UKIMWI huchukua muda gani kuonesha dalili?

mpiga era

JF-Expert Member
Aug 7, 2016
2,079
2,255
Habari wana JF, naomba kufahamu upungufu Wa kinga mwilini unachukua muda gani kuonekana? Punde baada ya kuupata? Na ipi ni dalili kuu kuliko zote? Na kwenye kipimo huonekana baada ya muda gani?

Nawasilisha.

PIA SOMA:
=========

MAONI YALIYOTOLEWA NA WADAU
Ukimwi una stage kuu tatu :

1) Acute HIV Infection / Primary stages.
Baada ya vijidudu kuingia mwili lazima utoe reaction ya mabadiliko.
Hii ni hatua ya kwanza kabisa kwa mtu aliyeambukizwa.
Inachukua week 2 hadi 6 kuonesha dalili kama, rushes, fever, headache, kuvimba tezi za shingo n.k
Dalili zinadumu kwa week 2 then zinapotea unakuwa kawaida.

2)Chronic HIV Infection.
Vijidudu vinaendelea kuzaliana ndani ya mwili kwa kiwango kidogo mno.
Mara nyingi hii hatua haina dalili za ugonjwa, wagonjwa huwa na afya njema kabisa, lakini anaambukiza kama kawaida.
Inachukua muda mrefu hata zaidi ya miaka 10 na kuendelea.

3)AIDS.
Vijidudu vinakuwa vimezaliana na kuongezeka kwa wingi mno,
Kinga ya mwili inakua imeshaharibika na kuelekea kumezwa na vijidudu kabisa.
CD4 zinashuka hadi chini ya 200cells/mm cubic.
Ndio hapa magonjwa nyemelezi yanakuandama, kama malaria, kuhara na mengine mengi.
Bila matibabu wala dawa ya aina yeyote mgonjwa anaweza survive kwa certainly miaka 3.

WINDOW PERIOD
Window period
ni muda kuanzia muda ulipopata infenctions hadi muda ambao vipimo vitaonesha umeathirika.
Ndani ya window period mgonjwa anaweza kuwa ameambukizwa lakini vipimo vikaonesha hajaathirika.
Muda huu huchukua zaidi ya week 4 hadi 12.

Kuhusu ipi ni dalili kubwa : Dalili zinatofautiana toka kwa mgonjwa mmoja hadi mwingine, unaweza kuwa na hii dalili mimi nisiwe nayo. Au ukawa na zote kwa pamoja.
Lakini mara nyingi dalili haiwi moja tu, zipo nyingi na sidhani kama ipo moja ambayo ni kubwa kuliko zingine.

Kwa maelezo zaidi nenda kituo cha afya.
========
Hapa kuna ishu mbili kuu...kuna kuambukizwa na kugundua kama umeambukizwa.

Njia pekee ya kujua kama umeambukizwa ni kupima...kitaalamu inaaminika kuwa vipimo vinaweza kuonyesha umeambukizwa baada ya wiki mbili hadi sita na kuendelea.

Kitaalamu huwezi kuanzishwa dawa mpaka CD4 zako zishuke kufikia kiwango fulani. Hivyo, kama umeambukizwa na hujapima na mwili wako una uwezo wa kuhimili VVU (yaani CD4 hazishuki), basi utaishi tu kama kawaida, na siku zote utajiamini kuwa huna vvu.

Na bado Wataalamu wanashinda maabara kutafuta ni nini haswa kinatokea kwa hao wenye uwezo wa kuwahimili vvu na wakaishi bila kuathirika maisha yao yote.

Kwa hiyo mtihani hapa ni kwamba huwezi kujua kama mwili wako unao huo uwezo mpaka upime, sasa ndio ujue kumbe unaishi na vvu na hawana uwezo wa kukuangamiza...sasa ni wangapi wenye uwezo wa kuhimili matokeo ya kuwa wanaishi na vvu? kwani unaweza kupima ndio ukaathirika kisaikolojia, na mawazo ndio yakaangamiza CD4 zako badala ya VVU.

