Ukweli kuhusu uwepo wa vampire

Ukweli kuhusu uwepo wa vampire

Story za vampires ni za kitambo kabla ya sinema.... Na huwezi kuwalaumu Hollywood.... Hawajawahi kuclaim kuwa matukio kwenye movie ni ya kweli... Ndio maana wanaweka categories ikiwamo fiction na documentaries
Wapi nimewalaumu Hollywood au niliposema zimeanzishwa na watu wa Hollywood? Nilichosema ni uzushi ULIOCHAGIZWA na Hollywood! Kutoka kwenye simulizi za kawaida na michoro; lakini yote hayo yakaja kupata umaarufu kutokana na filamu za Hollywood! Chukulia UFO kwa mfano... au hata Aliens... pamoja na kwamba palikuwa na simulizi za hapa na pale lakini wapo waliofikia kuamini masuala ya UFO na aliens baada ya Wajasiriamali wa Hollywood kutengeneza filamu kadhaa kuhusu UFO and aliens... same to vampires!
 
Habari zenu wakuu!
Nimekuwa interested kujua kama kweli vampire walikuwepo kama ninavyoona kwenye movies,na kama walikuwepo hawa wanaonekana kufanana na binadamu,..je ni nini kilitokea wakawa hivyooo(kisayansi uumbaji)!??

Pia kama mpenda movie za series unaeza kuwa unaifahamu movie ya supernatural humo ndani kuna SAM NA DEAN wanapambana na supernatural things,swali jingine kuna uwezekano hiyo series ikawa inaelezea uhalisia!?
 
Viasat History katika moja ya program zao kama sijakosea forbidden history, kuna kipindi wanazungumzia kwa kina hii kitu.
ni kwamba mnamo karne ya 17 nchi nyingi za Ulaya ziliamini uwepo wa vampires. pia yapo makaburi ya masalia ya watu wanaosemekana walikuwa vampires ama walikua katika hatua za kuwa vampires.
mengi ya mabaki hayo vichwa vimetenganishwa na viwiliwili au kuwekewa jiwe kwa juu, ili vampire asiweze kutoka usiku.
kwa kifupi ni imani tu za wakati huo, kwa kuwa hakuna uthibitisho wa kitaalam kama kweli walikuwepo ama la! ni nyakati ambazo nchi nyingi za ulaya ziliamini sana uganga na uchawi.
 
Wapi nimewalaumu Hollywood au niliposema zimeanzishwa na watu wa Hollywood? Nilichosema ni uzushi ULIOCHAGIZWA na Hollywood! Kutoka kwenye simulizi za kawaida na michoro; lakini yote hayo yakaja kupata umaarufu kutokana na filamu za Hollywood! Chukulia UFO kwa mfano... au hata Aliens... pamoja na kwamba palikuwa na simulizi za hapa na pale lakini wapo waliofikia kuamini masuala ya UFO na aliens baada ya Wajasiriamali wa Hollywood kutengeneza filamu kadhaa kuhusu UFO and aliens... same to vampires!
Ufo ni story ya ukweli
 
Ufo ni story ya ukweli
Hamna ukweli wowote ule... ni mambo/simulizi ambayo yalishika kasi sana enzi za vita baridi zikilenga sana kila mmoja (US-CIA/USSR-KGB) ku-divert attention ya mwenzake! Jiulize swali moja-- umeshawahi kusikia kuonekana kwa UFO popote pale duniani over the past 30 years?! Ikiwa enzi ambazo teknolojia haikuwa kubwa kama sasa bado UFO ziliweza kuonekana sehemu mbalimbali duniani; kwanini tushindwe kuziona siku hizi wakati teknolojia imekuwa maradufu?!
 
Kwa kua umeona kwenye movies kipo,hawa viumbe wapo,ukitaka kuamini haya mambo soma vitabu vinavyohusu secret societies, utajua ukweli wake,kama Mimi nilivyokuwa siamini uwepo Wa kiumbe mchanganyiko Wa Satan na binadam,lakini ni vitu vipo,kapakue kitabu kinaitwa The biggest secret,by David icke,aisee dunia INA mengi,
 
Kuna kitu mfano wa dish kubwa kilipita maeneo ya kwetu njombe mjini/chaugingi kilikua kinatoA mwanga mkali sana....umbali kama wa mita 10 toka ardhini,hakikuwA kinatoa mlio ila eneo lote lilikuwa na mwanga kamA mwezi umeshuka kwa maana ilikuwa usiku mida ya saa mbili...naweza kusema hiyo pengine ilikuwa UFO
 
Vampire wataanza kutokea 2040 ambapo mzungu atavumbua mashine za kufufua watu...kwa maana zaidi kuutoa ubongo kwenye mwili uliozeeka au kuumia vibaya na kuupeleka kwenye mwili salama (undamaged) ...maelezo zaid google...
 
