Ukifikiria sana kuhusu ndoa unaweza usione umuhimu wake

happy amos

JF-Expert Member
Feb 23, 2012
251
434
Leo nimekaa nimefikiria sana kuhusu ndoa
sikupata majibu. Yaani ukifikiria sana unaweza usione maana sana ya kuolewa.

Nakumbuka kuna kipindi dada angu mkubwa aliniambia mdogo wangu ndoa ni utumwa tu kwetu wanawake sasa namuelewa. Mfano mimi kabla sijaolewa nilikuwa na maisha yangu na ndoto zangu nyingi tu. Nilipanga mwaka huu usiishe sijajenga walau nyumba ya vyumba 3 na nikawa na juhudi za kufanikisha hilo.

Lakini tangu nimeolewa naona nakamilisha ndoto za mume wangu tu yaani malengo yake yeye aliyoyapanga kabla hatujawa pamoja naona ndio ninayo au tunayotimiza leo.

Mwenzangu nilimkuta kajipangia kutofanya chochote mpaka amalize kujenga kwao na kusomesha wadogo zake, tulivyoanza kuishi pamoja ndoto zangu za kutafuta kiwanja zikazimwa naambiwa subiri kwanza tumalize majukumu ya nyumbani.

Nikiwaza saaaaaana naona natimiza ndoto zake tu au za nyumbani kwao.

MTU unakosa jinsi sababu tuliumbwa tuwe chini yao na wao wawe juu yetu inabidi kuwa mdogo tu.
 
kabla ya ndoa hayo yote ya kuwekana sawa sawa... tatizo mnakuwa mnawaza harusi tu wadada na wakaka wanawaza papuchi tu... mnashindwa kuongea ya muhimu mapema..

ndoa nyingi sana zinavunjika now days.. hasa ambazo hazina kipato kikubwa kwa mume
 
Hapo ndo pabaya unaishi ndoto zake na pengine una mchango mkubwa kwa familia yake ila ikitokea mume katangulia mbele ya haki wanakusahau na hata mtoto wanamsahau,ushauri wanaume kabla hamjatuoa tunaomba mmalizane na familia zenu na hakikisha ushajenga kwenu,tukianzisha familia yetu tengeneza maisha ya wanao na mkeo jua siku ukiondoka wanao watateseka na hao uliowasomesha hawatolisha mwanao zaidi watadai mali zako.
Familia zetu za kitanzania mwanaume akiwa na uwezo ndugu wote wanajaa na kuwa extended family ila akifa inageuka kuwa nuclear family.
 
Mbona mambo ya mume yanaendelea?
ndoa ikiwa katika defaults zake, hakuwezi kuwa na mambo ya Mume, na mwanamke kama mleta mada naye analilia afanye mambo yake.
Hilo sio lengo la ndoa.
Ila kosa likifanyika, mimi sinaushauri zaidi ya Kumwambia aombe hekima ya Mungu.
"Mwanamke mpumbavu huvunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe''.


akitaka kwenda kienyeji.
Na yeye ajenge, maana nilisikia waziri wa sheria anasema Mwanamke akijenga nyumba ndani ya ndoa ni yake ila mwanaume akijenga ni Ya familia. Akiamua kupitia njia hii ya kienyeji ambayo siishauri atakuwa ameamua kuongeza gap na mwisho wataachana.
 
Familia zetu za kiafrika ukitangulia kusomeshwa lazima uje usomeshe wenzio labda nyumbani kwenu maisha ya wazazi wawe wanajimudu!

Kwahiyo Dada zetu kuweni wapole tu! Kama unahisi unapunjwa leta na Wewe wadogo zako tusomeshe wote ili iwe ngoma droo
 
bila shaka wote nyie mlisahau ule msemo wa "kuungana na kuwa mwili mmoja"

kama bado anatimiza ndoto zake tu ss hivi na ww endelea na ndoto zako alafu baadae ndio mtimize malengo yenu ya pamoja kama wanandoa.

ndoa sio kitu cha kukiendea tu kirahisi rahisi.

poleni sana.
 
teh..teh... waungwana mtoa mada ni mwanaume aliyeolewa ni dada yake mzingatie hilo katika kuchangia!
kitu kikubwa ambacho watu wengi hawaelewi kuwa ndoa ni mkataba kwa hiyo kama ni mkataba kuna makubaliano ya pande mbili na pia kuna kitu cha kubadilisha kwa maslahi ya kila mmoja sasa changamoto inakuja ni kwamba huyu anaona anataka mke na mwingine anataka mume halafu vipengele muhimu vinafanywa ndani ya mkataba kitu ambacho ni ngumu sana matokeo yake upande mmoja unapoteza kwa ubinafsi wa mwingine.
 
Umeongea kweli.mtu unapoolewa kama wewe ni mwanamke mwenye ndoto zako inakua ngumu ku adjust manake sasa mnakutana watu wenye fikra tofauti.inaweza kukurudisha nyuma au kutokuendeleza maono yako kabisa.cha muhimu pande zote mbili mkubaliane vipaumbele vyenu ni nini.Ila huyo mwanaume ni mbinafsi bado.hajali mawazo yako wakati mngeweza kugwana majukumu tu.Wanaume wa siku hizi bana!kuzaa uzae kwa shida na bado kujenga mjenge wote
 
ndoa ikiwa katika defaults zake, hakuwezi kuwa na mambo ya Mume, na mwanamke kama mleta mada naye analilia afanye mambo yake.
Hilo sio lengo la ndoa.
Ila kosa likifanyika, mimi sinaushauri zaidi ya Kumwambia aombe hekima ya Mungu.
"Mwanamke mpumbavu huvunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe''.


akitaka kwenda kienyeji.
Na yeye ajenge, maana nilisikia waziri wa sheria anasema Mwanamke akijenga nyumba ndani ya ndoa ni yake ila mwanaume akijenga ni Ya familia. Akiamua kupitia njia hii ya kienyeji ambayo siishauri atakuwa ameamua kuongeza gap na mwisho wataachana.
Mpaka kulileta hapa anaonyesha jinsi gani linavyomuumiza.
Nimevigundua hivi vitu hapa kwa mleta mada

1- wivu (roho ya kwa nini)
2- ligi.(ushindani)
3-huenda anashindwa kuelewa maana ya ndoa(kabla ya ndoa alikuwa anawaza ndoa tu shela na harusi baabu kubwa. Bila hata kuifikiria ndoa yenyewe
4-ubinafsi.(umimi kwanza)
 
Back
Top Bottom