Ukweli kabisa maisha ni magumu

Ukweli kabisa maisha ni magumu

Prof Koboko

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2020
Posts
350
Reaction score
2,550
Kuficha kusema ukweli ni ujinga na unafki. Ndani ya miaka hii 5 maisha yamekuwa magumu kupita kiasi kwa sababu ya serikali ya CCM.

Wao wamehodhi madaraka wanalipana mishahara mizuri na marupurupu na kupandishana vyeo tu, pesa hakuna wamewabana watumishi wa umma hawawaongezei mishahara na wamewaondolea allowances. Hii haikubaliki!

Unadanganya mtu eti unajenga nchi hupandishi mishahara, hii siyo sawa. Gharama za maisha zinapanda kipato kipo pale pale. Biashara haziendi kwa sababu mmeua uchumi wa watu.
 
Uchumi wa wananchi umekua, alisikika mlevi mmoja akisema huko ‘sadeki’!
 
Hakuna Rais atakaeingia madarakani akuletee mkate ule na familia yako, never

Kikubwa Ni kupambana mwenyewe na kuangalia fursa zinazokuzunguka eneo ulipo na kutengeneza kipato Cha ziada !!
 
Cha kushangaa tarehe 28 bado utachagua haohao waliosababisha hali ngumu.
 
2020 ni Yeye hii haina kutafuna maneno miaka 5 mmetunyonga kama mtuitavyo tena mitano mingine mtunyonge ? Hapana kwakweli pumzikeni sasa mle mlivyo vuna miaka 5 angalau na sisi wanyonge wenu tupate unafuu wa maisha make sio kwa kutunyonga huku na jina mmetuita wanyonge
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom