KikulachoChako
JF-Expert Member
- Jul 21, 2013
- 19,759
- 39,493
Moja ya madhara ya zinaa ni pamoja na umasikini na laana.......
Mimi kwa uzoefu wangu na kwa kesi nyingi nilizopokea za mambo haya ya ndoa ni kuwa msingi mkubwa wa kukosekana kwa amani na utulivu kwenye ndoa kunatokana na mambo makubwa yafuatayo......
1) Mawasiliano duni baina ya wanandoa...
Asilimia tisini ya matatizo ya kwenye chumba Cha wanandoa yanatatuliwa kwa kuzungumza.....kama watu mlikutana mkazungumza mkaelewana mpaka mkafunga ndoa kwanini iwe vigumu kuyaongelea mambo yenu ya ndani na kuyamaliza pasi na kudhalilishana.......???
2)Kiburi na dharau ndani ya ndoa.....
Mwanandoa mmoja anapohisi hathaminiwi na kusikilizwa na mwenzi wake ambaye ndio mtu wake wa karibu hujiona hana maana na hana thamani kwenye dunia hii...... lakini kwa kuwa hilo ni jambo la msingi maishani mwake lazima atatafuta comfort nje ya ndoa na hapo ndipo huzaliwa michepuko.........
3)Kukosea kuoa....
Wakati mwingine watu hufanya maamuzi makubwa ya ndoa kutokana na misukumo fulani kulingana na nyakati au mazingira huskia.....ule msukumo na mazingira yakiisha hujikuta hana furaha kwenye muunganiko huo na kujiona mpweke....... muendelezo wa hali hiyo hupelekea maugomvi na kukosekana kwa amani ndani ya ndoa na mwisho wa siku watu wanaamua kuishi bora liende........
NB;
Ndoa ni taasisi iliyojaa changamoto na purukushani za kila aina chagua mtu sahihi mtakayeweza kuvumilia naye changamoto hizo kwa upendo na amani.........
Mimi kwa uzoefu wangu na kwa kesi nyingi nilizopokea za mambo haya ya ndoa ni kuwa msingi mkubwa wa kukosekana kwa amani na utulivu kwenye ndoa kunatokana na mambo makubwa yafuatayo......
1) Mawasiliano duni baina ya wanandoa...
Asilimia tisini ya matatizo ya kwenye chumba Cha wanandoa yanatatuliwa kwa kuzungumza.....kama watu mlikutana mkazungumza mkaelewana mpaka mkafunga ndoa kwanini iwe vigumu kuyaongelea mambo yenu ya ndani na kuyamaliza pasi na kudhalilishana.......???
2)Kiburi na dharau ndani ya ndoa.....
Mwanandoa mmoja anapohisi hathaminiwi na kusikilizwa na mwenzi wake ambaye ndio mtu wake wa karibu hujiona hana maana na hana thamani kwenye dunia hii...... lakini kwa kuwa hilo ni jambo la msingi maishani mwake lazima atatafuta comfort nje ya ndoa na hapo ndipo huzaliwa michepuko.........
3)Kukosea kuoa....
Wakati mwingine watu hufanya maamuzi makubwa ya ndoa kutokana na misukumo fulani kulingana na nyakati au mazingira huskia.....ule msukumo na mazingira yakiisha hujikuta hana furaha kwenye muunganiko huo na kujiona mpweke....... muendelezo wa hali hiyo hupelekea maugomvi na kukosekana kwa amani ndani ya ndoa na mwisho wa siku watu wanaamua kuishi bora liende........
NB;
Ndoa ni taasisi iliyojaa changamoto na purukushani za kila aina chagua mtu sahihi mtakayeweza kuvumilia naye changamoto hizo kwa upendo na amani.........