Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Je umeshawahi kumtazama mkeo au rafiki yako wa kike katika namna yake ya kuvaa? Lakini je, hata wanawake unaowajua ambao unakutana nao kila siku, iwe kazini, mtaani au popote, umeshawahi kuwatazama na kujiuliza kuhusu uvaaji wao? Kama umekuwa ukiwatazama, labda umekuwa ukiwatazama kupendeza au kuchusha kwao tu, na siyo jambo lingine. Lakini kuanzia sasa itabidi uwe unawatazama kwa sababu na namna tofauti kabisa.
Kwa nini?
Ni kwa sababu watafiti wamebaini sasa kwamba, mwanamke anapokuwa kwenye siku zake za hatari, yaani kwenye zile siku ambazo anaweza kupata ujauzito kama atashiriki tendo, huwa anavaa tofauti na siku nyingine za kawaida. Utafiti mkubwa umefanywa na wataalamu mbalimbali, umeonesha kwamba, mwanamke hujikuta akivaa vizuri zaidi wakati ambapo yuko kwenye siku za hatari. Siyo kuvaa vizuri, bali pia huvaa nguo zenye kuonesha zaidi maungo au ngozi yake. Kama hiyo haitoshi, huvaa pia marembo au vito kama dhahabu au makochokocho mengine (Lebasi za ulimbwende) tofauti na siku nyingine. Ni kwamba hujipamba zaidi. Uvaaji huo unaelezwa kwamba, unatokana na maumbile, na mwanamke huwa hajui ni kwa nini anavaa vizuri au kujipamba zaidi wakati fulani kuliko wakati mwingine.
Pamoja na kwamba kuna sababu kadhaa za kujipamba, inapofika kipindi hiki cha hatari uvaaji wa mwanamke unabadilika bila mwenyewe kujua. Huvaa vizuri ikiwa ni nia ya kutoa taarifa kwa mwanaume kwamba, yuko tayari au kumvuta mwanaume, kimaumbile ikiwa ni lengo la kupata mtoto. Hii ni kawaida ya maumbile ambapo mnyama wa kike anapokuwa kwenye nyakati za kutaka kupandwa ili kuzaa huonesha dalili fulani. Kuna wanyama ambao hutoa harufu kali ambayo humfanya dume kujua kwamba mnyama huyo wa kike anataka kupandwa. Wanyama wengine hubadilika rangi ya ngozi.
Kwa binadamu anaonekana kuvaa kwa namna ya kuvuta ndiyo njia ambayo mwanamke anamjulisha mwanaume kwamba, yuko kwenye kipindi ambacho anaweza kupata ujauzito. Bila shaka, siku za nyuma kabisa kabla ya kile kinachoitwa ustaarabu wa kujua zuri na baya, kabla binadamu hajaanza kuingia katika ustaarabu wa kutongoza na kila mtu kuwa na wake, mwanamke kujipamba ilikuwa ndiyo njia ya kuwashawishi wanaume kufanya naye mapenzi ili kupata ujauzito.
Kama nilivyosema, hii ni kazi ya maumbile, kwa hiyo mwanamke anakuwa hajui ni kwa nini anachagua nguo fulani, au kujikuta akitamani kujipamba katika siku fulani. Kwa mfano, imebainika kwamba, mwanamke ambaye huwa anapenda kuvaa sketi fupi au wakati mwingine suruali, anapokuwa kwenye siku zake za hatari ni lazima atavaa sketi fupi badala ya suruali. Kama nilivyosema kuna sababu nyingine ni kwa nini mwanamke anavaa kwa njia fulani. Kwa mfano kama anataka kuonesha maungo yake kwa kuvaa nguo fupi au za kubana, akiwa kwenye siku zake za hatari atajikuta akiongeza na mapambo mengine au pengine kuvaa nguo zenye kuonesha maumbile yake zaidi.
