Black poison The Factor
JF-Expert Member
- May 31, 2020
- 854
- 1,257
Wakuu niende kwenye mada moja kwa moja
Kiukweli kabisa watu wengi wamejikuta njia panda kuhusu kutoboa kimaisha, ila kwa asilimia kubwa hivi vitu vitatu ndio chanzo kikubwa.
1. Kumtegemea mwanasiasa.
Hakuna kitu kibaya kama kumchagua mwanasiasa huku ukitegemea ipo siku atakutoa kimaisha, hilo sahau kabisa wewe mchague mtu bora kisha pambana na maisha na usahau kabisa kama ulipiga kura. hapa itakusaidia hata kisaikolojia.
Mwanasiasa mwenyewe anakutegemea wewe umpe mtaji.
2. Waganga/wachawi
Janga lingine ni hili pia watu wengi huwategemea hawa watu kwa kujua watatoboa ila mwisho wa siku hola hakuna maisha ya muujiza wewe, tafta hela kwa juhudi zako. hata kama utategemea ila usiweke 100%
3. Dini
Huu ni Moja kati ya ukweli mchungu kabisa, usijiloge kwamba kuna siku utaombewa upate muujiza wa kimaisha utaishia kuwachukia watu, hapa wahanga wengi ni wanawake. Kumekua na watoa Ibada wengi ambao wajifanya ni watoa miujiza kwa kutoza pesa,, ndugu utaibiwa mpaka uote kipara, wapo kabisa ambao wanakuambia ukitoa 300k basi muujiza wako utaupata ndani ya siku chache tu, ukishampa alafu ukafanyiwa hiyo Ibada siku ukirudi kuuliza kwamba mbn hakuna matokeo atakuambia kwamba Mungu hachelewi wala hawahi.
Mtu pekee wa kubadilisha maisha yako utamuona ukiweka kioo mbele yako tu, wengine ni madaraja ya kukusogeza tu ila sio kutoboa.
Tujitumeni kwa akili na nguvu zetu matokeo tutayapata.
Kiukweli kabisa watu wengi wamejikuta njia panda kuhusu kutoboa kimaisha, ila kwa asilimia kubwa hivi vitu vitatu ndio chanzo kikubwa.
1. Kumtegemea mwanasiasa.
Hakuna kitu kibaya kama kumchagua mwanasiasa huku ukitegemea ipo siku atakutoa kimaisha, hilo sahau kabisa wewe mchague mtu bora kisha pambana na maisha na usahau kabisa kama ulipiga kura. hapa itakusaidia hata kisaikolojia.
Mwanasiasa mwenyewe anakutegemea wewe umpe mtaji.
2. Waganga/wachawi
Janga lingine ni hili pia watu wengi huwategemea hawa watu kwa kujua watatoboa ila mwisho wa siku hola hakuna maisha ya muujiza wewe, tafta hela kwa juhudi zako. hata kama utategemea ila usiweke 100%
3. Dini
Huu ni Moja kati ya ukweli mchungu kabisa, usijiloge kwamba kuna siku utaombewa upate muujiza wa kimaisha utaishia kuwachukia watu, hapa wahanga wengi ni wanawake. Kumekua na watoa Ibada wengi ambao wajifanya ni watoa miujiza kwa kutoza pesa,, ndugu utaibiwa mpaka uote kipara, wapo kabisa ambao wanakuambia ukitoa 300k basi muujiza wako utaupata ndani ya siku chache tu, ukishampa alafu ukafanyiwa hiyo Ibada siku ukirudi kuuliza kwamba mbn hakuna matokeo atakuambia kwamba Mungu hachelewi wala hawahi.
Mtu pekee wa kubadilisha maisha yako utamuona ukiweka kioo mbele yako tu, wengine ni madaraja ya kukusogeza tu ila sio kutoboa.
Tujitumeni kwa akili na nguvu zetu matokeo tutayapata.