Kijakazi
Platinum Member
- Jun 26, 2007
- 10,436
- 17,768
Hilo ndilo tatizo kuuubwaaa sana.
Baregu alipendekezwa na CHADEMA kuwa mmoja wa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Hakwenda wala hakuteuliwa ili aweze kuwa msemaji wa CDM kwenye Tume au hakuteuliwa ili aweze kuipa taarifa CDM kwa kila kinachoendelea pale TUME. na kama angetoa taarifa ningemuona ni mjinga sana asiyejua maana ya kazi yake.
Hivi kumbe ndivyo mnavyotaka afanye atoe taarifa kuhusu kinachoendelea pale TUME?
Hayupo pale kuitumikia CDM kwa hiyo hapaswi kutoa taarifa zozote za Tume kwenda CDM. Baregu yupo pale kuwatumikia Watanzania na anayepaswa kutoa taarifa za Tume ni Mwenyekiti wa Tume na amekuwa akifanya hivyo.
Ulidhani Prof.Baregu aliupata u profesa kwa kuiba wake za watu alikaa shule. ana akili kuliko Mbowe, Slaa na wengine wa aina yao.
Ana linda heshma na haiba yake. Hivi leo akianza kutoa siri za Tume kesho CDM ikashika Nchi unadhani watamuamini tena? watajua huyu kazi yake ni kutoa siri.
Mzee Baregu hana Njaa kama wale vijana waliopo kwenye mitandao ya simu pale VODACOM, AIRTEL, TIGO, TTCL ZANTEL waliopandikizwa na CDM ili kuratibu kila aina ya ujumbe unatoka kwa Viongozi au watu maarufu au mashuhuri wa CCM au Seriikalini.
Nawaambia vijana hao maisha yao yapo hatarini nina uhakika kuwa siku CDM wakichukua Nchi watakaopigwa risasi za vichwa ni wao maana CDM itawahofia kuwa wanaweza kununuliwa tena na kutoa taarifa.
Nawasihi vijana hao waaache kabisa mtindo wa hatari.
Acha kuzunguka, mbona Gari la mamilioni hakulikataa, wakati alikuwa na uwezo huo?