Ukishangaa ya Trump utayaona ya Vladimir Putin

Mwakamajoka

Senior Member
Nov 21, 2017
170
149
Kabla hatujasahau tukumbushane kitu muhimu ambacho kimepelekea au kunishawishi kuandika uzi huu. Katika ulimwengu huu wa sasa na kwa mda mrefu Marekani ndiye taifa kubwa na lenye nguvu katika nyanja mbali mbali kwa mfano kiuchumi, kisiasa na kijeshi. Marekani pia amekuwa mstari wa mbele kama Kiranja Mkuu wa Dunia kwa kuwawekea vikwazo vya kibihashara mataifa mbali mbali akiwemo Urusi. Vikwazo hivi amevifanya kupitia nguvu yake na ushawishi wake alionao ndani ya Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya.

TUENDELEE NA MADA KUU :

Urusi imesafirisha gesi (Liquefied Natural Gas) kwenda Marekani. Sababu kubwa iliyopelekea kufanyika kwa mpango huo ni kupanda kwa bei ya gesi katika maeneo ya mwamboa wa pwani ya Mashariki ya Marekani.

Meli inayomilikiwa na kampuni ya nishati (Engie) kutoka Ufaransa imepata deal la kusafirisha gesi (Liquefied Natural Gas) kutoka Uingereza mpaka pwani ya mashariki kwenye kituo cha gesi cha Everett karibu na Boston Marekani.

Gesi inayosafirishwa kwenda EVERETT-BOSTON-USA inatoka Urusi kwenye kiwanda cha gesi(Liquefied Natural Gas) kinachofahamika kwa Jina la YAMAL LNG.

Meli kubwa inayofanya kazi ya kusafirisha gesi (Liquefied Natural Gas) kutoka bandari ya Isle-Grain-British kwenda kituo cha gesi cha Marekani kinachopatikana Everett karibu na Boston itafika kwenye kituo cha Marekani tarehe 22/1/2018.

Mpango huu umeitikia mfumko wa bei ya gesi usio wa kawaida unaofikia dola za kimarekani 6,300/= per thousand cubic metres katika pwani ya mashariki ya Marekani.

Vikwazo vya Marekani dhidi ya sekta ya nishati ya Urusi haijazuia moja kwa moja usambazaji na uuzwaji wa gesi kutoka Moscow mpaka Marekani. Ijapokuwa, Washington imeendeleza msimamo wake wa kumzuia URUSI kuwa Mfalme wa biashara ya gesi katika bara la ULAYA.

Meli inayosafirisha mzigo imepokea mzigo wa gesi(Liquefied Natural Gas) katika bandari ya Isle-Grain-British baada tu ya meli ya Urusi (Christophe De Margerie) kufika Uingereza mwezi wa 12/2017 na mzigo wa gesi kwa mara ya kwanza.

Meli ya Urusi iliyosafirisha mzigo wa gesi mpaka Uingereza ilipewa Jina la Christophe De Margerie baada ya aliyekuwa CEO wa kampuni ya TOTAL Bwana Christophe De Margerie kuaga dunia/ku-rest in peace, baada ya ajali mbaya ya ndege kutokea huko Urusi. Meli hiyo inauwezo wa kubeba shehena ya liquefied natural gas kiasi cha 173,000 cubic metres. Urusi ili kufanikisha malengo yake mengine ya badae anampango wa kutengeneza meli zingine kubwa 15 zenye ukubwa kama Meli ya Christophe De Margerie.

Source: Kommersant daily report
 
Mbona hamna la kushangaza hapa? ni sawa na NK wanavyofanya biashara Uchina kupitia visiwa vya Macau na over seas companies etc..sasa la kustaajabisha ni ?! au labda ndio sielewi kiswahili?
Asante sana Mheshimiwa kwa kuchangia.

