Ukiona mifuko ya Watu sasa imetuna usishangae sana bali jua ya kwamba...

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,516
108,791
Kutokana na Uhaba mkubwa wa Sukari iliyoadimika kwa Makusudi Watanzania sasa wamepata njia mbadala ya kunywa chai kwa kutumia aina nyingine ya Kichocheo kitamu.

Hali hii imepelekea sasa Watanzania wengi KUWEKEZA katika kununua Pipi nyingi na ukitaka kuligungua hili kila upandapo Daladala angalia ABIRIA hasa akina Baba walivyojaza Pipi katika mifuko yao ya Shati na Suruali ambapo wakifika Makazini kwao au Majumbani mwao huzimwanga hizo Pipi na kuzitumia katika kunywea chai.

Kinachofanyika sasa ni kwamba mzazi anahakikisha tu ananunua Pipi za Tsh 3,000/ kisha kila wanapokuwa wanakunywa Chai mwanafamilia anarushiwa tu Pipi moja na anaidumbukiza katika Kikombe cha Chai na kunywa Chai siku inaenda.

Akizungumza na mwandishi wa taarifa hii Mfanyakazi mmoja wa Kampuni ya Pipi aitwae Mr. Popoma Aliyetukuka alisema kuwa hata wao wanashangaa ni kwanini kwa sasa pipi zao zinauzika kupita kiasi na zinagombaniwa. " Mheshimiwa mwandishi wa Habari hivi unavyoniona hapa tumetoka kumaliza stoke yetu yote ya Sukari hapa Kiwandani kwani Watanzania wengi sasa wanatumia pipi kama kunywea chai kama njia mbadala ya kuondokana na uhaba wa Sukari majumbani mwao na kiukweli tumepata super profit kwa wiki hii na tunaomba Sukari iendelee kuadimika hivi hivi " alisema Bwana Popoma.

ANGALIZO:

Enyi Vibaka mnaotuibiaga kila mara na kila siku kaeni mkijua kuwa kwa sasa mnapoona Mifuko yetu imetuna msije mkadhani labda ni Simu au Hela bali jueni ya kwamba mkitupiga " ndole " tu mnaibuka na Pipi. Mtaisoma namba mwaka huu!

Ama hakika KUFA KUFAANA.
 
Kutokana na Uhaba mkubwa wa Sukari iliyoadimika kwa Makusudi Watanzania sasa wamepata njia mbadala ya kunywa chai kwa kutumia aina nyingine ya Kichocheo kitamu.

Hali hii imepelekea sasa Watanzania wengi KUWEKEZA katika kununua Pipi nyingi na ukitaka kuligungua hili kila upandapo Daladala angalia ABIRIA hasa akina Baba walivyojaza Pipi katika mifuko yao ya Shati na Suruali ambapo wakifika Makazini kwao au Majumbani mwao huzimwanga hizo Pipi na kuzitumia katika kunywea chai.

Kinachofanyika sasa ni kwamba mzazi anahakikisha tu ananunua Pipi za Tsh 3,000/ kisha kila wanapokuwa wanakunywa Chai mwanafamilia anarushiwa tu Pipi moja na anaidumbukiza katika Kikombe cha Chai na kunywa Chai siku inaenda.

Akizungumza na mwandishi wa taarifa hii Mfanyakazi mmoja wa Kampuni ya Pipi aitwae Mr. Popoma Aliyetukuka alisema kuwa hata wao wanashangaa ni kwanini kwa sasa pipi zao zinauzika kupita kiasi na zinagombaniwa. " Mheshimiwa mwandishi wa Habari hivi unavyoniona hapa tumetoka kumaliza stoke yetu yote ya Sukari hapa Kiwandani kwani Watanzania wengi sasa wanatumia pipi kama kunywea chai kama njia mbadala ya kuondokana na uhaba wa Sukari majumbani mwao na kiukweli tumepata super profit kwa wiki hii na tunaomba Sukari iendelee kuadimika hivi hivi " alisema Bwana Popoma.

ANGALIZO:

Enyi Vibaka mnaotuibiaga kila mara na kila siku kaeni mkijua kuwa kwa sasa mnapoona Mifuko yetu imetuna msije mkadhani labda ni Simu au Hela bali jueni ya kwamba mkitupiga " ndole " tu mnaibuka na Pipi. Mtaisoma namba mwaka huu!

Ama hakika KUFA KUFAANA.

Sahihisha mkuu
 
Gentamycine yani topic zako zimekaa kilumumba lumumba tu manake hazieleweki
 
Siyo lazima kila siku huanzishe mada

Na siyo lazima pia kila siku mimacho ikutumbuke kusoma threads zangu. Hata hivyo najua hadi umeusoma huu UZI wangu una Mahaba na Mimi. Safi sana je kuna jingine umelibakiza Mkuu? Halafu nilivyo na NYOTA ya JAHA huu UZI utaenda na kuchangamkiwa vile vile. Chochote nikianzichasho humu lazima kiwe na MASHIKO sasa anzisha Wewe UZI wako tuone kama utafika hata page 1.
 
Duuh, hii taarabu sasa! Kuna mdada mmoja nasikia wanamwita GIGY MONEY, wanasema eti yupo kutafuta kick Mitandaoni kwa kupost pic za utupu. Sasa naona kwa uandishi huu
na wewe upo kutafuta Kick Jf.
Na siyo lazima pia kila siku mimacho ikutumbuke kusoma threads zangu. Hata hivyo najua hadi umeusoma huu UZI wangu una Mahaba na Mimi. Safi sana je kuna jingine umelibakiza Mkuu? Halafu nilivyo na NYOTA ya JAHA huu UZI utaenda na kuchangamkiwa vile vile. Chochote nikianzichasho humu lazima kiwe na MASHIKO sasa anzisha Wewe UZI wako tuone kama utafika hata page 1.
 
Back
Top Bottom