Kuwa na VVU kwenyewe sio ugonjwa, hivyo ni ngumu kutarajia kuwepo kwa dalili za moja kwa moja zitakazofanana kutoka Mtu mmoja hadi mwingine...kinachotokea ni kwa kuwa kinga inapungua mwilini basi ugonjwa wowote unaweza kukushambulia na kukupelekesha.

Kwahiyo, ukiweka mambo kwenye mizani ni kuwa faida ya kupima ni kubwa kuliko kuishi tu kutegemea zali la mentali.
 
Inategemea na immune system yako wengine wanakaa mpaka miaka 10 baada ya maambukizi ndiyo wanajulikana. Dalili pia hutofautiana, wengine hupata magonjwa nyemelezi kinga inavyozidi kushuka kama TB na pneumonia ndipo wanapojulikana wana HIV pia.
Kwa suala la miaka 10 inanichukua vigumu sana kuamini. Samahani sana lakini hayo ni mawazo yangu yalio tokana na kukosa uthibitisho.
 
Inategemea na immune system yako wengine wanakaa mpaka miaka 10 baada ya maambukizi ndiyo wanajulikana. Dalili pia hutofautiana, wengine hupata magonjwa nyemelezi kinga inavyozidi kushuka kama TB na pneumonia ndipo wanapojulikana wana HIV pia.
Ni kweli kabisa wengine walijulikana toka miaka ya tisini hadi leo wapo wanadunda tu ila wanaopita halo wanakaa miaka miwili mitatu chali
 
Ukimwi una stage kuu tatu :

1) Acute HIV Infection / Primary stages.
Baada ya vijidudu kuingia mwili lazima utoe reaction ya mabadiliko.
Hii ni hatua ya kwanza kabisa kwa mtu aliyeambukizwa.
Inachukua week 2 hadi 6 kuonesha dalili kama, rushes, fever, headache, kuvimba tezi za shingo n.k
Dalili zinadumu kwa week 2 then zinapotea unakuwa kawaida.

2)Chronic HIV Infection.
Vijidudu vinaendelea kuzaliana ndani ya mwili kwa kiwango kidogo mno.
Mara nyingi hii hatua haina dalili za ugonjwa, wagonjwa huwa na afya njema kabisa, lakini anaambukiza kama kawaida.
Inachukua muda mrefu hata zaidi ya miaka 10 na kuendelea.

3)AIDS.
Vijidudu vinakuwa vimezaliana na kuongezeka kwa wingi mno,
Kinga ya mwili inakua imeshaharibika na kuelekea kumezwa na vijidudu kabisa.
CD4 zinashuka hadi chini ya 200cells/mm cubic.
Ndio hapa magonjwa nyemelezi yanakuandama, kama malaria, kuhara na mengine mengi.
Bila matibabu wala dawa ya aina yeyote mgonjwa anaweza survive kwa certainly miaka 3.

" WINDOW PERIOD ".

Window period ni muda kuanzia muda ulipopata infenctions hadi muda ambao vipimo vitaonesha umeathirika.
Ndani ya window period mgonjwa anaweza kuwa ameambukizwa lakini vipimo vikaonesha hajaathirika.
Muda huu huchukua zaidi ya week 4 hadi 12.

Kuhusu ipi ni dalili kubwa : Dalili zinatofautiana toka kwa mgonjwa mmoja hadi mwingine, unaweza kuwa na hii dalili mimi nisiwe nayo. Au ukawa na zote kwa pamoja.
Lakini mara nyingi dalili haiwi moja tu, zipo nyingi na sidhani kama ipo moja ambayo ni kubwa kuliko zingine.

Kwa maelezo zaidi nenda kituo cha afya.
 
