa Magharib eneo ambalo mwaka 1948 likawa Jimbo la Israel. Na mpaka Waingereza wanaondoka mwaka 1948 kulikuwa kumeshaibuka Vita kati ya Wayahudi na Waarabu na Nusu Karne iliyofuatia tumejionea wenyewe.

HISTORIA YA MGOGORO HUU KIBIBLIA.
Ukiona kuwa Biblia si imani yako soma Biblia kama Kitabu cha Historia pia itakusadia kuelewa asili ya Wayahudi na Waarabu.

Ibrahimi ametajwa sana kuhusiana na uhusiano wa Mataifa yote Mawili yaani Waisrael na Wapalestina. Wayahudi na Waarabu wanamchukulia Ibrahim kuwa ni mwanzilishi wa Mataifa yao.Mataifa mengine au asili za watu wengine inasemekana ni Uzao wa Shemu motto mkubwa wa Nuhu. Baada ya Mafuriko Makuu vizazi vya Nuhu vilisambaa Dunia yote.
Ilikuwa ni kutokea kwa Ile Jamii iliyokuwa Ikiabudu Mwezi Kaldea ambako Bwana Mungu alimuita Ibrahim na Mkewe Sara na mpwa wake Lutu kuishi Kaanani. Hili ni eneo Kusini mwa Mto Yufrate kuelekea chini Misri.Hili eneo walikuwa wakiishi Wakaanani, Wafilistini na Makabila mengine ambayo hayakuwa yakimwabudu Mungu. Kwa Imani Ibrahimu aliambiwa kuwa ile laana ya Babiloni siku moja itaondolewa na atafanywa kuwa Taifa Kubwa na ardhi/nchi itabarikiwa. Mwanzo (12:2-3)

Ilikuwa ahadi nzuri kweli kweli. Lakini Ibrahim alipofika Shekem(kwa sasa inaitwa Nablusi huko ukanda wa Magharibi) kwa mara ya kwanza alipokanyaga Kaanani Mungu akamwambia kuwa kwa uzao wake atampatia hiyo Nchi( Mwanzo 12:7) na baadaye Mungu akamwambia nitakupa nchi hii milele (Mwanzo 13:14-15) kuanzia mto wa Misri kusini mpaka kwenye Mto Yufrate Kaskazini Mashariki)......

TUTAENDELEA.....
ASILI YA WAARABU NA URITHI WA NCHI YAO.



mkuu mbona huendelei?tunafuatilia
 
mbona unamtukana mwenzio bila sababu za msingi?????????? tuishi kwa upendo ndugu yangu.


Jionee huruma wewe mwenyewe usie jijua wala kujitambua upo upo tu duniani hujui Mchana wala usiku. Nyumbu
 
mbona unamtukana mwenzio bila sababu za msingi?????????? tuishi kwa upendo ndugu yangu.
Hakuna tusi hapo. Aliekosa upendo ni nani kati yetu? Ikiwa mada iliyoletwa inafikia mtu kudai hana huruma kwa binadamu mwenzake pana upendo hapo?
 
Mgogoro wa Israel na Wapalestina Chimbuko na Ukweli wake.

Je Wayahudi wana haki ya kuishi eneo la Mashariki ya Kati? Je hakukuwepo Kundi la wenyeji waliofahamika kwa jina la Wapalestina toka mwanzo? Je Wayahudi si kwamba walifika mara baada ya Vita ya Pili ya Dunia na kuchukua Ardhi hiyo toka mikononi mwa Wapalestina?

Haya ni maswali mengi ambayo watu wamekuwa wakiuliza nap engine kuamini mambo flan kuhusiana na maswali haya. WAYAHUDI waliishi nchi ile toka siku za Musa na ndio inayofahamika kama nchi ya ahadi pale Musa alipowatoa Waisraeli/Wayahudi toka Utumwani Huko Misri.Pamoja na kuwa walipata wakati mgumu wakati mwingine kupigana na Wasiria na Wababiloni ila kwa miaka yote hiyo ilibaki kuwa ni nchi ya Wayahudi mpaka walipokuja Warumi na kuwasambalatisha. Tito mtoto wa Mfalme aliliharibu Hekalu mwaka 70 Baada Ya Kristo na baadaye karne ya Pili Mtawala Hadrian alizima Uasi wa Wayahudi. Kipindi hiki Wayahudi wengi sana walifukuzwa na wengine wakachukuliwa Utumwani na Warumi.

