UKAWA Vs SERIKALI, kwa staili hii sioni mshindi

UKAWA Vs SERIKALI, kwa staili hii sioni mshindi

Sasa hivi sirikali yetu hainyukani tena na UKAWA bali wameamua kushindana na Tundu Lissu ambaye amekuwa akiiumbua kila wanapomfikisha mahakamani. Ni aibu kwa sirikali kupambana na mtu mmoja kila mara huku akiwashinda kwenye sheria (sijazungumzia hukumu ya kesi za Tundu Lissu)
Kila utawala huibuka MPAMBANAJI tishio kwa serikali,Mkapa alikuwa na Mtikila,JK akawa na Slaa na awamu hii namuona Lissu kwa mbali anakuja
 
Mkuu umenena ukweli, ninacho amini serikali itende kazi zake kwa mujibu wa sheria. Vyama navyo vitekeleze majukumu yake kwa mujibu wa sheria. Magufuli akitenda vyema umma utaona. Lakini kwa hoja hizi za kuwa siasa hadi 2020 kweli Rais kapotoka. Je mikutano ya wapinzani inamuzuiaje yeye kutekeleza ilani? Rais asitake kushangiliwa tu na kuabudiwa, yapaswa pia akosolewe. Asidhanie kuzuia mikutano ya vyama vya siasa ndio kutampa uhalali wa yeye na chama chake kushinda general election 2020. No, Bali ni jinsi gani ameifanya nchi kupiga hatua mbele kiuchumi na kuleta usitawi mpana wa jamii. Wapo wenye mawazo mgando wanadhani kuwa vyama vikifanya mikutano inazuia maendeleo. TRA na wachumi wabobezi wake hapa wathibitishe kwa data kuwa pato letu hushuka kipindi cha uchaguzi na huwa juu kabula na baada ya kipindi hicho. Au mwenye ushahidi na siyo blaa blaa anikosoe kwa takwimu za kitafiti. LET DEMOCRACY REIGN, otherwise Rais atangaze state of emergency kwa mujibu wa katiba ili tujue nchi iko katika state of emergency. Vinginevyo statement kuwa siasa hadi 2020 ni batili na inakiuka katiba na sheria za nchi ikiwemo sheria ya vyama vya siasa.
 
Na huyo ndo anaweka negative mentality kwa watu kuwa rais ni dicteta....Kitu ambacho sio kweli....Nchi haipaswi kuendeshwa kwa lelemama....Raisi anapaswa kuwa serious kama anafanyavyo sasa ili mambo yaende....Mbele,pia watu wanapaswa kufahamu kuwa president is system...Kama akiwa weak everything will wrong.
Ndugu yangu!!
Sidhani kama sirikali ya inapingwa kihivo, maana ingejikita katika kutumbua majipu, kujipanga jinsi ya kuleta maendeleo kwa Wadanganyika sisi hakika nakuhakikishia kuwa kama wangejikita huko kutuletea neema, na kutupa mema ndugu yangu tungekuwa mbali katika nchi hii. Wapinzani hawana kitu ichochote ambacho kinge watoa wadanganyika kwa rahisi wetu mpendwa.
Nionavyo wote tumejazwa mihemko viongozi wetu, sisi wenyewe bado ni vipofu wa hali ya juu yaani ni zaidi ya nyumbu au ngombe wenye mikia na wasio na mikia ndivyo tulivyo ndugu yangu.
 
Ndugu yangu!!
Sidhani kama sirikali ya inapingwa kihivo, maana ingejikita katika kutumbua majipu, kujipanga jinsi ya kuleta maendeleo kwa Wadanganyika sisi hakika nakuhakikishia kuwa kama wangejikita huko kutuletea neema, na kutupa mema ndugu yangu tungekuwa mbali katika nchi hii. Wapinzani hawana kitu ichochote ambacho kinge watoa wadanganyika kwa rahisi wetu mpendwa.
Nionavyo wote tumejazwa mihemko viongozi wetu, sisi wenyewe bado ni vipofu wa hali ya juu yaani ni zaidi ya nyumbu au ngombe wenye mikia na wasio na mikia ndivyo tulivyo ndugu yangu.
Mm kwa maono yangu hii serikali iko kwa lengo la kuwaletea maendeleo sisi wanyonge,ndo maana imeanza kwa kuhakikisha wale wahusika wa kutupatia huduma mhimu maofisin na mawizaran wote wana kuwa waafilifu na wachapakazi....Ndo maana kuna mahakamaa ya mafisadi now...Kwa maana huwezi ukasema utaboresha huduma za jamii wakati kuna watu wazembe na wala rushwa....I hope utumbuaji wa majipu utakuja kuwa na tija baadae kwa watanzania....
 
Kuwazuia ndo shida za watanzania zitaisha!? au wakipewa ruhusa na maandamo /mikutano yao ikalindwa na polisi, vipaumbele vya serikali vitakosa bajeti!?
Uncle, ukitafakari kwa kina utagundua kuwa msingi wa matamko na makatazo haya havina lengo la kiuchumi wala usitawi wa jamii Bali ni kutafuta kuabudiwa, kutotaka kukosolewa na zaidi kuvinyima vyama vya upinzani platform ili ngosha na wenzie wapite kiulaini 2020. Na hiyo iliundiwa mkakati wa mapema kwa kuanza na issue ya kuzuia matangazo ya bunge live kwa sababu ambazo hadi leo zimeshindwa kueleweka. But l'm sure it is a wrong decision, ni maamuzi yaliyojengwa na hofu iliyotokana na mchaka mchaka wa 2015. Rais asiache hofu hiyo imutawale kwani akitenda vyema watanzania tutaona na kumpa kura zetu muda ukifika, vinginevyo ataifanya 2020 kuwa zaidi ya 2015. The President should not govern impulsively
 
Jamani Rasi hatakiwi atawale anatakiwa aongoze. Maana ya kuongoza ni kwamba kiongozi ana timu ya viongozi wengine ambao anakubaliana nao na ndipo anayatangaza yaliyokubaliwa. Na kati ya hao anajadiliana nao kuna wakulima, wafanyakazi, vyama vyote vya siasa including wapinzani. Huo ndio uongozi. Ijapokuwa Raisi anatoka Ccm yeye hapaswi kubagua watu wake kwani yeye ni baba wa taifa zima. Haiwezekani Raisi awaseme Ukawa katika mikutano yake halafu wao wakae kimya mpaka 2020. Simple logic!! Rasi wetu tunampenda lakini afuate sheria na kuwatendea vyama vyote sawa. Hapo atapendeka kuliko sasa. Simple!
 
Kwa maoni yangu mimi nadhani pamoja na mambo yote lakini serikali inatakiwa kuwa strong, vinginevyo kila mtu anaweza kujitangazia kuwa yeye ni rais. Hata hivyo, rais angeenda mbali zaidi, yaani angeongeza kibano kwa mtu yeyote anayetamka maneno ya kejeli na uchochezi.
Utapata u dc kazana sana atakufikiria
 
Tangu mkutano wake wa kwanza bungeni aliwawaita "watoto" eti kwa sababu walisimama na kutoka nje wakati Mh. Shein alipoingia ukumbini kuhusiana na mambo ya Znzbar. Je mambo ya kule ni madogo? Ni kwa nini Raisi anayaona ni upuuzi na wala hataki mazungumzo? Haoni kuwa ni uonevu mkubwa sana na kila moja anaona hata kama hawasemi? Wapinzani walitaka angalau Raisi atoe neno linaloonyesha kuwa yeye ni binadamu mwenye huruma kwa watu wote na siyo tu wanachama wa chama chake. Tabia hii itatucost siku moja. Kuongea ni muhimu kama alivyoshauri Mh. Lowasa ambaye amejaa utu.
 
UKAWA died a long time ago. There are merely illegal users of the brand.
 
Na huyo ndo anaweka negative mentality kwa watu kuwa rais ni dicteta....Kitu ambacho sio kweli....Nchi haipaswi kuendeshwa kwa lelemama....Raisi anapaswa kuwa serious kama anafanyavyo sasa ili mambo yaende....Mbele,pia watu wanapaswa kufahamu kuwa president is system...Kama akiwa weak everything will wrong.
Vizuri ndg, yafaa pia umshauri Mkulu aheshimu na kufuata katiba. Vyama kuendesha siasa halitakiwi kuwa jambo la hisani au kuonewa huruma. Wakubali kukosolewa kwani nchi ni yetu wote watz. Pale ambapo wengine hawaridhiki na baadhi ya maamuzi, kufungua mjadala ndio busara, na sio kulazimisha cha Mkubwa. Polisi wana kazi kubwa sana ya kulinda usalama wa raia, sasa hivi wanatumika zaidi kulazimisha matakwa ya kisiasa. Sasa nao wameanza kuweka na kutekeleza maamuzi yao kwenye siasa.
Maendeleo sio wananchi kuwa wa NDIOO, bali ni kukua kwa uwezo kwa mwananchi kupata mahitaji yake. Kwa mipango mizuri (na sio kukurupuka na mapya kila siku) INAWEZEKANA bila ya kukaba wananchi wengine.
 
Ni vema kwa Raisi kuwa strong lakini kuna tofauti ya kuwa strong na kuwa a bully or sadist. Raisi aliye strong ni mwenye haki kwa wote ila anakuwa mkali kwa wale wenye kufanya uovu. Raisi asifurahie kutumia polisi ili kubully wale ambao hawawezi kutumia polici. Raisi kwa cheo chake is a very strong person hakuna wa kumzidi yeye. Anajifanya weak kwa kutumia police bila ya sababu. Aketi chini na wapinzani na chama chake na wapange pamoja jinsi ya kutuletea maendeleo tunayolilia sote. Tumechoka na usanii huu wa sasa ambao unaletwa na Ikulu yetu. Vyama vyote ni sawa hakuna bora kuliko kingine. Wote wapate nafasi sawa. Na tutaishi kwa amani. Full stop!!
 
Kitu kingine ni hiki. Viongozi waongoze kwa mifano na siyo kwa nguvu. Kama kiongozi anawaita watoto wake vilasa na mwingine anawaita wapiga kura malofa kwa kuwa tu wanapingana na mawazo yake hao ni viongozi ambao hatutaki tabia zao kwani wawakwaza wengine. Hawa wanatakiwa pia wapelekwe mahakamani siyo tu wale wanaomwita Raisi dikteta. Kama baba unaonyesha tabia mbaya kwa watoto wako inabidi ukubali wakianza na wao kukutukana. Kiongozi asijione yuko juu ya sheria. Mimi nimemsikiliza Obama kwa miaka saba sijawahi akisema mimi anasema "we not I" na sijamsikia akitukana hata siku moja.
 
Nadhani tuache siasa turudishe nchi kwenye maadili kama mkuu wetu anavyodhamiria lakini anakosea mbinu
 
Na huyo ndo anaweka negative mentality kwa watu kuwa rais ni dicteta....Kitu ambacho sio kweli....Nchi haipaswi kuendeshwa kwa lelemama....Raisi anapaswa kuwa serious kama anafanyavyo sasa ili mambo yaende....Mbele,pia watu wanapaswa kufahamu kuwa president is system...Kama akiwa weak everything will wrong.
Ni kweli kabisa, kuwa serious ikiwemo kuwazuia wapinzani kuzungumza na wananchi hata kama katiba inawaruhusu!
 
Katiba lazima iheshimiwe. Iwe Raisi isiwe Raisi. Maana ya maadili ni pamoja na kuiheshimu katiba ya nchi. Nchi hii pia iwe na checks and balances. Na hiyo ni pamoja na kuwa na upinzani makini.
 
Vizuri ndg, yafaa pia umshauri Mkulu aheshimu na kufuata katiba. Vyama kuendesha siasa halitakiwi kuwa jambo la hisani au kuonewa huruma. Wakubali kukosolewa kwani nchi ni yetu wote watz. Pale ambapo wengine hawaridhiki na baadhi ya maamuzi, kufungua mjadala ndio busara, na sio kulazimisha cha Mkubwa. Polisi wana kazi kubwa sana ya kulinda usalama wa raia, sasa hivi wanatumika zaidi kulazimisha matakwa ya kisiasa. Sasa nao wameanza kuweka na kutekeleza maamuzi yao kwenye siasa.
Maendeleo sio wananchi kuwa wa NDIOO, bali ni kukua kwa uwezo kwa mwananchi kupata mahitaji yake. Kwa mipango mizuri (na sio kukurupuka na mapya kila siku) INAWEZEKANA bila ya kukaba wananchi wengine.
Umesema vema sana mkubwa,pia naomba nikuambie kuwa hii nchi inawatu wengi sana na pia wenye mawazo na matamanio tofauti....Kutokana na hilo maamzi ya serikali ni ngumu sana kumlizisha kila mtu wa nchi hiii.....Ndo maana serikali huingia madarakani ikiwa na ilan kama muongozo na dira ya serikali.... Pia yafanyayo na serikali hii yamo ndan ya ilan yao..... PIa nakuomba na ww usiamimishwe na wanasiasa kuwa mkuu wa nchi hii anakiuka katiba ya nchi hii lakin anasimamia misingi ya utawala bora ambao kila raia huwa hapendwi kubanwa na sheria..... PIa suala la mikutano ya kisiasa haiwezi kuwa kichocheo cha maendeleo ya nchi na ndo maana mkuu ameweka kapuni kidogo kuliko kuruhusu watu wawe bize na siasi pasipo kufanya kazi za maendeleo yao....Asante
 
Ni vema kwa Raisi kuwa strong lakini kuna tofauti ya kuwa strong na kuwa a bully or sadist. Raisi aliye strong ni mwenye haki kwa wote ila anakuwa mkali kwa wale wenye kufanya uovu. Raisi asifurahie kutumia polisi ili kubully wale ambao hawawezi kutumia polici. Raisi kwa cheo chake is a very strong person hakuna wa kumzidi yeye. Anajifanya weak kwa kutumia police bila ya sababu. Aketi chini na wapinzani na chama chake na wapange pamoja jinsi ya kutuletea maendeleo tunayolilia sote. Tumechoka na usanii huu wa sasa ambao unaletwa na Ikulu yetu. Vyama vyote ni sawa hakuna bora kuliko kingine. Wote wapate nafasi sawa. Na tutaishi kwa amani. Full stop!!
Nakumbuka kauli ya Lowasa alisema,Siasa ni mazungumzo na makubaliano huja kwenye meza ya mazungumzo,hivyo basi UKAWA wanapaswa kufuata huo ushauri na watafute namna ya kukutana na wanasiasa wenzao wazungumze kuliko kujitokeza mbele ya hadhara na kutoa matamko yenye kuvunja aman ya nchi kwa wananchi wenye...... imagine ww ni raisi afu unaskia matamko kama hayo....Utachukua uamzi gan....Akiacha kuwa wasihi polisi walinde usalama wa raia afu wapate matatizo baada ya hiyo Ukuta napo watakuwa na kiki ya kuzungumzia....Tuacheni siasa na tuwe realistics buana...
 
Kwa maoni yangu mimi nadhani pamoja na mambo yote lakini serikali inatakiwa kuwa strong, vinginevyo kila mtu anaweza kujitangazia kuwa yeye ni rais. Hata hivyo, rais angeenda mbali zaidi, yaani angeongeza kibano kwa mtu yeyote anayetamka maneno ya kejeli na uchochezi.
Mkuu makalio yana kazi ya kutoa kinyesi hayahusiki na kufikiri mkuu! So ukifikiri kwa makalio ni sawa na kujisaidia mbele za watu
 
Back
Top Bottom