Niliwahi sikia vampire wapo, ila so mama tuonavyo ktk movie , mama no Bulgaria , sjui Slovakia, kuna popo wanyonya damu, inasemekana wapo ktk mapango hao wakikuuma unabadilika na kuwa na vijitabia flan tofauti, pia kulikuwa na jamii ya mavampire ambao walikuwa wakila majani na damu ya wanyama was porini, Mimi naamini vampire wapo ila si mama tuonavyo ktk movie, kingine mwaka 2010 niliwahi kumuona mtoto Ana memo mama Vampire nchini Burundi, huyu mtoto baba yake ni mkongoman na mama yake ni mwarabu , wakati namuona huyu mtoto alikuwa na miaka minne alikuwa na meno marefu yale manne juu na chini pia yale meno hayakuwa meupe kama mengine, yale manne yalikuwa yana rangi kama ya dhahabu hivi , pia huyu mtoto alikuwa ana hasira muda wote na alikuwa anakula nyama mbichi kama haitawekwa sehemu nzuri, nilijaribu kuongea na mamayake kujua amechukua hatua gani kuhusu mwanaye akasema amejaribu kumpeleka kila mahari ,ila akasema huko Congo ukweni wamemwambia yule mtoto akifikisha miaka saba atakufa, au wakijaribu kuyatoa pia atakufa na ndio sababu wakahama congo kwenda burundi ili kunusuru maisha ya mwanae, wakati anasema hayo alikuwa mwenye huzuni sana, skupenda kuendelea kumuuliza maswali mengine sababu hata mimi sikujua ni jinsi gani ningemsaidia. Nikaishia hapo.. Mpaka leo sijajua hatma ya yule mtoto maana miaka saba ishafika sasa... Mimi naamini wapo ila si kama tuonavyo vituko vya wazungu.
 
Niliwahi sikia vampire wapo, ila so mama tuonavyo ktk movie , mama no Bulgaria , sjui Slovakia, kuna popo wanyonya damu, inasemekana wapo ktk mapango hao wakikuuma unabadilika na kuwa na vijitabia flan tofauti, pia kulikuwa na jamii ya mavampire ambao walikuwa wakila majani na damu ya wanyama was porini, Mimi naamini vampire wapo ila si mama tuonavyo ktk movie, kingine mwaka 2010 niliwahi kumuona mtoto Ana memo mama Vampire nchini Burundi, huyu mtoto baba yake ni mkongoman na mama yake ni mwarabu , wakati namuona huyu mtoto alikuwa na miaka minne alikuwa na meno marefu yale manne juu na chini pia yale meno hayakuwa meupe kama mengine, yale manne yalikuwa yana rangi kama ya dhahabu hivi , pia huyu mtoto alikuwa ana hasira muda wote na alikuwa anakula nyama mbichi kama haitawekwa sehemu nzuri, nilijaribu kuongea na mamayake kujua amechukua hatua gani kuhusu mwanaye akasema amejaribu kumpeleka kila mahari ,ila akasema huko Congo ukweni wamemwambia yule mtoto akifikisha miaka saba atakufa, au wakijaribu kuyatoa pia atakufa na ndio sababu wakahama congo kwenda burundi ili kunusuru maisha ya mwanae, wakati anasema hayo alikuwa mwenye huzuni sana, skupenda kuendelea kumuuliza maswali mengine sababu hata mimi sikujua ni jinsi gani ningemsaidia. Nikaishia hapo.. Mpaka leo sijajua hatma ya yule mtoto maana miaka saba ishafika sasa... Mimi naamini wapo ila si kama tuonavyo vituko vya wazungu.
Mtanisamehe keyboard inazingua nilikuwa hiyo mama inayojirudiarudia nilikuwa namaanisha kama
 
Kuna kitu mfano wa dish kubwa kilipita maeneo ya kwetu njombe mjini/chaugingi kilikua kinatoA mwanga mkali sana....umbali kama wa mita 10 toka ardhini,hakikuwA kinatoa mlio ila eneo lote lilikuwa na mwanga kamA mwezi umeshuka kwa maana ilikuwa usiku mida ya saa mbili...naweza kusema hiyo pengine ilikuwa UFO
Lini mkuu..? Mbona haikutangazwa
 
Binadamu unaweza ukawaza ndani ya boksi,nje ya boksi na ukaliondoa kabisa boksi.Hivyo hao watunzi movies hizo walijaribu tu kuwaza nje ya boksi na haina uhalisia wowote
 
Lini mkuu..? Mbona haikutangazwa
Ilikuwa ni zamani sana,kila mtu aliamini ni ndege,sasa muda ulivyoenda nikaanza kuhoji kwa kuzingatia kigezo cha kuwa ndege haiwez kupita usawa huo pia labda ingekuwa helcopter ambayo lazima tungesikia makelele....
 
Vampire ni story za zamani ambazo watu wa ulaya Mashariki walikuwa wanaamini baadhi ya watu waliyefariki baada ya kuzikwa walikuwa wana toka makaburini kama ghost au mizimu na kuongea na ndugu zao kwa kutaka damu na kama wakikosa wana kunyonya kimiujiza mpaka unakufa na unaweza kuuwa ndugu wengi na majirani mpaka wazee wafanye kitu ktk kaburi.

Kiasi kwamba kuna wengine wakawa wanazika huku wakiwa wamemkata marehemu kichwa ili asiamke tena au wanatoboa moyo na kisu ili asipate uhai tena kaburi.

Wengine wakawa wanazikwa kichwa chini miguu juu ili asifufuke tena.

Na wengine wengi walihisisha na mambo ya uchawi,mapepo na majini na ikaenea sana tu ulaya Mashariki mpaka amerika ya kusini na China.

Kwa hiyo hizi hadithi zimekuwa zikisimuliwa kizazi hadi kizazi hatimaye mpaka Hollywood wakaanza kutengeneza filamu zake.
 
Back
Top Bottom