Ukweli kuhusu kile kinachoitwa Chunusi

Ukweli kuhusu kile kinachoitwa Chunusi

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,396
Reaction score
829,698
Kwanza Niombe radhi kwa kuahidi mara nyingi kuweka hii post lakini bila kufanya hivyo!

Tunazungumzia chunusi mnyama, shetani, jini au kizuka. Sio chunusi zile za usoni zinazotokana kwa sehemu kubwa kuibana au kuwa domozege! Hapa ni chunusi mtoa roho, majini.

Tumekulia kwenye hizo habari, tumepoteza ndugu jamaa na hata marafiki huko kwenye mito maziwa na hata baharini sababu ikitajwa kuwa ni chunusi.

Ukweli huu hapa
1. Chunusi wa kishirikina - Hapa ni kiumbe jini ndio kinaua kimazingara na binadamu kutafsiri kuwa ni chunusi (nimeshindwa kwa hakika kupata uhalisia na chanzo cha chunusi kuhusishwa na maji)

1475754511072.jpg


2. Wanyama wa majini(kwenye maji). Wapo wanyama wasiojulikana sana waishio kina kirefu cha maji ambao nao kwa namna moja au nyingine wamesababisha mauaji na kudhaniwa kuwa ni chunusi - hapa hakuna chembe ya ushirikina.

1475754479974.jpg


3. Chunusi kutokana na mkondo wa maji (strong current) Haya ndio yanaweza kuwa maelezo sahihi zaidi kuhusu chunusi.

Mara nyingi chini ya uso wa maji hupita mikondo ya maji inayoenda kasi sana na inayopita kina kirefu cha maji. Mikondo hii iko ya aina mbili;

- Mikondo ya maji inayoonekana juu ya uso wa maji
- Mikondo ya maji isiyoonekana juu ya uso wa maji.

Hii sasa ndio hatari sana kwa kuwa ukiangalia utaona maji yametulia kabisa lakini kumbe huko chini yake ni habari nyingine

1475754854033.png

1475754870751.png


Wenzetu ambao sio wavivu wa kufikiri waliamua kufanya utafiti wa kwanini kuna baadhi ya maeneo yanaua sana (dhana ya chunusi) na hiki ndicho walichogundua na kuweka tahadhari kwa wasiojua.
1475755013961.jpg


Sisi tumekuzwa na hulka moja mbaya sana ya kupuuzia mambo hata kama kuna chunusi wa kichawi lakini ufafanuzi wa jinsi hii ungehitajika!

Kumbuka bado tuko kwenye msiba wa ndugu zetu watatu waliopoteza maisha kwa kudhaniwa ni mumiani wanyonya damu. Tungekuwa na matangazo kwenye vyombo vya habari yanayotoa elimu na ufafanuzi kuhusu mambo kama haya wale ndugu pengine wangesalimika.

Kwenye dhana nzima ya chunusi inasemekana kuna chunusi wa aina mbili;

A. Chunusi anayeua na kuondoka na maiti (uhalisia ni mkondo mkali wa maji)

B. Chunusi anayeua na kuacha maiti akinyonya damu tuu (uhalisia ni kifo kinachotokana na viumbe wa majini)

Hizi za mwisho ni picha zinazodhaniwa ni za chunusi ambao wamewindwa na kuuawa na sasa nyama yao iko sokoni (sio Tanzania).

1475755446791.jpg
 
The King of Msata at his best.

Halafu hizi rip currents hata uwe mwogeleaji kumzidi Michael Phelps ukinasa umenasa aisee. Halafu watu wanabaki wanashangaa mwogeleaji mzuri yule hawezi kuzama lazima atakuwa amechukuliwa kichawi kumbe masikini umeburuzwa na kuwa squeezed na presha kali ya maji kama kimwanasesere tu. Na ukipanick na kujaribu kushindana na mkondo wenyewe ndo kabisa huponi.

Uchawi ndiyo upo lakini tukifikia mahali tukiona tukio tunatafuta kwanza sababu za kisayansi kabla ya kukimbilia ushirikina tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana. Siyo kila kitu ni ushirikina!
 
hizi za mwisho ni picha zinazozdhaniwa ni za chunusi ambao wamewindwa na kuuawa na sasa nyama yao iko sokoni (sio Tanzania)
Kwa hiyo nyama yao inaliwa ama wanaozinunua wanaenda kuzitumia kwa mambo ya kiuchawi
 
Mkuu miaka ya 90 maeneo ya mbagala mimi nilishuhudia tulienda kuoga kwenye Bwawa tena huwa lina jaa msimu wa mvua tu kiangazi kaji yote yanakauka kuna kijana mwenzetu alizama kwa masaa mengi kidogo ila alipoibuka alikuwa maiti tayari.

Hizo sababu za kisayansi naona zinaelezea zaidi kwenye mito au bahari so vipi kwenye haya maji yaliyotuama ambayo hayatembei tena?
 
The King of Msata at his best.

Halafu hizi rip currents hata uwe mwogeleaji kumzidi Michael Phelps ukinasa umenasa aisee. Halafu watu wanabaki wanashangaa mwogeleaji mzuri yule hawezi kuzama lazima atakuwa amechukuliwa kichawi kumbe masikini umeburuzwa na kuwa squeezed na presha kali ya maji kama kimwanasesere tu. Na ukipanick na kujaribu kushindana na mkondo wenyewe ndo kabisa huponi.

Uchawi ndiyo upo lakini tukifikia mahali tukiona tukio tunatafuta kwanza sababu za kisayansi kabla ya kukimbilia ushirikina tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana. Siyo kila kitu ni ushirikina!
1475757201002.jpg
1475757207371.jpg
 
Eeehee Baba Wewe utaacha Uchawi lini Baba angu
Hahahaa! Mkuu umenichekesha? Lakini Mshana katoa somo zuri sana, we wamwita mchawi tena, wakati mwngn watu husema uchawi upo kwa anaeamini lkn asiye amini hupoteza muda mwingi kufanya tafiti (wazungu), hapa simaanishi uchawi haupo, upo! https://www.google.com/url? sa=t&source=web&rct=j&url=http://www.thywordistruth.com/quest...ggyMAQ&usg=AFQjCNFRXKw5hU089BmAN8Jtwuh4fPrTwQ na ndicho walichokifanya kutafiti kujua the hidden truth.
 
Kwanza Niombe radhi kwa kuahidi mara nyingi kuweka hii post lakini bila kufanya hivyo!
Tunazungumzia chunusi mnyama shetani jini au kizuka sio chunusi zile za usoni zinazotokana kwa sehemu kubwa kuibana au kuwa domozege! Hapa ni chunusi mtoa roho majini
Tumekulia kwenye hizo habari, tumepoteza ndugu jamaa na hata marafiki huko kwenye mito maziwa na hata baharini sababu ikitajwa kuwa ni chunusi
Ukweli huu hapa
1.chunusi wa kishirikina- hapa ni kiumbe jini ndio kinaua kimazingara na binadamu kutafsiri kuwa ni chunusi (nimeshindwa kwa hakika kupata uhalisia na chanzo cha chunusi kuhusishwa na maji)View attachment 413290
2.wanyama wa majini(kwenye maji)wapo wanyama wasiojulikana sana waishio kina kirefu cha maji ambao nao kwa namna moja au nyingine wamesababisha mauaji na kudhaniwa kuwa ni chunusi- hapa hakuna chembe ya ushirikina View attachment 413289
3.chunusi kutokana na mkondo wa maji (strong current! Haya ndio yanaweza kuwa maelezo sahihi zaidi kuhusu chunusi
Mara nyingi chini ya uso wa maji hupita mikondo ya maji inayoenda kasi sana na inayopita kina kirefu cha maji..mikondo hii iko ya aina mbili
- mikondo ya maji inayoonekana juu ya uso wa maji
-mikondo ya maji isiyoonekana juu ya uso wa maji
Hii sasa ndio hatari sana kwakuwa Ukiangalia utaona maji yametulia kabisa lakini kumbe huko chini yake ni habari nyingine View attachment 413300View attachment 413301wenzetu ambao sio wavivu wa kufikiri waliamua kufanya utafiti wa kwanini kuna baadhi ya maeneo yanaua sana (dhana ya chunusi) na hiki ndicho walichogundua na kuweka tahadhari kwa wasiojua View attachment 413302
Sisi tumekuzwa na hulka moja mbaya sana ya kupuuzia mambo
Hata kama kuna chunusi wa kichawi lakini ufafanuzi wa jinsi hii ungehitajika! Kumbuka bado tuko kwenye msiba wa ndugu zetu watatu waliopoteza maisha kwa kudhaniwa ni mumiani wanyonya damu
Tungekuwa na matangazo kwenye vyombo vya habari yanayotoa elimu na ufafanuzi kuhusu mambo kama haya wale ndugu pengine wangesalimika
Kwenye dhana nzima ya chunusi inasemekana kuna chunusi wa aina mbili
A. Chunusi anayeua na kuondoka na maiti(uhalisia ni mkondo mkali wa maji)
B. Chunusi anayeua na kuacha maiti akinyonya damu tuu (uhalisia ni kifo kinachotokana na viumbe wa majini)View attachment 413304hizi za mwisho ni picha zinazozdhaniwa ni za chunusi ambao wamewindwa na kuuawa na sasa nyama yao iko sokoni (sio Tanzania)
Haya mambo huwa yananisumbua sana umejaribu kunieleza maana kuna rafiki yangu aliwai kufa Ziwa victory kuna bichi inahitwa Mamba beach, yaani alikuwa anajua kuogelea balaa mpaka wingereza alifika kwa ajili ya kuogerea lakini alikufa hapo mamba beach mwanza maeneo kama unakwenda airport ya mwanza baada ya kuliwa na maji kuna mtu alisema huyu mwezenu mtampata kesho muda kama huu aliozama, tuliita watu wa kuzamia majini wa aina zote lakini hatukumpata mpaka ilipofika kesho yake mida kama ile ndio wazamiaji kutoka South Africa walimkuta amenasa kwenye tope yaani tulilia sana huwa kitu icho uwa kinanisumbua sana kwakweli wenyeji walituambia ameliwa na chunusi.
 
mkuu na wadada warembo ambao nusu mtu chini samaki huwa inasemekana wanakuaga baharini ukienda kuogelea wanakuitia katikat ya maji ni nani wale
Nguva navyo ni viumbe bahari vya kufikirika na ilivyo kwa dragons hata kama vilikuwepo ilikuwa ni zamani sana siku hizi havipo tena
1475757994959.jpg
na hata troojan pia
1475758017241.jpg
 
Mkuu miaka ya 90 maeneo ya mbagala mimi nilishuhudia tulienda kuoga kwenye Bwawa tena huwa lina jaa msimu wa mvua tu kiangazi kaji yote yanakauka kuna kijana mwenzetu alizama kwa masaa mengi kidogo ila alipoibuka alikuwa maiti tayari.

Hizo sababu za kisayansi naona zinaelezea zaidi kwenye mito au bahari so vipi kwenye haya maji yaliyotuama ambayo hayatembei tena?
Kuna wakati sehemu kama hizo huwa na viumbe wa ajabu ambao hutoweka baada ya maji kukauka lakini pia ishu za kichawi zinahusika hapo hasa ukizingatia na hilo eneo lenyewe la mbagala
 
Haya mambo huwa yananisumbua sana umejaribu kunieleza maana kuna rafiki yangu aliwai kufa Ziwa victory kuna bichi inahitwa Mamba beach, yaani alikuwa anajua kuogelea balaa mpaka wingereza alifika kwa ajili ya kuogerea lakini alikufa hapo mamba beach mwanza maeneo kama unakwenda airport ya mwanza baada ya kuliwa na maji kuna mtu alisema huyu mwezenu mtampata kesho muda kama huu aliozama, tuliita watu wa kuzamia majini wa aina zote lakini hatukumpata mpaka ilipofika kesho yake mida kama ile ndio wazamiaji kutoka South Africa walimkuta amenasa kwenye tope yaani tulilia sana huwa kitu icho uwa kinanisumbua sana kwakweli wenyeji walituambia ameliwa na chunusi.
Huyo kwa vyovyote (ukiachana na dhana ya uchawi)alinasa kwenye mkondo wa maji kupwa ama kujaa ambayo round yake huchukua masaa 24 kamili! Nilimpoteza ndugu yangu miaka ya 80 kifo chake kinafanana sana na hiki cha jamaa yako
 
Asante mkuu. Mwaka juzi nilibahatika kufika Waikiki Beach Honolulu kwa wiki tatu. Wanachukulia rip currents seriously na maonyo yapo kila mahali. Hata wale surfers wazoefu huwa inatokea wakinasa hawachomoki. Hata baharini sikuingia kwa woga. Niliishia kupata helicopter tour tu na kwenda Pearl Harbor kuona kitu ambacho Wajapan waliacha hapo.

Halafu pengine waweza kunisaidia katika hili. Tulipoenda Kilauea volkeno tulikatazwa kubeba lava iliyopoa kama souvenir. Wengine walisema eti ni hatari kupanda ndege na hiyo lava lakini sababu hasa ilikuwa ni imani za kishirikina na kuna tetesi kwamba ukichukua hayo mawe ukifika nayo nyumbani basi mikosi inakuandama na hata vifo. Kwa uzoefu wako unafikiri kuna ukweli katika hili?
 
Asante mkuu. Mwaka juzi nilibahatika kufika Waikiki Beach Honolulu kwa wiki tatu. Wanachukulia rip currents seriously na maonyo yapo kila mahali. Hata wale surfers wazoefu huwa inatokea wakinasa hawachomoki. Hata baharini sikuingia kwa woga. Niliishia kupata helicopter tour tu na kwenda Pearl Harbor kuona kitu ambacho Wajapan waliacha hapo.

Halafu pengine waweza kunisaidia katika hili. Tulipoenda Kilauea volkeno tulikatazwa kubeba lava iliyopoa kama souvenir. Wengine walisema eti ni hatari kupanda ndege na hiyo lava lakini sababu hasa ilikuwa ni imani za kishirikina na kuna tetesi kwamba ukichukua hayo mawe ukifika nayo nyumbani basi mikosi inakuandama na hata vifo. Kwa uzoefu wako unafikiri kuna ukweli katika hili?
Kuna hizo imani kwakuwa hata mimi nilishataka kubeba(ilikuwa Taiwan mji wa Taijong)lakini tukakatazwa nafikiri hii iko kiimani zaidi japo kuna mmoja alisema kuwa volcano iliyopoa ina reactors segments( sikuwahi kuelewa sana)
 
Back
Top Bottom