jfmwaipopo
Member
- Nov 1, 2012
- 26
- 20
Ndugu wana jf ni ukweli usiopingika kuwa taifa la tanzania lipo katika hali mbaya takriinaban katika maeneo yote. Leo hii ukimuuliza hata mtoto wa darasa la kwanza atakuambia kuwa hali ya maisha si nzuri kwani wazaz wanashindwa kuwapatia mahitaji yao muhimu kutokana na ugumu wa maisha unaotokana na kupanda kwa gharama za vyakula na nauli kuongezeka, matababu ya kubahatisha, wanafunzi kufeli na kuhitimu bila ya kujua kusoma na kuandika, shida ya maji na mambo mengine mengi yanatofanana na hayo.
Tukiacha itikadi zetu za kichama na kuutanguliza utaifa mbele utajua mambo yote hayo yanatokana na kuwa na katiba mbovu inayoshindwa kumtetea mwananchi wa chini kabisa ili naye afurahie maziwa na asali zilizopo nchini mwake. Katika hotuba ya majumuisho ya waziri mkuu haoni umuhimu wa kulipatia kipa umbele swala hili zito la mchakato wa katiba mpya na kubeza kuwa upinzani unapiginia hili kwa kutazama 2015. Ukitafakari kwa kina kauli hii inathibitisha kuwa kumbe hata wao wanajua kuwa katiba iliyopo inapendelea upande mmoja wa chama cha siasa ndio maana badala ya kufikiri kwa mapana juu ya kuwa na katiba mpya kiongozi mwandamizi anawaza seheu moja tu ya uchaguzi 2015 na hivyo kutoona umuhimu wa kuupa kipaumbele mchakato wa katiba.
Hali inayoendelea sasa kwa anayefuatilia mchakato huu katiba mpya kwa kutanguliza uzalendo wa taifa lake atakubaliana na mimi kuwa mchakato umechakachuliwa kwani wajumbe waliochaguliwa na wananchi wamefanyiwa mchujo na viongozi kata WDC ambao vigezo walivyotumia hakuna anayejua na kuwaacha wananchi katika hali kubwa ya kukosa imani na mchakato unaendelea hivi sasa. Nilifikiri kuwa kwa kuwa katiba ya wananchi uteuzi wa mwisho ungefanywa na wanachi wenyewe kuliko ilivyo hivi sasa ambapo viongozi wachache wa WDC ambao zaid ya asilimia tisini ni kutoka ccm ndio wanaofnya mchujo na hivyo kufanya mchakato mzima kubakwa na chama kimoja cha siasa.
Hili ni swala ambalo pinda na wabunge wa ccm hawapaswi kulibeba kwa ushabiki. Kiongozi wa kambi ya upinzani kalileta kama kipa umbele kwa sasa lkn pinda anabeza na wabunge wengine waliokosa uzalendo wanashangalia .Kama tutalibeba taifa hili kiushabiki ktk masuala mazito hatutafika popote.
Profesa Baregu ambaye ni mjumbe wa tume ya katiba na ndiye mwakilishi pekee wa chadema kinachonishangaza ni ukimya wake na ushirikiano wake kwa chama kilichomteua. Wakati mkt na kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni akipambana na udhalimu huu profesa baregu yupo kimya kana kwamba haelewi kabisa kinachoendelea juu mchakato.Sasa nashindwa kuelewa ni kulewa nafasi hizi ndogo ndogo au anaona msimamo wa chama juu hili si sahihi.Kama kiongozi mahili tunayemwamini kwa uzoefu , umri na elimu yake atoe msimamo wake juu hiki kinachoendelea vinginevyo atajishushia sifa na heshima ailiyonayo kwa wananchi na chama chake.
Tukiacha itikadi zetu za kichama na kuutanguliza utaifa mbele utajua mambo yote hayo yanatokana na kuwa na katiba mbovu inayoshindwa kumtetea mwananchi wa chini kabisa ili naye afurahie maziwa na asali zilizopo nchini mwake. Katika hotuba ya majumuisho ya waziri mkuu haoni umuhimu wa kulipatia kipa umbele swala hili zito la mchakato wa katiba mpya na kubeza kuwa upinzani unapiginia hili kwa kutazama 2015. Ukitafakari kwa kina kauli hii inathibitisha kuwa kumbe hata wao wanajua kuwa katiba iliyopo inapendelea upande mmoja wa chama cha siasa ndio maana badala ya kufikiri kwa mapana juu ya kuwa na katiba mpya kiongozi mwandamizi anawaza seheu moja tu ya uchaguzi 2015 na hivyo kutoona umuhimu wa kuupa kipaumbele mchakato wa katiba.
Hali inayoendelea sasa kwa anayefuatilia mchakato huu katiba mpya kwa kutanguliza uzalendo wa taifa lake atakubaliana na mimi kuwa mchakato umechakachuliwa kwani wajumbe waliochaguliwa na wananchi wamefanyiwa mchujo na viongozi kata WDC ambao vigezo walivyotumia hakuna anayejua na kuwaacha wananchi katika hali kubwa ya kukosa imani na mchakato unaendelea hivi sasa. Nilifikiri kuwa kwa kuwa katiba ya wananchi uteuzi wa mwisho ungefanywa na wanachi wenyewe kuliko ilivyo hivi sasa ambapo viongozi wachache wa WDC ambao zaid ya asilimia tisini ni kutoka ccm ndio wanaofnya mchujo na hivyo kufanya mchakato mzima kubakwa na chama kimoja cha siasa.
Hili ni swala ambalo pinda na wabunge wa ccm hawapaswi kulibeba kwa ushabiki. Kiongozi wa kambi ya upinzani kalileta kama kipa umbele kwa sasa lkn pinda anabeza na wabunge wengine waliokosa uzalendo wanashangalia .Kama tutalibeba taifa hili kiushabiki ktk masuala mazito hatutafika popote.
Profesa Baregu ambaye ni mjumbe wa tume ya katiba na ndiye mwakilishi pekee wa chadema kinachonishangaza ni ukimya wake na ushirikiano wake kwa chama kilichomteua. Wakati mkt na kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni akipambana na udhalimu huu profesa baregu yupo kimya kana kwamba haelewi kabisa kinachoendelea juu mchakato.Sasa nashindwa kuelewa ni kulewa nafasi hizi ndogo ndogo au anaona msimamo wa chama juu hili si sahihi.Kama kiongozi mahili tunayemwamini kwa uzoefu , umri na elimu yake atoe msimamo wake juu hiki kinachoendelea vinginevyo atajishushia sifa na heshima ailiyonayo kwa wananchi na chama chake.