Uko wapi ukweli kuhusu panya road?

Uko wapi ukweli kuhusu panya road?

Omba yasikukute. Pale Tabata kisiwani watu wamechezea visu na mapanga halafu wewe unaleta utani.

Kunduchi hadi mtoto wa miaka Tisa/9 kala mapanga ya panya road halafu wewe unaleta story za sungura na fisi.

Jaribu kufatilia vyombo vya habari hasa TV ili ujionee kwa macho sio kushinda tu Instagram kuangalia makalio ya kina Gigy money.
Nazani hujanielewa kausome tena na tena ili unielewe nacho maanisha.
Kuna wajinga wachache ndio muna kuza mambo haya Panya Road wamevamia tabata, Mbagala wanakimbizana. Alie kwenye daladala anaenda kigamboni anaenda sema Panya Road wapo Mbagala.huo upuuzi unasambaa kwa stahili hiyo.
NB:
Sina Account Instagram, na sina muda na kufuatilia maisha ya watu.
 
Habari Mabibi na Mabwana wa Jf;

Haya matukio ya Panya Road kwa sasa yamekua yana tatanisha sana.
Mfano Mimi ni mkazi wa Temeke (Tandika) sikuwai kusikia wala kuona Panya Road.

Lakini cha ajabu nikienda kazini maeneo ya Sinza nawasiki watu wanahadisia kua Panya Road wamevamia Temeke (Tandika ).

Basi nabaki najiuliza, mbona mimi nakaa huko na hiyo siku ambayo wanasema Panya Road wamevamia nilishinda uko na nikawa ktk mizunguko mpaka saa 4 Usiku sikusikia wala kuona Panya Road?.

Hii inanifanya nikumbuke story ya Babu yangu, kuhusu Mwizi Maaru hapa jijini Dar alieitwa MAHMOUDU.
Ipo hivi;

Miaka ya nyuma kulitokea Mwizi maarufu kwa jina MAHMOUDU, kipindi hicho Dar yote kituo cha polisi kilikua Msimbazi Police tu ukiondoa makao Mkuu Centre, hii zamani kidogo.

Kesi za wizi zilizokua zikilipotiwa zote mtuhumiwa wao ni MAHMOUDU.

Haijalishi mleta mashtaka katokea wapi iwe Magomeni au Temeke, tena hata kama matukio yalitokea kwa wakati Mmoja.

Police walimtafuta MAHMOUDU na kumuweka ndani, chakushangaza kesi zikawa zinakuja na mtuhumiwa wao ni yuleyule bwana MAHMOUDU.

Sasa hawa Panya Road kweli wapo kama tunavyo Peana taarifa au tunatishana tu na kulikuza hili jambo.
The reason ni kwamba Sirro na Maza hawapo in good term....huenda Sirro anataka kumwamisha maza kuwa anafanya kazi (Kwerikweri In Magu Voice) maana kila tukisikia Panya road leo, kesho tunasikia wamekamatwa!!
 
Back
Top Bottom