TUNTEMEKE
JF-Expert Member
- Jun 15, 2009
- 4,587
- 579
CHAMA cha wananchi (CUF) sasa kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kuonyesha kwa vitendo kupinga kauli ya kichochezi za uvunjaji wa amani zinazotolewa na chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA ) na kudai kuwa Chadema si chama chenye nia njema a amani ya Tanzania.
CUF imesema kuwa Rais Kikwete Kikwete ameshindwa kuwachukulia hatua dhidi ya Chadema pamoja na kuapa kuilinda na kuitetea katiba ya Tanzania ila ameiacha katiba hiyo ikiendelea kuvurugwa kwa kauli za kichochezi dhidi ya serikali yake.
Kauli hiyo imetolewa na mjumbe wa baraza kuu la CUF Taifa Hamad Rashid ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Wawi na kiongozi wa kambi ya wabunge wa CUF bungeni ,kuwa Chadema wasitumia shida za watanzania kwa ajili ya kufanikisha matakwa yao ya kuchochea vurugu na kulifanya Taifa la Tanzania kuwa Misri na nchi nzingine.
Alisema kuwa hakuna mtanzania ambaye anapendezwa na ugumu wa maisha yaliyopo sasa chini ya uongozi wa chama cha mapinduzi (CCM) chini ya Rais Kikwete ila hakuna mtanzania ambaye yupo tayari kuona amani inapotea na watanzania wakiuana kwa vita kutokana na kauli za uchochezi zinazofanywa na Chadema.
Alisema kuwa vyombo vya dola vya Tanzania vimeendelea kunyamaza kimya na kuchelewa kuchukua hatua ya kulinda amani ya Taifa hili na kuacha Chadema kuendelea kutoa kauli za kichochezi dhidi ya serikali huku vikitambua wazi kuwa kauli hiyo zinakwenda kinyume na katiba ya nchi yetu .
Hatuna imani na katiba ya Tanzania ila hatupo tayari kuhamasisha wananchi kufanya vurugu ili kuiondoa serikali madarakani kama wanavyo fanya wenzetu Chadema .sisi tunatambua njia pekee ya kuiondoa CCM ni kusubiri uchaguzi mkuu mwaka 2015 na sio vinginevyo..tunasema CUF hatuungi mkono hata kidogo uchochezi unaofanywa na Chadema dhidi ya serikali yetu wananchi mkiano chama chochote cha siasa hakiheshimu maamuzi ya wananchi chama hicho hakifaa kupewa hata kuongoza kundi la watu kumi
CUF imesema kuwa Rais Kikwete Kikwete ameshindwa kuwachukulia hatua dhidi ya Chadema pamoja na kuapa kuilinda na kuitetea katiba ya Tanzania ila ameiacha katiba hiyo ikiendelea kuvurugwa kwa kauli za kichochezi dhidi ya serikali yake.
Kauli hiyo imetolewa na mjumbe wa baraza kuu la CUF Taifa Hamad Rashid ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Wawi na kiongozi wa kambi ya wabunge wa CUF bungeni ,kuwa Chadema wasitumia shida za watanzania kwa ajili ya kufanikisha matakwa yao ya kuchochea vurugu na kulifanya Taifa la Tanzania kuwa Misri na nchi nzingine.
Alisema kuwa hakuna mtanzania ambaye anapendezwa na ugumu wa maisha yaliyopo sasa chini ya uongozi wa chama cha mapinduzi (CCM) chini ya Rais Kikwete ila hakuna mtanzania ambaye yupo tayari kuona amani inapotea na watanzania wakiuana kwa vita kutokana na kauli za uchochezi zinazofanywa na Chadema.
Alisema kuwa vyombo vya dola vya Tanzania vimeendelea kunyamaza kimya na kuchelewa kuchukua hatua ya kulinda amani ya Taifa hili na kuacha Chadema kuendelea kutoa kauli za kichochezi dhidi ya serikali huku vikitambua wazi kuwa kauli hiyo zinakwenda kinyume na katiba ya nchi yetu .
Hatuna imani na katiba ya Tanzania ila hatupo tayari kuhamasisha wananchi kufanya vurugu ili kuiondoa serikali madarakani kama wanavyo fanya wenzetu Chadema .sisi tunatambua njia pekee ya kuiondoa CCM ni kusubiri uchaguzi mkuu mwaka 2015 na sio vinginevyo..tunasema CUF hatuungi mkono hata kidogo uchochezi unaofanywa na Chadema dhidi ya serikali yetu wananchi mkiano chama chochote cha siasa hakiheshimu maamuzi ya wananchi chama hicho hakifaa kupewa hata kuongoza kundi la watu kumi