Zheneba
Member
- Aug 5, 2011
- 75
- 9
Leo ni siku ya nane hakuna maji Kahama kwa sababu TANESCO wamewakatia umeme, sisi wananchi tunalipa bili kwa wakati na usipolipa unakatiwa maji hivi hela zetu zinaenda wapi? Kama wangetenga kila mwezi walipe hata milioni 10 TANESCO sidhani kama wangekatiwa umeme.
Hali ya vyoo hasa mahospitali, mashuleni na majumbani ni mbaya sana, Leo buchani hakuna nyama maana hakuna maji machinjioni muda si mrefu milipuko ya magonjwa itaanza.
Hata hivyo imeonyesha wazi Mkurugenzi wa KASHUWASA ameshindwa kazi aondolewe.
Hali ya vyoo hasa mahospitali, mashuleni na majumbani ni mbaya sana, Leo buchani hakuna nyama maana hakuna maji machinjioni muda si mrefu milipuko ya magonjwa itaanza.
Hata hivyo imeonyesha wazi Mkurugenzi wa KASHUWASA ameshindwa kazi aondolewe.