Ubumuntu
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 14,316
- 10,782
Salaam wana JF!
Nimekua nikijiuliza mara nyingi,hivi ni lini TZ yetu itakombolewa kutoka kwenye huu utawala dhalimu? Na mara zote sipati jibu la uhakika! Nimejiuliza tena,hivi kuna chama cha siasa ambacho kinaweza kututoa waTZ kwenye hili janga la shida na umasikini? Hapa pia naona chenga tu!
Lakini mwishowe nimekuja kufahamu kua ukombozi wa kweli utafanikiwa pale sisi raia tutakapoamua kuushikisha adabu utawala huu dhalimu. Pale raia tutakapoifanya serikali ituogope na si sisi tuigope! Na wasaa huu hauletwi na wala hautaletwa na chama chochote cha siasa!
Kwa hiyo waTZ tusitarajie chama chochote ndio kiwe mstari wa mbele katika kuuongoza mapambano ya kutafuta ukombozi wetu! Maana siku za hivi karibuni kumekua na hisia kua chama fulani ndio kiongoze mapambano ya ukombozi;chama fulani ndio kiandae maandamano ya kudai serikali ipunguze ukali wa maisha n.k. Kwa namna hiyo ndugu zangu tutasubiri mpaka Yesu atakaporudi!
Ndugu zangu UKOMBOZI utaletwa na sisi raia! Hivyo ni wakati muafaka wa sisi kuanza kuifanya serikali itimize wajibu wake kwa raia. Na katika nchi za kidemokrasia,maandamano ndio njia kuu ya kuishurutisha serikali.
WaTZ tuwe na mioyo ya uthubutu,tutoe hofu (najua baadhi yetu tunaweza kuuwawa au kujeruhiwa) na tuwe tayari kuikomboa nchi yetu. Wakati ni huu!
Haya ni mawazo yangu,kukosolewa kunaruhusiwa!
Nimekua nikijiuliza mara nyingi,hivi ni lini TZ yetu itakombolewa kutoka kwenye huu utawala dhalimu? Na mara zote sipati jibu la uhakika! Nimejiuliza tena,hivi kuna chama cha siasa ambacho kinaweza kututoa waTZ kwenye hili janga la shida na umasikini? Hapa pia naona chenga tu!
Lakini mwishowe nimekuja kufahamu kua ukombozi wa kweli utafanikiwa pale sisi raia tutakapoamua kuushikisha adabu utawala huu dhalimu. Pale raia tutakapoifanya serikali ituogope na si sisi tuigope! Na wasaa huu hauletwi na wala hautaletwa na chama chochote cha siasa!
Kwa hiyo waTZ tusitarajie chama chochote ndio kiwe mstari wa mbele katika kuuongoza mapambano ya kutafuta ukombozi wetu! Maana siku za hivi karibuni kumekua na hisia kua chama fulani ndio kiongoze mapambano ya ukombozi;chama fulani ndio kiandae maandamano ya kudai serikali ipunguze ukali wa maisha n.k. Kwa namna hiyo ndugu zangu tutasubiri mpaka Yesu atakaporudi!
Ndugu zangu UKOMBOZI utaletwa na sisi raia! Hivyo ni wakati muafaka wa sisi kuanza kuifanya serikali itimize wajibu wake kwa raia. Na katika nchi za kidemokrasia,maandamano ndio njia kuu ya kuishurutisha serikali.
WaTZ tuwe na mioyo ya uthubutu,tutoe hofu (najua baadhi yetu tunaweza kuuwawa au kujeruhiwa) na tuwe tayari kuikomboa nchi yetu. Wakati ni huu!
Haya ni mawazo yangu,kukosolewa kunaruhusiwa!