Hii ni kwa binadamu wote, siyo kwa waafrika peke yake kwani ni suala la kimaumbile. Hata wazungu ambao huvaa nguo za kuonesha maungo bila kujali, linapokuja suala la siku za hatari za mwanamke, uvaaji wao huwa tofauti. Ni lazima wataongeza chumvi kwenye uvaaji wenye kuonesha maungo au kubana na pengine kuwa na mapambo mengi maungoni. Jarida la Hormones Behaviour linaonesha kuhusu utafiti ambao ulifanywa kwa wanafuzni wa kike wa vyuo vikuu. Linaripoti kwamba, hata wale wasichana ambao uvaaji wao ni wa hovyohovyo, wakati wa siku zao za hatari walionekana kuvaa kwa kuvutia na kujipamba pia. Mtafiti Martie Haselton wa chuo kikuu cha Califonia Los Angeles nchini Marekani na timu yake ambao wamefanya utafiti kuhusu jambo hili, amesema, hakuna mtu anayeweza kujua kwamba, anavaa kwa namna fulani kwa sababau yuko kwenye siku zake za hatati, hivyo anaweza kudhani anavaa kwa namna fulani kwa sababu nyingine au kwa mazoea.
Ndio maana unaweza kuona mwanamke anaazima nguo fulani kwa mwenzake, mkufu au kitu kingine kinachoweza kumfanya apendeze zaidi, wakati wala haendi mahali ambapo ingekuwa ni lazima abadili. Kuna kitu kinamsukuma kuvaa tofauti kidogo. Kuna namna nyingi ambapo mwanaume anaweza kujua kwamba, mkewe au mwanamke mwingine yuko kwenye siku zake za hatari. Kuvaa kwa namna ambayo inaonesha kuwa inalenga kuvuta zaidi wanaume ni moja ambayo ni kubwa. Haina maana pia kwamba, mwananamke aliye kwenye siku zake za hatari, ni lazima avae kwa njia yenye kuamsha hisia za mwanaume, hapana. Bali atavaa kwa njia yenye kuonesha zaidi ngozi yake na pia kuwa na mapambo ya ziada.Hivyo mtu asije akadhani kila mwanamke anayevaa kwa njia ya kumtia mwanaume ushawishi yuko kwenye kipindi chake cha hatari.
Kwa nini?
Ni kwa sababu watafiti wamebaini sasa kwamba, mwanamke anapokuwa kwenye siku zake za hatari, yaani kwenye zile siku ambazo anaweza kupata ujauzito kama atashiriki tendo, huwa anavaa tofauti na siku nyingine za kawaida. Utafiti mkubwa umefanywa na wataalamu mbalimbali, umeonesha kwamba, mwanamke hujikuta akivaa vizuri zaidi wakati ambapo yuko kwenye siku za hatari. Siyo kuvaa vizuri, bali pia huvaa nguo zenye kuonesha zaidi maungo au ngozi yake. Kama hiyo haitoshi, huvaa pia marembo au vito kama dhahabu au makochokocho mengine (Lebasi za ulimbwende) tofauti na siku nyingine. Ni kwamba hujipamba zaidi. Uvaaji huo unaelezwa kwamba, unatokana na maumbile, na mwanamke huwa hajui ni kwa nini anavaa vizuri au kujipamba zaidi wakati fulani kuliko wakati mwingine.
Pamoja na kwamba kuna sababu kadhaa za kujipamba, inapofika kipindi hiki cha hatari uvaaji wa mwanamke unabadilika bila mwenyewe kujua. Huvaa vizuri ikiwa ni nia ya kutoa taarifa kwa mwanaume kwamba, yuko tayari au kumvuta mwanaume, kimaumbile ikiwa ni lengo la kupata mtoto. Hii ni kawaida ya maumbile ambapo mnyama wa kike anapokuwa kwenye nyakati za kutaka kupandwa ili kuzaa huonesha dalili fulani. Kuna wanyama ambao hutoa harufu kali ambayo humfanya dume kujua kwamba mnyama huyo wa kike anataka kupandwa. Wanyama wengine hubadilika rangi ya ngozi.
Kwa binadamu anaonekana kuvaa kwa namna ya kuvuta ndiyo njia ambayo mwanamke anamjulisha mwanaume kwamba, yuko kwenye kipindi ambacho anaweza kupata ujauzito. Bila shaka, siku za nyuma kabisa kabla ya kile kinachoitwa ustaarabu wa kujua zuri na baya, kabla binadamu hajaanza kuingia katika ustaarabu wa kutongoza na kila mtu kuwa na wake, mwanamke kujipamba ilikuwa ndiyo njia ya kuwashawishi wanaume kufanya naye mapenzi ili kupata ujauzito.
Kama nilivyosema, hii ni kazi ya maumbile, kwa hiyo mwanamke anakuwa hajui ni kwa nini anachagua nguo fulani, au kujikuta akitamani kujipamba katika siku fulani. Kwa mfano, imebainika kwamba, mwanamke ambaye huwa anapenda kuvaa sketi fupi au wakati mwingine suruali, anapokuwa kwenye siku zake za hatari ni lazima atavaa sketi fupi badala ya suruali. Kama nilivyosema kuna sababu nyingine ni kwa nini mwanamke anavaa kwa njia fulani. Kwa mfano kama anataka kuonesha maungo yake kwa kuvaa nguo fupi au za kubana, akiwa kwenye siku zake za hatari atajikuta akiongeza na mapambo mengine au pengine kuvaa nguo zenye kuonesha maumbile yake zaidi.
Hii ni kwa binadamu wote, siyo kwa waafrika peke yake kwani ni suala la kimaumbile. Hata wazungu ambao huvaa nguo za kuonesha maungo bila kujali, linapokuja suala la siku za hatari za mwanamke, uvaaji wao huwa tofauti. Ni lazima wataongeza chumvi kwenye uvaaji wenye kuonesha maungo au kubana na pengine kuwa na mapambo mengi maungoni. Jarida la Hormones Behaviour linaonesha kuhusu utafiti ambao ulifanywa kwa wanafuzni wa kike wa vyuo vikuu. Linaripoti kwamba, hata wale wasichana ambao uvaaji wao ni wa hovyohovyo, wakati wa siku zao za hatari walionekana kuvaa kwa kuvutia na kujipamba pia. Mtafiti Martie Haselton wa chuo kikuu cha Califonia Los Angeles nchini Marekani na timu yake ambao wamefanya utafiti kuhusu jambo hili, amesema, hakuna mtu anayeweza kujua kwamba, anavaa kwa namna fulani kwa sababau yuko kwenye siku zake za hatati, hivyo anaweza kudhani anavaa kwa namna fulani kwa sababu nyingine au kwa mazoea.
Ndio maana unaweza kuona mwanamke anaazima nguo fulani kwa mwenzake, mkufu au kitu kingine kinachoweza kumfanya apendeze zaidi, wakati wala haendi mahali ambapo ingekuwa ni lazima abadili. Kuna kitu kinamsukuma kuvaa tofauti kidogo. Kuna namna nyingi ambapo mwanaume anaweza kujua kwamba, mkewe au mwanamke mwingine yuko kwenye siku zake za hatari. Kuvaa kwa namna ambayo inaonesha kuwa inalenga kuvuta zaidi wanaume ni moja ambayo ni kubwa. Haina maana pia kwamba, mwananamke aliye kwenye siku zake za hatari, ni lazima avae kwa njia yenye kuamsha hisia za mwanaume, hapana. Bali atavaa kwa njia yenye kuonesha zaidi ngozi yake na pia kuwa na mapambo ya ziada.Hivyo mtu asije akadhani kila mwanamke anayevaa kwa njia ya kumtia mwanaume ushawishi yuko kwenye kipindi chake cha hatari.