Ukifa, usijali kuhusu mwili wako...!

Ukifa, usijali kuhusu mwili wako...!

Somotimes sio kifo bali tunaowaach na wanaotuacha

Bab
Mam
Mke
Watoto
Jamaa zako


Very sad

Kifo chako binafs si issue
 
Very sad ni kwamba wote tutakufa

Kuna usiku mmoja nililala nikaota nimekufa, kwa kweli kuna upweke fulani niliuona ambao ulinikosesha amani, yani ni kwamba baada ya kuwa nimekufa nikawa nimetokea eneo fulani kama nyika hivi na nikatambua kuwa na mm nimekufa ,ila eneo hilo halina watu wengi ,ni kama eneo la watu wanao subiria kitu fulani, yani kila mtu yupo kivyake vyake.

Eneo hilo halina mwanga mkali kama wa mchana ,ni mwanga ambao upo kama inataka kunyesha mvua, au wakati jua limefunikwa na mawingu. Basi baada ya kujijua nimekufa nikaanza kuwaza mwenyewe kwamba, nilikuwa naambiwa kuna hukumu baada ya kufa sasa mimi itakuwaje kwa matendo yangu? ... Ila nikajipa moyo kwamba kama Mungu husamehe basi na mm nitasemehewa mana nilikumbuka kuwa kabla ya kulala usiku huo nilitubu. Nikawaida yangu kutubu na kuomba rehema kabla ya kulala kila mara,Hili nilifundishwa na mchungaji fulani.

Sasa eneo nililo fikia baada ya kugundua kuwa na mm ni miongoni mwa marehemu tayari, ni eneo ambalo linaupweke mno na zaidi ya yote kuna majuto fulani ya kuona ya kuwa maisha ya duniani si kitu, yaani unaona kabisa kama duniani ulikuwa unapoteza mda tu na kujilaumu baadhi ya mambo uliyokuwa ukiyafanya. Eneo hilo linarudisha picha nyuma ya maisha ya duniani harafu unaona hayakuwa na maana kabisa, kwa maana unajiona kabisa kuwa unaanza maisha mengine ambayo unakuwa haujui hatima yake.

Hii ndoto ilinishitua sana mana nilisituka usingizin ndo nikajua kumbe bado sijafa,ila hadi leo huwa najiiuliza ni nn maana ya ile ndoto.
 
Dah ee mola nisaidie kila nifanyalo nikumbuke napita maana nisipowaza hivyo nitajikweza bure

Rest easy my parents mliniacha imara japo i was too yangu japo mliniachia upweke baada ya ndugu wa pekee wa damu pia kuwafuata

Mshana Jr umenigusa sana na kunirudisha mbali sana be blessed kaka .
 
Kaka umenipa tafakari nzito sanaa 🤦🏽‍♂️🤦🏽‍♂️

Ni vile binadamu tumeumbwa kufanya attachment kwa watu na vitu ila mwisho wa siku havitokuwa na maana kama hukuishi kwa furaha kwa kila sekunde

Kujijali na kujipenda kwanza ni muhimu zaidi kuliko kitu kingine chochote.. 🙏
 

Ayu 1:21​

"...Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe."
 
Ndugu na jamaa zako watafanya kila kitu
Watakuvua nguo
Watakuosha
Watakuvisha
Watakutoa nje ya nyumba na kukupeleka kwenye anuani yako mpya.
Wengi watakuja kwenye mazishi kwa kukuheshimu wengine hata wataghairi mipango yao na kuomba ruhusa kwenda msibani.

Vitu vyako ambavyo ulivipenda sana vitauzwa, kugawiwa au kuchomwa moto.
Vitu vyako
Nguo zako
Vitabu vyako
Mali zako...

Misha maisha yataendelea.
Mtu aliye na uwezo sawa au hata bora atachukua nafasi yako.
Mali yako itabadilika kuwa urithi.
Na usiwe na shaka kuwa juu yako kwa mambo madogo na makubwa uliyofanya katika maisha yako yatazungumza, kuhukumu, kutia shaka na kukosoa.

Watu waliokujua tu usoni watasema, "Maskini!"
Marafiki wako wazuri watalia kwa saa chache au siku kadhaa, lakini kisha watacheka tena.
Familia yako kipenzi watazoea mmiliki mpya.
Picha zako zitaning'inia ukutani kwa muda, kisha zitawekwa kwenye kabati na hatimaye kuhifadhiwa chini ya boksi.

Mtu mwingine atakaa kwenye kitanda chako na kula kutoka humo.
Maumivu makali ndani ya nyumba yako yatadumu wiki, mbili, mwezi mmoja, mwaka mmoja, ... .basi utajiunga na kumbukumbu na kisha hadithi yako itaisha.
Itaisha kati ya watu, itaishia hapa, itaishia katika ulimwengu huu.
Lakini hadithi yako huanza katika ukweli mpya ... katika maisha yako baada ya kifo.
Maisha yako ni ya duniani ambapo hutaweza kuondoka na vitu ulivyokuwa navyo hapa utapoteza maana huko uendako havina maana tena ...!

Uzuri wa mwili wako
Jina la familia
Mali
Nafasi ya kazi
Akaunti ya benki
Nyumba
Gari

Vyeo vya kitaaluma
Wanafunzi wenzako
Nyara
Marafiki wa dunia
watoto
Familia
Katika maisha yako mapya, utahitaji roho yako tu.
Mali pekee itakayodumu ni nafsi.

Kwa hivyo jaribu kuishi maisha yako kamili na kuwa na furaha ukiwa hapa kwa sababu, “Hutachukua ulicho nacho kutoka hapa. Unachukua tu kile ulichotoa!" .View attachment 2327416
Mkuu una akili Sana ,ni wachache watakuelewa
 
Naogopa mauti, naogopa siku ambayo watu wataacha kuniita jina langu na kuniita marehemu....watanivua nguo zangu na kuniosha, huku siwezi kujitetea😭

Kinachonitisha naenda wapi? Nitakuwa Nani? Wakati huo sina huu mwili wangu mzuri nnaoupenda, sina Kazi, sina vyeti....vitachomwa Moto😭 sina familia wala kampani, nitakuwa wapi? Kama Nani? Nitapotea? Nitapoteaje?
 
Naogopa mauti, naogopa siku ambayo watu wataacha kuniita jina langu na kuniita marehemu....watanivua nguo zangu na kuniosha, huku siwezi kujitetea

Kinachonitisha naenda wapi? Nitakuwa Nani? Wakati huo sina huu mwili wangu mzuri nnaoupenda, sina Kazi, sina vyeti....vitachomwa Moto sina familia wala kampani, nitakuwa wapi? Kama Nani? Nitapotea? Nitapoteaje?
Ndio maana tunatakiwa tusiwekeze kwenye roho zaidi kuliko mwili uharibikao..

Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana.
 
Back
Top Bottom