Shida ni pale unapoambiwa CD4 zimeshuka na uanze kunywa dawa.ni kama hapa kwenye hizi dawa ndo penye shida maana ukianza tu kuzinywa hutakiwi kuacha, na ukiacha tu umekwenda na maji. hivi ukweli ni kwamba hata ukiwa na mafua makali bila hiyo HIV si CD4 zinashuka pia? ukiwa na Maralia imekushika si CD4 zinakua zimeshuka pia?sasa ukiwa na HIV unaambiwa pia CD4 zimeshuka kula ARVs na ukizianza tu ndo forever.maana yake ni kama hizi dawa ndo zinawamalizia watu.nawaza kwa SAUTI

JAH RASTAFARI MORNING AFRICA
 
Habari wana JF, naomba kufahamu upungufu Wa kinga mwilini unachukua muda gani kuonekana? Punde baada ya kuupata? Na IPI dalili kuu kuliko zote?

Nawasilisha

Sent using Jamii Forums mobile app

Window period ni siku 90 kitu huonekana kama kipo, but Huwa hutambuliwa na ELIZA TEST MACHINE ambayo hugundua mtu kama ameathirika na ukimwi kwa baada ya wiki tatu.
 
G'taxi,
Ukiwa HIV+ na CD4 zimeshuka unapoanza kunywa dawa zinaua vidudu vinavyotembea kwenye damu na isipokuwa vile vilivyojificha. Vidudu vinapokufa vinatoa nafasi kwa CD4 kutengenezwa na kuanza Tena kuulinda mwili. Uki acha kunywa dawa wale waliojificha wan arudi kwa ari mpya.

Tofauti na CD4 kupungua kwa maradhi mengine zinajitengeneza na hazina adui wa kuzishambulia
 
Ukiwa HIV+ na CD4 zimeshuka unapoanza kunywa dawa zinaua vidudu vinavyotembea kwenye damu na isipokuwa vile vilivyojificha. Vidudu vinapokufa vinatoa nafasi kwa CD4 kutengenezwa na kuanza Tena kuulinda mwili. Uko acha kunywa dawa wale waliojificha wan arudi kwa ari mpya.

Tofauti na CD4 kupungua kwa maradhi mengine zinajitengeneza na hazina adui wa kuzishambulia
Pamoja na yote na aksante kwa ufafanuzi lakini ugonjwa huu ni kama wa kimkakati tu. Na karibia hii biashara itakwisha watavumbua nyingine,nahisi muda c mrefu watasema dawa imepatikana au chanjo.it is like ndui

JAH RASTAFARI MORNING AFRICA
 
Kuna dawa Uingereza walianza kuijaribu tangu 2014, inamaliza wadudu wote hatavwale waliojificha hivyo mgonjwa jua cha kutumia ARVs. Hata hivyo hajathibifisha kuwa aliye acha kutumia dawa hawezi kumuambukiza mtu na pia kuna wagon kwa ambao immune system zao hazitakaa zirejee kama awali.
Ila si mchezo hii kitu imepukucha watu huku Africa.people wamekufa kama senene aisee!

JAH RASTAFARI MORNING AFRICA
 
Ninakumbuka miaka ya 90 uliathiri sana delta ya umma
Sasa hiyo miaka kutoka 1981 pale HIV ilikua inaondoa watu wakiwa na nusu kilo..mtu anakwisha na nywele zinasinyaa huwezi mtamani, tofauti na siku hz ndo mana nasema muda si muda hii kitu itapita.

Nina wasi wasi sana na watu weupe, watu ambao ni tishio kwao hawapendi wazaliane maana kuzaliana ni nguvu moja wapo ya kukua kiuchumi,ndo mana utasikia HIV,Maralia,vidonge vya uzazi wa mpango na mbinu nyingi tu za kuhakiki watu tuzidi kupungua badala ya kuongezeka.

Ni vile tu wametuwahi kutushikia akili lakini Africa ilipaswa kufunga mipaka yake na kua moja.tungepaswa kua na nchi kama 4 au 5 tu ktk Africa nzima na tukatae mipango yao mibovu juu yetu.

JAH RASTAFARI MORNING AFRICA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom