Nitazungumzia vitu viwili;-
1- Katika nukuu za mwalimu aliwahi kusema kua "
muogopeni sana mtu anayetaka kwenda ikulu kwa gharama yoyote" na pia alisema kua "
ikulu hamna biashara ikulu ni mzigo ni lawama" hivyo mtu anaeng'ang'ania kwenda kule lazima atuambie kuna nini huko, mbona anatumia nguvu nyingi sana kwendAa huko?? Sikatai kua Magufuli anataka kwenda ikulu kama mgombea mwingine yoyote lakini njia, utapeli, ujanja, ulaghai, gharama, zinazotumiaka na wagombea hawa wakubwa wawili ndizo zinazowatutofautisha na kutufanya tumjue nani mwenye tamaa ya ikulu na nani anania ya kwenda ikulu kuwatumikia wananchi. Lowasa alipochukua fomu ya Urais CCM alijua dhahiri kua kuna wagombea wengi na hivyo anaweza kukosa au kupata. Ila alipoona amekosa kwa vile anabiashara yake yeye na kundi lake wanataka wakaifanye ikulu akaamua kuhama na kuzinunua taasisi nyingine 4 kwa usiku mmoja kwa sababu tu aliahidiwa kua atapewa nafasi ya kutimiza nia yake ya kufanya biashara yake ikulu. Kila mtanzania ni shahidi kua ni kias gani Lowasa ametumia cha fedha tangu akiwa CCM hadi sasa ili tu apate nafasi ya kuingia ikulu. Swali la kujiuliza ni 1) anatumia fedha zote ili aende ikulu kwa maslahi ya nani?? 2) fedha zote kazipata wapi?? basi tufanye marafiki zake ndio waliomchangi sawa, ila wamemchangia yeye ili aende ikulu wao watafaidikaje?? Kila mtazania anataka mabadiliko ila mabadiliko gani hapo ndo wengi tunatofautiana. Magufuli kila mmoja anaujua utendaji kazi wake, Hakuna wakupinga kua ni mchapakazi, mfuatiliaji na mtu makini. Mabadiliko ninayoyataka mimi ni kumchagua kiangozi mchapakazi, amabae kila mmoja anajua na ameshuhudia. Mtanzania tafakari kura yako ni ya dhamani sana, usiipoteze.
[URL=https://www.jamiiforums.com/usertag.php?do=list&action=hash&hash=hapakazitu]#hapakazitu .[/URL]
2- Suala la mfumo. Huwa nashangaa sana chadema wanapopiga kelele juu ya mfumo wa ccm na hua najiuliza swali moja dogo, je! kama wao mfumo wa kupata viongozi wa chama mpaka karne hii ni wakuruthishana, kama wao wanachukia mifumo mibovu, kwanini wasirekebise mfumo wa chama chao ili uwe mfano na tuweze kuwaamini kua hata wakija kwenye nchi wataweka mfumo mzuri. Kama mtu jambo dogo limekushinda utaniaminishaje kua kubwa utaliweza?? Pia angalia mfumo wao wanaotumia kupata mgombea. Ni mfumo uliojaaa usiri wa hali ya juu. Alafu mnadhubutu kujiita chama cha demokrasia, Demokrasia ganai ya kujifungia chumbani na kuja na mgombea?? Demokrasia gani ya kupuuza mawazo ya mtu aliekipandisha chama toka chini hadi juu alafu leo mnamleta mtu mwingine kuja kuchukua nafasi ya huyo mpiganaji?? Kama nyie wenyewe mnasalitiana, kwanini tuwaamini kua hamtatusaliti sisi wananchi tukiwapa nafasi. Mnakua wanafki mpaka kwa nafsi zenu wenyewe. Uroho na njaa zitawamaliza na hii dhambhi ya usaliti itawatafuna hata muende wapi. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki CCM, Mungu mbariki Magufuli.
#hapakazitu