Idadi ndogo ya Wayahudi walibaki katika ardhi hiyo mpaka ilipofika karne ya 20. Hata hivyo Jina la nchi hii lilibadilishwa kwa kuwa Hadrian alidhamilia kufuta kabisa uwepo au utambulisho wa Wayahudi. Na Hivyo akaiita hii nchi kuwa ni Syria-Palestinia” Palestinian i neno la Kilatini likimaanisha Philistine au kwa jina Maarufu Wafilisti hawa ambao tunakumbuka mara nyingi walipigana sana na Waisrael na kama umewahi kusikia kisa cha Daudi na Goliathi ambaye alikuwa ni Mfilisti au Samsoni na Delila. Hawa walikuwa ni maadui wakubwa wa Waisrael. Ukitaka zaidi vifungu vipo kwenye Biblia.leo nimeleta habari hizi Kihistoria si Kiimani au kufuata Biblia. Kwa hiyo Hadrian kwa makusudi kabisa aliamua kuwaudhi na kuwatukana Wayahudi.

Hivyo hakukuwa na nchi iliyokuwa ikiitwa Palestina. Hili lilikuwa jina la Utani kwa nchi Takatifu lililotolewa na Warumi. Watu wanaojiita leo hii kuwa ni Wapalestina ni Waarabu na siku zote walikuwa wakijitambulisha kuwa wao ni Waarabu mpaka Walipokuja kuitwa kuwa wao ni Wapalestina na Mwanzilishi wa PLO Yassir Arafat (Mungu aiweke roho yake panapostahili amen) Mwaka 1964.

Hata tungesema ni Kweli kuwa Waarab walishi Katika ardhi ile kwa Karne nyingi

Kwa miaka mingi waarabu wamekuwa wakipatikana sehemu nyingi nyinginezo lakini hawakuwah kuwa katika ardhi takatifu kwa kiasi kinachoeleweka Mpaka wakati Muhamad alipokuja kueneza Uislamu. Na waislamu walifanikiwa kuiteka ardhi yaw a bizantina ambao walikuwa ni Kanisa la mabaki ya Himaya ya Kirumi.

Kwa miaka mingi wakipigana vita vya kidini na vita mbalimbali nchi ikawa inakua chini ya tawala tofaut tofaut chini ya Kanisa la Katoliki na Waislamu. Yaani wakibadilishana kutegemeana na matokeo ya vita hivyo. Mwishowe iliangukia chini ya Himaya nyingine y kiislamu iliyokuwa ikifahamika kama Himaya ya Ottoman au (Ottoman Empire) Baada ya Himaya ya Ottoman kushindwa katika vita ya Kwanza ya Dunia Mashariki ya Kati iliangukia chini ya Utawala wa Uingereza Kuu( Great Britain). Hata hivyo Mashariki ya kati ikawa ni kama Zawadi ya Himaya ya Uingereza. Uingereza haikuwa na Nia wala uwezo wa kulishikiria eneo hilo milele.

Kwa sababu hiyo walianza kuunda states mbalimbali ambazo walishirikisha Waarabu waliowasaidia katika vile vita(kulikuwa na waaarabu ambao waliunga mkono upande wa Uingereza katika vile vita) walipewa states hizi waendeshe mambo yao wenyewe.. neno Arabia lilikuwa tayari limekuwa likitumika kuelezea sehemu kubwa ya eneo hili. Mashariki ya kati hii tunayoifahamu leo haikuwa huru mpaka Uingereza ilipojiondoa katika mambo ya kiutawala ya eneo hili.

Wakati waingereza wakiunda state mbalimbali. Kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa enzi hizo (League of Nations) wakatoa tamko kuwa watatoa nafasi kwa Wayahudi walio sehemu mbalimbali Duniani kurudi katika nchi yao. Na mwaliko au nafasi hii iliitwa Tamko la Balfour. Hivyo Wayahudi wengi waliamua kurudi toka huko walipokuwepo nchini mwao ambako walifukuzwa miaka mingi sana na Utawala wa Kirumi. Hivyo wana hawa wa Ibrahimu wakajikusanya toka Urusi,Ulaya Magharibi na maeneo mbalimbali kurudi nchini kwao kujumuika na wenzao Wakristo na Waislamu waliokuwa katika nchi hiyo ambayo nao waliiona kuwa ni nchi Takatifu.

