UKAWA Vs SERIKALI, kwa staili hii sioni mshindi

Uncle Jei Jei

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
1,684
2,157
Sio serikali wala UKAWA mtakaoibuka kededea kwenye hii minyukano ya kisiasa ya kila siku.

Kila mara viongozi waandamizi wa serikali wanaposimama huja na kauli tata juu ya upinzani na kwa watanzania kwa ujumla kana kwamba uwepo wa upinzani ndio sababu ya umaskini na matatizo yasiyoisha ya watanzania.

Katika kujibu hoja, wapinzani nao wakiibuka wanakuja kifua mbele kupinga na kueleza msimamo wao wa kupinga kauli tata za serikali.

Katika hali ya kusikitisha misimamo ya wapinzani na kauli hizo tata za serikali za mara kwa mara vyote kwa pamoja havina tija ya moja kwa moja kwa watanzania zaidi ni kama vinachochoe hali mbaya kwa watanzania.

Nionavyo mimi serikali Katika wiki kadhaa za mwanzo wa uhai na upya wake ni kama walikuwa wanakuja vizuri. Nasema hivi kwa sababu serikali ilianza kushughulika na matatizo ya watanzania kwa vitendo moja kwa moja. Lakini kadiri siku zinavyoenda naona kama wamehama nakuelekeza nguvu zao kushughulika na wanasiasa wa upinzani.

Mara kwa mara serikali imekuwa ikisisitiza nidhamu na nidhamu yenyewe wanayoitaka kwa mtazamo wangu ni ile ya "akikohoa hata kwa bahati mbaya itika Naaamu". Na hao wanaoambiwa waitike hawako tayari na hawatakaa wakubali kuitika eti kisa yeye ni mkubwa kwani hata wakiitika au wasipoitika hakuna baya watakalokuwa wametenda.

Kwanini serikali isiindelee kama ilivyokuwa imeanza!? Kwani muhimbili tayari vitanda vimetosha!? Bandarini je, makontena yanalipa ushuru na hayatoroshwi!? Wanafunzi je, wote wameshapata madawati, vitabu, maabara, chemicals na walimu wakutosha!? Hivi, hizi zahanati na vituo vya Afya, hospitali na maduka ya dawa ya msd vina dawa na vifaa tiba vya kutosha!?

Kipi kitawamaliza wapinzani, ni kukimbizana nao kila siku barabarani, kwenye mikutano na mahakamani au kutatua matatizo ya moja kwa moja ya watanzania!?

Hivi haya matatizo ya elimu, Afya, miundombinu, na stahiki za wafanyakazi vikishughulikiwa ipasavyo na serikali, hawa wanaoitisha maandamano wataitisha kwa sababu gani!? Na hata wakiitisha nani ataenda wakati anaona matatizo yake yanafanyiwa kazi!?
Huku kutunishiana misuli kukiendelea hivi, si serikali wala upinzani watakaoibuka na ushindi zaidi zaidi ni watanzania wote tutakaoendelea kuumia!
Wekeend njema!
 
Umeelezea kwa uzr kabsa....Ila stl serikali inafanya ivyo sema kuna mambo mengi yanaingilia hayo....Ikiwemo suala ya upinzan kupiga masuala hayo!!!
 
Sasa hivi sirikali yetu hainyukani tena na UKAWA bali wameamua kushindana na Tundu Lissu ambaye amekuwa akiiumbua kila wanapomfikisha mahakamani. Ni aibu kwa sirikali kupambana na mtu mmoja kila mara huku akiwashinda kwenye sheria (sijazungumzia hukumu ya kesi za Tundu Lissu)
 
Na huyo ndo anaweka negative mentality kwa watu kuwa rais ni dicteta....Kitu ambacho sio kweli....Nchi haipaswi kuendeshwa kwa lelemama....Raisi anapaswa kuwa serious kama anafanyavyo sasa ili mambo yaende....Mbele,pia watu wanapaswa kufahamu kuwa president is system...Kama akiwa weak everything will wrong.
 
Na huyo ndo anaweka negative mentality kwa watu kuwa rais ni dicteta....Kitu ambacho sio kweli....Nchi haipaswi kuendeshwa kwa lelemama....Raisi anapaswa kuwa serious kama anafanyavyo sasa ili mambo yaende....Mbele,pia watu wanapaswa kufahamu kuwa president is system...Kama akiwa weak everything will wrong.
hapo mwishoni kwenye hayo maneno ambayo sii ya kiswahili....nadhani kuna maneno ya hiyo lugha ....umeyaacha.....na mengine umeyatumia kimakosa...

ama nakushauri utumie kiswahili tu utaeleweka bila shida.....
 
Nimepapenda hapa


Nionavyo mimi serikali Katika wiki kadhaa za mwanzo wa uhai na upya wake ni kama walikuwa wanakuja vizuri. Nasema hivi kwa sababu serikali ilianza kushughulika na matatizo ya watanzania kwa vitendo moja kwa moja. Lakini kadiri siku zinavyoenda naona kama wamehama nakuelekeza nguvu zao kushughulika na wanasiasa wa upinzani.

Hongera zako kaka
 
Sio serikali wala UKAWA mtakaoibuka kededea kwenye hii minyukano ya kisiasa ya kila siku.

Kila mara viongozi waandamizi wa serikali wanaposimama huja na kauli tata juu ya upinzani na kwa watanzania kwa ujumla kana kwamba uwepo wa upinzani ndio sababu ya umaskini na matatizo yasiyoisha ya watanzania.

Katika kujibu hoja, wapinzani nao wakiibuka wanakuja kifua mbele kupinga na kueleza msimamo wao wa kupinga kauli tata za serikali.

Katika hali ya kusikitisha misimamo ya wapinzani na kauli hizo tata za serikali za mara kwa mara vyote kwa pamoja havina tija ya moja kwa moja kwa watanzania zaidi ni kama vinachochoe hali mbaya kwa watanzania.

Nionavyo mimi serikali Katika wiki kadhaa za mwanzo wa uhai na upya wake ni kama walikuwa wanakuja vizuri. Nasema hivi kwa sababu serikali ilianza kushughulika na matatizo ya watanzania kwa vitendo moja kwa moja. Lakini kadiri siku zinavyoenda naona kama wamehama nakuelekeza nguvu zao kushughulika na wanasiasa wa upinzani.

Mara kwa mara serikali imekuwa ikisisitiza nidhamu na nidhamu yenyewe wanayoitaka kwa mtazamo wangu ni ile ya "akikohoa hata kwa bahati mbaya itika Naaamu". Na hao wanaoambiwa waitike hawako tayari na hawatakaa wakubali kuitika eti kisa yeye ni mkubwa kwani hata wakiitika au wasipoitika hakuna baya watakalokuwa wametenda.

Kwanini serikali isiindelee kama ilivyokuwa imeanza!? Kwani muhimbili tayari vitanda vimetosha!? Bandarini je, makontena yanalipa ushuru na hayatoroshwi!? Wanafunzi je, wote wameshapata madawati, vitabu, maabara, chemicals na walimu wakutosha!? Hivi, hizi zahanati na vituo vya Afya, hospitali na maduka ya dawa ya msd vina dawa na vifaa tiba vya kutosha!?

Kipi kitawamaliza wapinzani, ni kukimbizana nao kila siku barabarani, kwenye mikutano na mahakamani au kutatua matatizo ya moja kwa moja ya watanzania!?

Hivi haya matatizo ya elimu, Afya, miundombinu, na stahiki za wafanyakazi vikishughulikiwa ipasavyo na serikali, hawa wanaoitisha maandamano wataitisha kwa sababu gani!? Na hata wakiitisha nani ataenda wakati anaona matatizo yake yanafanyiwa kazi!?
Huku kutunishiana misuli kukiendelea hivi, si serikali wala upinzani watakaoibuka na ushindi zaidi zaidi ni watanzania wote tutakaoendelea kuumia!
Wekeend njema!
Hao tunasubiri tarehe 1 waandamane.
 
Sio serikali wala UKAWA mtakaoibuka kededea kwenye hii minyukano ya kisiasa ya kila siku.

Kila mara viongozi waandamizi wa serikali wanaposimama huja na kauli tata juu ya upinzani na kwa watanzania kwa ujumla kana kwamba uwepo wa upinzani ndio sababu ya umaskini na matatizo yasiyoisha ya watanzania.

Katika kujibu hoja, wapinzani nao wakiibuka wanakuja kifua mbele kupinga na kueleza msimamo wao wa kupinga kauli tata za serikali.

Katika hali ya kusikitisha misimamo ya wapinzani na kauli hizo tata za serikali za mara kwa mara vyote kwa pamoja havina tija ya moja kwa moja kwa watanzania zaidi ni kama vinachochoe hali mbaya kwa watanzania.

Nionavyo mimi serikali Katika wiki kadhaa za mwanzo wa uhai na upya wake ni kama walikuwa wanakuja vizuri. Nasema hivi kwa sababu serikali ilianza kushughulika na matatizo ya watanzania kwa vitendo moja kwa moja. Lakini kadiri siku zinavyoenda naona kama wamehama nakuelekeza nguvu zao kushughulika na wanasiasa wa upinzani.

Mara kwa mara serikali imekuwa ikisisitiza nidhamu na nidhamu yenyewe wanayoitaka kwa mtazamo wangu ni ile ya "akikohoa hata kwa bahati mbaya itika Naaamu". Na hao wanaoambiwa waitike hawako tayari na hawatakaa wakubali kuitika eti kisa yeye ni mkubwa kwani hata wakiitika au wasipoitika hakuna baya watakalokuwa wametenda.

Kwanini serikali isiindelee kama ilivyokuwa imeanza!? Kwani muhimbili tayari vitanda vimetosha!? Bandarini je, makontena yanalipa ushuru na hayatoroshwi!? Wanafunzi je, wote wameshapata madawati, vitabu, maabara, chemicals na walimu wakutosha!? Hivi, hizi zahanati na vituo vya Afya, hospitali na maduka ya dawa ya msd vina dawa na vifaa tiba vya kutosha!?

Kipi kitawamaliza wapinzani, ni kukimbizana nao kila siku barabarani, kwenye mikutano na mahakamani au kutatua matatizo ya moja kwa moja ya watanzania!?

Hivi haya matatizo ya elimu, Afya, miundombinu, na stahiki za wafanyakazi vikishughulikiwa ipasavyo na serikali, hawa wanaoitisha maandamano wataitisha kwa sababu gani!? Na hata wakiitisha nani ataenda wakati anaona matatizo yake yanafanyiwa kazi!?
Huku kutunishiana misuli kukiendelea hivi, si serikali wala upinzani watakaoibuka na ushindi zaidi zaidi ni watanzania wote tutakaoendelea kuumia!
Wekeend njema!

ukawa ukawa !!! mbona hatuuni huo ukawa zaidi ya CDM
 
Sasa hivi sirikali yetu hainyukani tena na UKAWA bali wameamua kushindana na Tundu Lissu ambaye amekuwa akiiumbua kila wanapomfikisha mahakamani. Ni aibu kwa sirikali kupambana na mtu mmoja kila mara huku akiwashinda kwenye sheria (sijazungumzia hukumu ya kesi za Tundu Lissu)

Namuona kwa mbaaaali Rama akipiga jaramba, ole wenu mjaribu huo ushetani wenu.
 
Meli ni chache sana bandarini,sijui ni jitihada gani tunafanya za kuona idadi inaongezeka, tunabaki kukimbizana huku vichochoroni bila sababu ya msingi. biashara ni matangazo na wahenga walisema mteja ni mfalme,huku kwetu mteja ni fala.
 
Nimepapenda hapa


Nionavyo mimi serikali Katika wiki kadhaa za mwanzo wa uhai na upya wake ni kama walikuwa wanakuja vizuri. Nasema hivi kwa sababu serikali ilianza kushughulika na matatizo ya watanzania kwa vitendo moja kwa moja. Lakini kadiri siku zinavyoenda naona kama wamehama nakuelekeza nguvu zao kushughulika na wanasiasa wa upinzani.

Hongera zako kaka

Asante Mkuu
 
Serikali iko vizuri imehama kunyukana NA Ukawa Yaani UKUTA ambapo ni general objective hadi kunyukana na Tundu Lissu yaani Specific, tumepata serikali makini. Mshahara ya watumishi kuongezwa sio tatizo ila Tundu Lissu ni tatizo, Bora maaskari wale posho ya kumlinda kuliko walimu kuongezewa mshahara.Tumepata viongozi makini, tuwaombee
 
Ni ukweli, nikiangalia mambo yanavyoenda naona upinzani wanaanza kupata umaarufu na kukubalika zaidi, ni vyema serikali ikaacha vyama vya siasa vikafanya kazi yao, na wao wakatimiza wajibu wao lakini kupiga marufuku na kuzuia watu kuonesha hisia zao au kuongea mtazama wao ambao unatofautiana na serikali umeanza kuleta hisia kuwa serikali haitaki kukosolewa jambo ambalo wengi wameanza kuona ni tatizo. Bado tunamatumaini mengi na serikali lakini ikubali kukosolewa ili na wao wajirekebishe kwa maslahi ya taifa na nchi yetu wote.

Mungu ibariki Tanzania

Sio serikali wala UKAWA mtakaoibuka kededea kwenye hii minyukano ya kisiasa ya kila siku.

Kila mara viongozi waandamizi wa serikali wanaposimama huja na kauli tata juu ya upinzani na kwa watanzania kwa ujumla kana kwamba uwepo wa upinzani ndio sababu ya umaskini na matatizo yasiyoisha ya watanzania.

Katika kujibu hoja, wapinzani nao wakiibuka wanakuja kifua mbele kupinga na kueleza msimamo wao wa kupinga kauli tata za serikali.

Katika hali ya kusikitisha misimamo ya wapinzani na kauli hizo tata za serikali za mara kwa mara vyote kwa pamoja havina tija ya moja kwa moja kwa watanzania zaidi ni kama vinachochoe hali mbaya kwa watanzania.

Nionavyo mimi serikali Katika wiki kadhaa za mwanzo wa uhai na upya wake ni kama walikuwa wanakuja vizuri. Nasema hivi kwa sababu serikali ilianza kushughulika na matatizo ya watanzania kwa vitendo moja kwa moja. Lakini kadiri siku zinavyoenda naona kama wamehama nakuelekeza nguvu zao kushughulika na wanasiasa wa upinzani.

Mara kwa mara serikali imekuwa ikisisitiza nidhamu na nidhamu yenyewe wanayoitaka kwa mtazamo wangu ni ile ya "akikohoa hata kwa bahati mbaya itika Naaamu". Na hao wanaoambiwa waitike hawako tayari na hawatakaa wakubali kuitika eti kisa yeye ni mkubwa kwani hata wakiitika au wasipoitika hakuna baya watakalokuwa wametenda.

Kwanini serikali isiindelee kama ilivyokuwa imeanza!? Kwani muhimbili tayari vitanda vimetosha!? Bandarini je, makontena yanalipa ushuru na hayatoroshwi!? Wanafunzi je, wote wameshapata madawati, vitabu, maabara, chemicals na walimu wakutosha!? Hivi, hizi zahanati na vituo vya Afya, hospitali na maduka ya dawa ya msd vina dawa na vifaa tiba vya kutosha!?

Kipi kitawamaliza wapinzani, ni kukimbizana nao kila siku barabarani, kwenye mikutano na mahakamani au kutatua matatizo ya moja kwa moja ya watanzania!?

Hivi haya matatizo ya elimu, Afya, miundombinu, na stahiki za wafanyakazi vikishughulikiwa ipasavyo na serikali, hawa wanaoitisha maandamano wataitisha kwa sababu gani!? Na hata wakiitisha nani ataenda wakati anaona matatizo yake yanafanyiwa kazi!?
Huku kutunishiana misuli kukiendelea hivi, si serikali wala upinzani watakaoibuka na ushindi zaidi zaidi ni watanzania wote tutakaoendelea kuumia!
Wekeend njema!
 
Ukawa vs CCM kisheria ukawa anashinda

Ukawa vs CCM kwa nguvu ya jesh la polic, CCM inashinda
 
Kwa maoni yangu mimi nadhani pamoja na mambo yote lakini serikali inatakiwa kuwa strong, vinginevyo kila mtu anaweza kujitangazia kuwa yeye ni rais. Hata hivyo, rais angeenda mbali zaidi, yaani angeongeza kibano kwa mtu yeyote anayetamka maneno ya kejeli na uchochezi.
 
Back
Top Bottom