Cha kushangaza hapa ndugu yangu ni kwamba, Three Supper Powers on Earth United Kingdom, USA and France ndio mabingwa wa kuweka na kusimamia vikwazo vya biashara dhidi ya Urusi lakini hi leo wamekubali kufanya biashara ya gesi na Urusi.
1: Marekani kuuziwa gesi na Urusi (Amewekewa vikwazo na Umoja wa mataifa na umoja wa Ulaya)
2: Uingereza kuwa njia ya kusafirisha gesi hiyo toka Urusi, ambae ni kisiki ndani ya Umoja wa mataifa tena ni rafiki na ndugu wa karibu kabisa wa Marekani wote kwa pamoja walipigia debe vikwazo dhidi ya Urusi.
3: Meli inayomilikiwa na kampuni ya Ufaransa kusafirisha shehena hiyo ya gesi mpaka Marekani.
4: Hapo hapo Washington inasema inaendelea na mpango wa kumdhibiti Urusi kuwa muuzaji mkubwa wa gesi katika bara la Ulaya.

Kwa North Korea kufanya anachokifanya mi naona kawaida sana kwasababu mafuta yanatoka kwa usiri kwa rafiki zake China, Urusi na mataifa mengine ambao ni watukutu kama yeye.

Ishu hapa ni kwamba adui kufanya biashara na adui.
 
Kwa sasa Tanzania ndio inaongoza kati ya Nchi inayo chimba Gesi na bado haiwanufaishi Wananchi wake ipasavyo...
 
Hivi unadhani gesi ni sawa na mahindi kwamba mkulima anafaidi msimi was kwanza?
Nimenena hili nikiwa tayari nina utafiti, yawezekana pia tuko katika msimu wa kwanza ili rasilimali kama Dhahabu na Utalii viweze kutubadirishia Maisha...!
 
Asante sana Mheshimiwa kwa kuchangia.

Cha kushangaza hapa ndugu yangu ni kwamba, Three Supper Powers on Earth United Kingdom, USA and France ndio mabingwa wa kuweka na kusimamia vikwazo vya biashara dhidi ya Urusi lakini hi leo wamekubali kufanya biashara ya gesi na Urusi.
1: Marekani kuuziwa gesi na Urusi (Amewekewa vikwazo na Umoja wa mataifa na umoja wa Ulaya)
2: Uingereza kuwa njia ya kusafirisha gesi hiyo toka Urusi, ambae ni kisiki ndani ya Umoja wa mataifa tena ni rafiki na ndugu wa karibu kabisa wa Marekani wote kwa pamoja walipigia debe vikwazo dhidi ya Urusi.
3: Meli inayomilikiwa na kampuni ya Ufaransa kusafirisha shehena hiyo ya gesi mpaka Marekani.
4: Hapo hapo Washington inasema inaendelea na mpango wa kumdhibiti Urusi kuwa muuzaji mkubwa wa gesi katika bara la Ulaya.

Kwa North Korea kufanya anachokifanya mi naona kawaida sana kwasababu mafuta yanatoka kwa usiri kwa rafiki zake China, Urusi na mataifa mengine ambao ni watukutu kama yeye.

Ishu hapa ni kwamba adui kufanya biashara na adui.
Wewe unafahamu hivyo vikwazo vililenga sekta gani na kwa ukubwa gani?..Maana unweza kuweka vikwazo kwenye gas kwa kiwango fulani na kiasi ukaachia.Huwezi ku block 100%....Unashangaa kwa sababu hujui terms kwenye ile package ya vikwazo.Hata N.K siyo kila kitu amezuiwa kuuza,ni vitu fulani kwa kiasi fulani.
 
Nani akubadilishie maisha ww?Hata iuzwe nchi, hutapata hata senti tano. Kwan hao ambao maisha yao yamebadilika iliuzwa ges gani? Tena kwa utawala huu, sahau maana pesa zinakusanywa toka kwa wananchi sio zinaenda! Kodi,ushuru, rushwa,penalty na fines unatoa na unapewa risiti.Gharama za matibabu hospitali za serikali kwa sasa hazina utofauti na binafsi kwa vipimo na wameweka kampuni kwaajiri ya kukusanya. Af mtu anawaza kubadilishiwiwa maisha! Ulimwengu wa kibepali ni kupambana kivyako hata ukienda ishi uingereza usipopigana utapaona pagumu tu.
Nimenena hili nikiwa tayari nina utafiti, yawezekana pia tuko katika msimu wa kwanza ili rasilimali kama Dhahabu na Utalii viweze kutubadirishia Maisha...!
 
Back
Top Bottom