Wayahudi wengi walipofika walinunua Ardhi kutoka kwa wamiliki Wakiarabu waliokuwepo wakati huo ambayo haikuwa nzuri,ilikuwa ni yenye madimbwi na taratibu wakaanza kuigeuza kuwa ni ardhi nzuri kwa kilimo na kupanda miti kila sehemu. Uchumi ukakua na wakaligeuza eneo hili kuwa zuri hata maeneo yaliyokuwa makame au majangwa.Wakageuza eneo hili kuwa la kuchumi na kazi zikawa zinapatikana kwa wingi Waaabu wengi wakaja wakiona kama ni sehemu yenye fursa. Wakulima na Wafanyabiashara wa Kiyahudi ndio walioweza kugeuza eneno hili kuwa lenye manufaa.

1. SWALI MUHIMU “ NI NANI MWENYE HAKI NA ARDHI/NCHI HII”
Naomba sasa niwaletee chimbuko la ugomvi huu kuanzia miaka ya nyuma kabisa kabla ya Uislamu na ukristo.
Naomba sasa niwaletee chimbuko la ugomvi huu kuanzia miaka ya nyuma kabisa kabla ya Uislamu na ukristo.

MADAI YA HUU MGOGORO
Israel ambayo ina wananchi wa kutoa jamii na makundi mbalimbali ya dini kwa kikubwa ni nchi ambayo inatawaliwa Wayahudi. Ina wakazi wapatao Mil 6.5 na zaidi ya Mil 5.ni wenye asili ya Kiyahudi. Wayahudi duniani kote hudai wao ndiyo wakazi halisi wa eneo hili. Na wao histori yao inarudi nyuma miaka 4000 kipindi cha Ibrahim, Isaka na Yakobo ambao ni wazazi wa Kwanza kabisa kuanza kuishi Nchini hapo. Na hapa tunaona au tunapata Kumbukumbu zao kwnye Kitabu kiitwacho Biblia.

Wapalestina pia wao wanadai kuwa wana uhusiano mkubwa na eneo hilo. Wanasema kuwa waarabu pia walitokana na Uzao wa Ibrahim ambaye alimzaa Ishmael, Esau na wengineo. Wao kiasili ni Wapwa wa Wayahudi. Na hawa wengi wao wanaishi maeneo ya Ukanda wa Magharibi na pia Gaza wakisema wana haki sawa na wayahudi kwa sababu ya uzao huo.

Uwepo wa Wayahudi na Waarabu.
Hebu tuangalie kwa kifupi matukio yaliyopelekea hali iliyopo . inabidi kurudi nyuma mbali zaidi ya mwaka 1948 au 1967. Na hivyo kurudi miaka mingi zaidi kipindi cha waanzilishi wa Makabila haya ya Kiyahudi na Kiarabu. Hebu kwa sasa tuangalie miaka 2000 iliyopita.

Haina ubishi kuhusiana na ukweli kuwa mwanzoni mwa karne ya kwanza 1st C. AD. Kipindi cha Yesu Kristo eneo la Palestina lilianza kukaliwa na Wayahudi. Eneo Kipindi hiki lilikuwa chini ya Utawala wa Kirumi. Hata hivyo Wayahudi waliasi kiasi kwamba Warumi waliuzingira mji wa Yerusalem . mwaka 70 B.K (70AD.) Yaani BAADA ya Kristo. hekali lilibomolewa

Wayahudi wengi waliangamizwa na wengine walifukuzwa katika Huo Mji wa Yerusalem. Na wengi walitawanyika sehemu mbalimbali duniani wakikimbia utawala wa Kirumi uliokuwa katili sana.

Hata hivyo kuna Wayahudi ambao walibaki katika ardhi hiyo hasa hasa sehemu za Galileya na kuendelea na maisha yao ya Kiyahudi.Karne nyingi zikapita weng zaidi wakawa wanarudi kwenye Miji Mikuu ya Uyuda ambayo ni Yerusalem, Hebrofeni,Tiberia na Safed. Huko kulikuwa na makazi ya Kiyahudi toka enzi za Kibiblia. Na kule mwanzo nlisema toka Karne 1 hadi ya 19 hakukuwa na Taifa lililoitwa Palestina. Waarabu na Wayahudi waliishi pamoja kwa amani kabisa.

Kwa mtizamo wa mgogoro ulipo kwa sasa ulichocehwa sana na Imani ya Uislam na Uyahudi. Na hapa tunajiuliza nini athari za kuibuka kwa |Dini ya Kiislamu? Mpaka Karne ya 7 B.K Wayahudi walikuwa wakiishi vizuri pasipo Ugomvi na Waarabu. Na Wayahudi wengi waliishi sehemu mbalimbali za Kiarabu ikiwepo Arabia. Na baadaye akaja Muhamad akasema kuwa haiwezekani kwa DINI MBILI KUKAA SEHEM MOJA katika peninsula ya Waarab. Na kuna sehemu katika quran inayowataka Waislamu kuwachukia au kuwapinga Wayahudi(sitoiweka hapa si lengo langu kuzungumzia dini,ila mtu akitaka naweza weka. Naepuka kuingiza UDINI katika historia) hata hivyo kwa zaidi ya miaka 1300 Wayahudi na Waarabu waliishi kwa kuvumiliana huko Mashariki ya kati.na Hapa lazima pia mjue baadaye Wayahudi pia walikuja Kupata shida sana na kuteswa na Wakristo wakati wa Vita Takatifu.

UZAYUNI NA KURUDI KWA WAYAHUDI.
Karne ya 19 Wayahudi walianza kurudi Nchi Takatifu.na mwisho wa Karne hiyo tuliona mwanzo wa kuanza Uzayuni mapak mwanzo mwa karne ya 20 Waingereza walipoamua kushikiria na kusimamia suala la Wayahudi kurudi Israel kupitia Azimio la Balfrour. Tuliona kule mwanzo kuwa baada ya vita ya kwanza ya Dunia Umoja wa Mataifa uliikabidhi Uingereza kuisimamia Palestina kwa kwa neno Palestina hapa hatumaanishi Jordan peke yake ila mpaka Bahari ya Mediteraniani,Arabia mpaka kwenye eneo la Iraq ya leo. Na pia kuanzia Misri,Lebanoni na Syria. Hata hivyo Mwaka 1921 katika hali ya kujenga imani kwa Waarab wakatoa sehemu ya Jordan Mashariki(Trasnjordan) kwa Sheikh Abdulllah. Na Hii ikawa Ufalme wa Jordan na wakapata mpaka Ukanda wa Magharib eneo ambalo mwaka 1948 likawa Jimbo la Israel. Na mpaka Waingereza wanaondoka mwaka 1948 kulikuwa kumeshaibuka Vita kati ya Wayahudi na Waarabu na Nusu Karne iliyofuatia tumejionea wenyewe.

HISTORIA YA MGOGORO HUU KIBIBLIA.
Ukiona kuwa Biblia si imani yako soma Biblia kama Kitabu cha Historia pia itakusadia kuelewa asili ya Wayahudi na Waarabu.

Ibrahimi ametajwa sana kuhusiana na uhusiano wa Mataifa yote Mawili yaani Waisrael na Wapalestina. Wayahudi na Waarabu wanamchukulia Ibrahim kuwa ni mwanzilishi wa Mataifa yao.Mataifa mengine au asili za watu wengine inasemekana ni Uzao wa Shemu motto mkubwa wa Nuhu. Baada ya Mafuriko Makuu vizazi vya Nuhu vilisambaa Dunia yote.
Ilikuwa ni kutokea kwa Ile Jamii iliyokuwa Ikiabudu Mwezi Kaldea ambako Bwana Mungu alimuita Ibrahim na Mkewe Sara na mpwa wake Lutu kuishi Kaanani. Hili ni eneo Kusini mwa Mto Yufrate kuelekea chini Misri.Hili eneo walikuwa wakiishi Wakaanani, Wafilistini na Makabila mengine ambayo hayakuwa yakimwabudu Mungu. Kwa Imani Ibrahimu aliambiwa kuwa ile laana ya Babiloni siku moja itaondolewa na atafanywa kuwa Taifa Kubwa na ardhi/nchi itabarikiwa. Mwanzo (12:2-3)

Ilikuwa ahadi nzuri kweli kweli. Lakini Ibrahim alipofika Shekem(kwa sasa inaitwa Nablusi huko ukanda wa Magharibi) kwa mara ya kwanza alipokanyaga Kaanani Mungu akamwambia kuwa kwa uzao wake atampatia hiyo Nchi( Mwanzo 12:7) na baadaye Mungu akamwambia nitakupa nchi hii milele (Mwanzo 13:14-15) kuanzia mto wa Misri kusini mpaka kwenye Mto Yufrate Kaskazini Mashariki)......

TUTAENDELEA.....
ASILI YA WAARABU NA URITHI WA NCHI YAO.



Aisee ungeweka na namba yako ya simu tuwe tunakutwangia kukumbusha uendelee,upo kimya sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom