Kinachopingwa si umaarufu wa Prof. Lipumba, hapana Prof. Lipumba ni maarufu.
Kinachopingwa si usomi wa Prof. Lipumba, la hasha, usomi wa Prof. hauna shaka.
Kinachopingwa si tendo la kupokewa na CUF, hapana, wanampokea mwenyekiti wao.
Hebu tuangalie hii ripoti;
Umati wa wafuasi wa Chama cha Wananchi CUF hii leo umejitokeza kumpokea Mwenyekiti wa Chama hicho Profesa IBRAHIM LIPUMBA aliyekuwa nchini Marekani kwa kazi maalum aliyopewa na Umoja wa Mataifa kwa lengo la kuangalia njia bora zinazoweza kutumika katika kurekebisha uchumi wa dunia uliporomoka hususani kwa mataifa yanayoendelea.
Kinachopingwa ni sababu inayotolewa na CUF ya kupewa hayo mapokezi.
Kinachopingwa ni uwongo unaotolewa na CUF kuhusu safari ya Prof. Lipumba.
Kinachopingwa ni sifa anayopewa Prof. Lipumba kuhusiana na safari yake hiyo.
Kwanza, hakuna kazi yoyote maalum aliyopewa na Umoja wa Mataifa, huu ni uongo wa kwanza.
Pili, safari yake nchini Marekani haukuwa na uhusiano wowote na uchumi wa dunia, uwongo wa pili.
Tatu, nini lengo la CUF kuudanganya Umma na inapata faida gani kwa kuwadanganya wafuasi wake?
Jibu la swali hili lipo wazi kwa yeyote mwenye mwenye pua anuse, mwenye sikio asikie na mwenye jicho aone!
Tukumbuke pia hata Raisi aliombwa na CUF akampokee shujaa huyu aliyeliletea taifa heshima kubwa!