Ukweli ndio mapenzi ya kweli?

Ni vizuri kutokuwa na mawazo machafu kwa mkeo/mmeo (hata kama atafanya uchafu). Hii ndo maana ya ndoa. Ila sentensi yako Mama kaoge kwanza maana jasho limekupiga sana" inaleta tafsiri nyingi mno, zilizo sahihi na zisizo. Uvumilivu unatakiwa.

Mkuu kweli sijawahi kumwambia kitu kama hicho ila kila siku mie nikirudi huwa nasema natoa ng'e eeehhh ngoja nikaoge nzi wasije nizingira...anachekaga sana lkn jana kumwambia yeye...kumbe mkuki kwa nguruwe bwana.....sasa kama ningemwambia mama unatoa ng'e si ndoa ingekufa kabisa?
 
Jamani wana MMU hapa mwenzenu yamenikuta kujifanya mkweli kwa kila jambo....Jana jioni mama karudi toka kwenye mihangaiko yake, kama kawa nikamhug kimahaba, tukakissiana kama, tukavutana kuelekea MANSION kwetu, sasa hapo kiama kikaja baada ya kumwambia..."Mama kaoge kwanza maana jasho limekupiga sana", mwenzenu kusema tu hivyo mama kaja juu, mie nanuka au sio? nenda katafute wasionuka na maneno kibao tu...Nikajiuliza, mbona nikimwambia leo nimepata hiki hufurahia, nikimwambia jana fulani kanitextia ujumbe huu usome anafurahi....Je, ni vitu gani tuambiane ukweli na vipi tusiambiane? niko Dilema jamani....

Kauli yako ilistahili kuwa mpenzi twende tukaoge naona jua leo limenipiga sana, hapo ingekuwa poa kabisa wala mama asingekujia juu.
 
mkuu usiombe yakukute hayo...niligugumia na kuachwa na ukwasu wangu siku nzima....

Kabla ya kutoa kauli inabidi ufikirie mara mbili mbili kabla hujaitoa ili kuepusha shari. Kuna kesi nyingine kama ya kwako mother house aliishia kulalamika hivyo hivyo kwamba siku hizi mie nanuka kawatafute wasionuka :) Hakikisha kauli kama hizo zimekaa kimapenzi mapenzi la sivyo inabidi ujiandae kwa varangati na si ajabu jiko kununa :) hapo inabidi uanze kazi ya kubembeleza na kuomba samahani kama milioni hivi :) ndipo usamehewe
 
Hahahaha lohhhh

Magu bana pole sana..
Ulichomwambia ni sawa..
Ila njia au njinsi ulivyomwambia dahhh
Uliharibu...

Ungeremba kidogo, weka maneno mawili
Matatu matamu..au vipi..

Aksante AD ......kweli kabisa au naye angepropose mchezo uanzie bafuni wakiwa wanaoga. au nawe Magu ni 'mwoga' wa kuoga eh?

Ila haiwezekani bana wanawake wengi huwa tuko sensitive sana unapofika wakati huo ...haiwezekani ye atoke juani moja kwa moja 'jukwaani'
 
Ukweli utumike pale ambapo utajenga mahusiano mazuri kati ya wanandoa lakini kama unaamini ukweli huo utavuruga mahusiano yenu basi uwongo utumike mahali pa ukweli ili kujenga badala ya kubomoa.
 
Aksante AD ......kweli kabisa au naye angepropose mchezo uanzie bafuni wakiwa wanaoga. au nawe Magu ni 'mwoga' wa kuoga eh?

Ila haiwezekani bana wanawake wengi huwa tuko sensitive sana unapofika wakati huo ...haiwezekani ye atoke juani moja kwa moja 'jukwaani'

MwanajamiiOne pole nimepewa mimi asante waitoa wewe? Mbona unaninyanyapaa lakini? haikuwa jukwaani bwana....nilimpokea kwa yale mambo yetu yale...makisikisi, mahug hug na maneno matamu huku mishumaa inside the MANSION ikitoa ule mwanga hafifu ready to see only those thangs, na mziki wetu maridhawa taratiibu...mambo yale ya LIZZY jikoni yakisubiri kuliwa, ma wine mezani ya kumwaga we acha tu......ukwasu pia ukigusa mapigo ya moyo utadhani ndo our first date......Mie napenda kuoga ka bata.....
 
Kabla ya kutoa kauli inabidi ufikirie mara mbili mbili kabla hujaitoa ili kuepusha shari. Kuna kesi nyingine kama ya kwako mother house aliishia kulalamika hivyo hivyo kwamba siku hizi mie nanuka kawatafute wasionuka :) Hakikisha kauli kama hizo zimekaa kimapenzi mapenzi la sivyo inabidi ujiandae kwa varangati na si ajabu jiko kununa :) hapo inabidi uanze kazi ya kubembeleza na kuomba samahani kama milioni hivi :) ndipo usamehewe

mkuu inabidi nianze upya mipango ya jana maana si utani lazima ukwasu wa jana uhamie leo....
 
Ukweli utumike pale ambapo utajenga mahusiano mazuri kati ya wanandoa lakini kama unaamini ukweli huo utavuruga mahusiano yenu basi uwongo utumike mahali pa ukweli ili kujenga badala ya kubomoa.

namhala imekamatwa kunako....noma lkn poa tu nitafanya remix..
 
MwanajamiiOne pole nimepewa mimi asante waitoa wewe? Mbona unaninyanyapaa lakini? haikuwa jukwaani bwana....nilimpokea kwa yale mambo yetu yale...makisikisi, mahug hug na maneno matamu huku mishumaa inside the MANSION ikitoa ule mwanga hafifu ready to see only those thangs, na mziki wetu maridhawa taratiibu...mambo yale ya LIZZY jikoni yakisubiri kuliwa, ma wine mezani ya kumwaga we acha tu......ukwasu pia ukigusa mapigo ya moyo utadhani ndo our first date......Mie napenda kuoga ka bata.....

Ah hapana mpendwa sikuitika pole yako jamani, nilimshukuru AD kwa kumaliza nlotaka kusema LOL. Oh masikini haya pole ila basi kwenye hayo maandalizi ungekumbuka kuweka na section ya "Kuoga pamoja".
 
labda hakua tayari kuupokea kwa wakati huo.but ukweli unahitajika kwa watu mlio kwenye ukweli kama wewe
 
Ah hapana mpendwa sikuitika pole yako jamani, nilimshukuru AD kwa kumaliza nlotaka kusema LOL. Oh masikini haya pole ila basi kwenye hayo maandalizi ungekumbuka kuweka na section ya "Kuoga pamoja".

haina noma nitafanya remix soon ngoja mida yake ya kurudi ifike...ujue nimemwandikia ubeti mmoja wa shairi enzi zetu tunatongozana kanijibu with :) sijui vina maana gani au ndo nimeharibu kabisa?
 
Aksante AD ......kweli kabisa au naye angepropose mchezo uanzie bafuni wakiwa wanaoga. au nawe Magu ni 'mwoga' wa kuoga eh?

Ila haiwezekani bana wanawake wengi huwa tuko sensitive sana unapofika wakati huo ...haiwezekani ye atoke juani moja kwa moja 'jukwaani'


MJ1 hujambo mami??

yaani hapo kwenye red ndio futa kazi ..
Magu chukua hiyo penseli juu ya meza
na hiyo bahasha ya bili ya umeme andika
hiyo kitu MJ1 aliyo kwambia ..
sante dear
 
Ah hapana mpendwa sikuitika pole yako jamani, nilimshukuru AD kwa kumaliza nlotaka kusema LOL. Oh masikini haya pole ila basi kwenye hayo maandalizi ungekumbuka kuweka na section ya "Kuoga pamoja".

hahahaah loohh
Maguu umeona aee hilo neno la "PAMOJA"
lilivyo muhimu ... Hope umeandika na hii :)
 
haina noma nitafanya remix soon ngoja mida yake ya kurudi ifike...ujue nimemwandikia ubeti mmoja wa shairi enzi zetu tunatongozana kanijibu with :) sijui vina maana gani au ndo nimeharibu kabisa?

Kukujibu tu ni dalili njema!! Chombeza na kajiutani kidogo (Hata ka chumbani mwe) Mtayarishe tangu mapema bana ajue kuwa ana'overtime' inamsubiri. Kila la kheri Bro.
 
MJ1 hujambo mami??

yaani hapo kwenye red ndio futa kazi ..
Magu chukua hiyo penseli juu ya meza
na hiyo bahasha ya bili ya umeme andika
hiyo kitu MJ1 aliyo kwambia ..
sante dear

Aksante AD, mzima kabisa dada yangu mkoloni kidooooogo ameniachia jana na leo!
 
Kwanza AD ujue hapo namwambia hivyo tayari jikoni yale mambo ya LIZZY yalikuwa tayari...niliremba utadhani ndo siku ya kwanza tunakutana...Hapo AD najua kusema mpaka yeye ananambiaga najua kusema...UKWELI UMENIPONZA au?


Nadhani saa nyingine tunaongea sana
mpaka ile point na ule utamu unaondoka..

muhumu kusema machache yenye maana....
kuliko kujaza chungu na mabovu...

Binafsi nakuamini sana Maguu ikija kwenye maneno matamu
maana nakumbuka mashairi yako ....ila leo umeniangusha kwa kweli
hahahahahah lol
 
Hahahahaahah acha uchimvi we mwali lol
Nasubiria malaika kama Magulumangu atokee ndotoni mwe!! Outing muhimu mydia akili itafubaa

hahahahahah lohhh
...
Maguu mpaka apate hayo maneno mmmhh
Usijali lakini atajitokeza tu ..... piga moyo konde dear ....
Haya ungenialika tungefanya ( girls/women night out hahaha )
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom