Ukomavu mkubwa wa kisiasa CHADEMA

Ukomavu mkubwa wa kisiasa CHADEMA

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
17,285
Reaction score
23,584
Napenda kuipongeza CHADEMA kwa ukomavu mkubwa wa kisiasa walioonesha katika kipindi hiki kigumu cha mpito na mtikisiko mkubwa wa kisiasa kuwahi kutokea ndani ya chama.

Wengi walifikiri
CHADEMA ingepasuka vipande vipande pale Zito alipotoka, lakini CHADEMA imebaki imara na kuendelea hata kuwa na nguvu zaidi, aliyepasuka ni Zito mwenyewe.

Halafu watu walifikiri
CHADEMA ingevunjika aliporudi nyuma Dk Slaa, lakini nimefurahishwa na ukomavu wa wanachadema kwani wameona kuwa hata bila ya Slaa CHADEMA inawezekana na wamebaki kuwa wamoja na chama kimekuwa na nguvu hata zaidi ya huko nyuma.

Tuendeleze mshikamamo kwani adui wa taifa letu siyo mtu binafsi ni mfumo mzima wa CCM.
 
Kama ilivyo kwa msemo wetu kuwa cdm ni tunu ya taifa na tulianza na mungu na tutamaliza na mungu
 
Mbowe alifanya kazi sana bila kulala hadi akaanguka kwa fatigue. Bravo Kamanda Mbowe. Umeonyesha ukomavu na ujasiri wa hali ya juu sana. "Mwenyezi Mungu azidi kukutia nguvu!" Amina!
 
upepo umeshapuliza nyeti za kuku hakuna namna ya kuikowa ccm labda watuuwe vijana wote kitu ambacho ni vigumu !!
 
Fuatilieni na mchakato wa daftari la wapiga kura na zoezi zima la upigaji wa kura. Safari hii hatutaki kelele za kuchakachuliwa matokeo yatakapotolewa. Mpaka leo nasubiri ahadi ya Dr. Slaa ya kueleza kwa uwazi yeye na CHADEMA walivyochakachuliwa kura za uraisi za mwaka 2010 lakini hola.
 
Napenda kuipongeza CHADEMA kwa ukomavu mkubwa wa kisiasa walioonesha katika kipindi hiki kigumu cha mpito na mtikisiko mkubwa wa kisiasa kuwahi kutokea ndani ya chama.

Wengi walifikiri
CHADEMA ingepasuka vipande vipande pale Zito alipotoka, lakini CHADEMA imebaki imara na kuendelea hata kuwa na nguvu zaidi, aliyepasuka ni Zito mwenyewe.

Halafu watu walifikiri
CHADEMA ingevunjika aliporudi nyuma Dk Slaa, lakini nimefurahishwa na ukomavu wa wanachadema kwani wameona kuwa hata bila ya Slaa CHADEMA inawezekana na wamebaki kuwa wamoja na chama kimekuwa na nguvu hata zaidi ya huko nyuma.

Tuendeleze mshikamamo kwani adui wa taifa letu siyo mtu binafsi ni mfumo mzima wa CCM.

CHADEMA ni mpango wa MUNGU.
 
Kura si kigezo pekee cha uhalali wa kuongoza watu zaidi ya million 40, ndio maana wako wasiopiga kura na bado katiba inawapa haki na wajibu wa kuheshimu mamlaka ya Urais, ukiacha kura mgombea ajipime kwa namna anavyoungwa mkono na anaowaongoza.

Unaweza kuanza kutoa tathmini ni mgombea gani mpaka sasa anayeungwa mkono mijini, kabla hata ya kampeni, rejea jk alipoingia madarakani 2005, muelekeo wa ushindi wa kishindo ulianza pale tu alipoonyesha nia na kupitishwa na chama chake. Watu tulijitokeza kila alipopita kuonyesha namna tulivyokuwa na imani naye, na matokeo yaliakisi uungwaji mkono wa wazi, hakuhitaji mkapa ampigie kampeni kuweza kushinda, alisimama kwa miguu yake mwenyewe kwa kushirikiana na washirika wake, ikamuwezesha kushinda kwa kishindo bila ubishi.

Vivyo hivyo hivi sasa tuanze kufanya tathmini namna wagombea wanavyo hitaji backup ya hali ya juu kuweza kusimama, hii inatukumbusha mwalimu nyerere aliposema "mjue mtu mnaye mchagua ni lazima akubalike, kwa kuwa hatakuwa kiongozi wa ccm peke yake ila Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo ni lazima akubalike na umma".

Nguvu kubwa inatumika kuwachafua wagombea walioruhusiwa kuchukua fomu kwenye vyama vyao hapo kabla, ikidhihirisha vigezo walivyokuwa navyo, na sasa wamehama, tuhuma peke yake haziondoi haki kwa anaye tuhumiwa, hasa ukizingatia kwamba tuhuma nyingi za kisiasa ni chuki zinazolenga kuwathoofisha washindani, mfano na wajibu wa kuwashitaki waliohusika kwenye kashfa ya Richmond ilibaki kwa waliomadaraki kwa miaka zaidi ya saba, hii ikimaanisha kwamba tuhuma hazikuwa na mashiko na uhalali wa kuwashitaki mliwachafua.

Mliopo madarakani mtujuze vision ya taifa iko wapi?, ahadi mlizo toa tangu awamu ya kwanza ni kwa kiasi gani zimetekelezwa?, mnahitaji miaka mingine mingapi kukamilisha ahadi mpya na za zamani?, kapu la madeni limejaa kwa kiasi gani?, shillingi ya Tanzania inakwenda wapi?, ongezeko ajira kupitia viwanda limefikia wapi?, na mwisho takwimu za idadi ya watu wasiojua kesho yao?

Itaendelea muda mfupi ujao....................
 
Back
Top Bottom