Ukomo wa ajira vyeti feki huu

Ukomo wa ajira vyeti feki huu

umesaidiaje kwenye hili wewe,umetoa tarifa takukuru au polisi?
Tunaamini wanafanya kazi kwa umakini wa hali ya juu sana hasa ukizingatia mda ulio tumika na unaoendelea kutumika kutekeleza zoezi hilo , na isitoshe wanatumia mitambo na technology pia hivyo nadhani walisha jiridhisha na utendaji wao, Na wangekuwa wanahitaji manual work kwenye hili wangetushirikisha hilo, lakini walikuja na mbinu zao ambazo waliona ni bora zaid na hazikwepeki hivyo mimi sina mamlaka juu ya hilo.
 
Kifupi zoezi litaisha pale Pogba atakaposema liishe, akiamua hata leo utasikia uhakiki umekamilika na akiamua wandelee hadi 2018 wataendelea tu.
 
Inauma sana.. Waliogundulika na vyeti feki bado wanakula bata.. Wanaosubiri marekebisho ya kada na kupandishwa vyeo wanaendelea kusafa.. Binafsi naamini tatizo ni fedha and nothing else
 
huyu ni kazi ya mawaziri wadada wasio wachoyo.....
 
Kinacho nishangaza kuna watu hawana vyeti na wengine wana share vyeti na wengine wanvyo feki bado wapo na wanalamba salaries kama kawa sijui walikuwa wana hakiki nini maana hata siwaelewi hawa watu ,nguvu nyingi matokeo hakuna.
Mapema sana tulimwambia huyu Kairuki kwamba mkishafika jeshini na polisi mtakwama , na hizi zoooote ni porojo tu , kule bandarini huo uzushi wa vyeti umefutwa na vijana wanaendelea na kazi na wanalamba mshahara mnono kwa vyeti vya Kariakoo - Gerezani .

Uhakiki wa zaidi ya mwaka kwa wafanyakazi wasiozidi laki 6 ni uongo wa kishamba sana .
 
Mtoto wa Masikini Cheti feki atakipatia wapi? Tunapohoji tuwe tunajaribu kufikiria kwanza. Kwanza Fake Certificate inategemea na Uchumi wa mtu. Maana Cheti hicho hununuliwa kwa gharama kubwa.
Upo wewe unayehoji?
Mimi ni mtoto wa masikini Ila nina gamba feki mkuu, usigeneralize
 
Mwigulu Nchemba alishawahi kutamka hapa jukwaani kuwa Yeye Binafsi asingependa zoezi hili liendelee maana linapoteza watu wenye ujuzi na uzoefu wa kazi. Kwa hili nilimuelewa Mwigulu
 
Mwigulu Nchemba alishawahi kutamka hapa jukwaani kuwa Yeye Binafsi asingependa zoezi hili liendelee maana linapoteza watu wenye ujuzi na uzoefu wa kazi. Kwa hili nilimuelewa Mwigulu

Kwa hiyo watu waache kupiga shule watagute tu vyeti feki ili mradi wawe na ujuzi sio? Hajaniingia akilini hii
 
Kwa hiyo watu waache kupiga shule watagute tu vyeti feki ili mradi wawe na ujuzi sio? Hajaniingia akilini hii
Hahahaha Mpwa unachanganya madesa! Point yake ni kwamba umeshaajiri watu, umeshawafunza kazi, others are good performers halafu from nowhere unawaondoa! Kwa mfano, ukienda kwa Walimu ndio utashangaa! Tanga-Korogwe walikutwa Walimu wenye vyeti feki kama mia tatu-300, Lushoto Tanga wakakutwa kama 250! Kwa Wilaya hizi mbili tu ukisema uwaondoshe INA maana utakua na uhaba wa Walimu kama 500-600, je ni chuo gani kinaweza kuzalisha Walimu wa ku-replace hawa Walimu? Lakini pia kumbuka kuwa Kuna Wakaguzi Wa Elimu ambao huwa wanawakagua kila Mwaka na kuwafanyia marekebisho! Hakuna Mkaguzi aliyewahi kuwasimamisha kwa kushindwa kufundisha kwa kuwa wana Vyeti Feki..... Huo ni mfano tu.

Mwisho, serikali imeshindwaje kuhakiki na kumaliza Hao Wafanyakazi kwa zaidi ya miezi 12 sasa??
 
HILI ZOEZI LINGEENDA BILA KUATHIRI SHUGHULI ZINGINE LINGEKUWA ZURI SANA. ILA KWA VILE SIKU ZOTE SERIKALI YA SISIEM NI YA UFISADI, UVIVU NA UPIGAJI DILI NDIYO MAANA HAIWEZEKANI KUMALIZIKA KWA MUDA MFUPI.
WATASINGIZIA UHAKIKI HUKU WANAPIGA DILI MPAKA TUNAINGIA 2018. Wao waseme tu hawana pesa za kuajiri na kutoa increment basi kuliko hiz drama wanazifanya.
HUYU MAMA ANAKULA NA KUNYWA PAMOJA NA FAMILIA YAKE LINI ATASIKIA MAUMIVU YA WATU WENGINE? Ubabe tu akili ndogo
 
Back
Top Bottom