UKAWA vs Magufuli: Kisa cha nahodha na meli

UKAWA vs Magufuli: Kisa cha nahodha na meli

Jamal Akbar

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2014
Posts
413
Reaction score
473
Wengi wa wanaosapoti UKAWA wana hoja kwamba MAGUFULI hafai kuwa Raisi kwasababu eti yu katika MFUMO (SYSTEM) ambayo ndio tatizo. Watu hawa wamefika mbele zaidi na kutoa mifano ya Nahodha mzuri (MAGUFULI) ambaye wanadai hawezi kuivusha meli mbovu iliyotoboka kutokana na dhoruba. Nitajadili hoja hii kwa kujikita zaidi katika mfano huu huu wa MELI na NAHODHA (Meli na Nahodha zikisimama "symbolize" kwa nafasi ya Nchi na Raisi)

Kwa kawaida kabla ya NAHODHA kuanza safari HUKAGUA MELI yake kuhakikisha iko salama ikiwa ni moja kati ya jitihada za kuhakikisha anamaliza safari salama. Ukaguzi huu hauishii tu kwa NAHODHA kukagua MELI, Uimara na utayari wa Nahodha kukisimamia chombo pia ni suala la msingi na muhimu (ikumbukwe ukaguzi haufanywi kwa kukurupuka tu SAFARI ikikaribia kwani unaweza kufika katikati ya SAFARI na kugundua hukuandaa kila kitu hivyo kuangamiza KILA KILICHOMO KWENYE MELI kwa kifupi ni kwamba Maandalizi Kurupushi ya maigizo ni HATARI sana kwa SAFARI hii).

Ni dhahiri kuwa MAGUFULI alifanya UKAGUZI SAHIHI WA MELI HII kabla ya kuanza kwa safari na amelidhihirisha hilo katika Wizara zote alizoziongoza na ndio maana hahitaji kuingia kwenye masoko na na barabarani leo hii kutafuta matatizo kwani ni wazi ukikurupuka unaweza pata SPARE ZA KICHINA zisizoweza kustahimili MAWIMBI NA DHORUBA YA SAFARI HASA PALE UNAPOKUWA NA NAHODHA ASIYE NA UTAYARI WA KIUTENDAJI NA KIAFYA. Umuhimu wa NAHODHA imara upo waziwazi kwani hata tukirudi kwenye Maandiko matakatifu wakati Bwana Yesu alipokuwa akisafiri na wanafunzi wake aliamshwa kutoka usingizini ili kutuliza Dhoruba (naomba nieleweke simfananishi kwa namna yeyote ile Mgombea yeyote Yule na Bwana Yesu BALI naonyesha umuhimu wa Nahodha hodari katika safari)

Ieleweke kwamba kama MELI ina matobo hata kutia Nanga haitoweza kwani ITAZAMA. Kichekesho kinakuja unapowauliza UKAWA ni jinsi gani Watatuvusha katika Dhoruba hii wengi hujibu "haijalishi nahodha gani anaingia kuongoza alimradi wasafirishaji hawa wametoka kwanza", haya ni majibu yanayostahili kuitwa ya KILOFA. Hatuwezi kufanya gambling katika uongozi wa Nchi la sivyo yatatukumba kama yaliyoikumba Titanic. Hatutaki kupata NAHODHA yeyote tu aingie KUONGOZA MELI hii, Tunataka aliyejipanga kuongoza nchi apate nafasi hiyo. Hatutaki NAHODHA aliyehamia kampuni nyingine kutafuta nafasi ileile aliyonyimwa katika kampuni ya awali baada ya kunyimwa kazi kisa alizamisha Boti na Mitumbwi hapo kabla kisha leo hii tumpe unahodha wa MELI KUBWA.

Ikumbukwe pia Mfumo unaundwa na Wanasiasa (Politicians) + Watendaji (Bureaucrats). Politicians hupatikana kwa kura lakini Bureaucrats hupatikana kwa Merits. Bureaucrats wanatakiwa kuwa non-political lakini kwa mfumo wa Nchi yetu ulivyo sasa wako subordinate to Politicians ambapo WAZIRI MKUU ndiye MKUU WAO. CHADEMA wanasema wanataka kupambana na MFUMO lakini wameshindwa kuuvunja MFUMO MBOVU WALIO NAO HIVI SASA. Nikirejea moja kati ya thread zilizowekwa humu ndani kuelezea mfumo wa CHADEMA unaohoji Jinsi CHADEMA wanavyopeana uongozi na kuachiana vyeo ni dhahiri mfumo wao ni mbovu zaidi. Nanukuu "Aliyeanzisha chama ni Edwin Mtei na ndiyo mwasisi wa Chadema na ndio Mwenyekiti wa kwanza wa Chama hicho, Mwenyekiti aliyefuata ni marehemu Bob Makani ambae alimuoa dada wa Mtei, na Mwenyekiti wa sasa Kamuoa mtoto wa Mtei ambae ni mwasisi na mwenyekiti wa kwanza wa chadema". Hapo Bado hawajashika MELI wana mfumo mbovu hivi, vipi wakipata UNAHODHA.

Kiulinganishi Mmoja wa waomba nafasi ya UNAHODHA aliwahi kuwa mkuu wa MFUMO na MATOBO ALIYOYALETA kwa nchi hii yanafahamika. UKAWA WALILIONA HILI KUANZIA MUDA MREFU NA WALIMSHAMBULIA HADI AKAACHIA NGAZI, LEO HII WAMEMPA UONGOZI WAKITAKA AONGOZE JITIHADA ZAO ZA KUPEWA TENDA AMBAPO NAHODHA WAO ATAKUWA YULEYULE WALIYEMPINGA SIKU ZOTE. (This is Non-sense na ni hapa ndipo tunatakiwa Tunapoanza kuhoji na kupata mashaka kwamba huyu NAHODHA anayetafuta nafasi kwa nguvu zote hataleta mtandao wake kama ambavyo amekwishaanza kwa kumvuta SUMA-YEYE?

Watanzania hatuko tayari kumkabidhi fisi bucha, hatuwezi kutoa tenda ya UNAHODHA wa meli kwa NAHODHA MCHOVU, anayepita mitaani kujua matatizo wakati safari imekwishawadia, hatuko tayari kuzama. Ninaamini TINGATINGA la kazi lipo Kura Yangu nitampa NAHODHA SAHIHI MTENDAJI WA KUAMINIKA Dr. JOHN POMBE MAGUFULI "Every era has its chair, THIS IS MAGUFULI's ERA #HapaKaziTu
 
Afadhali ukawa nahodha anaweza akawa si mzuri. Ila huko meli mbovu, ukawa kuna manahodha wasaidizi wasaidizi wazuri.. Uko unapopatetea pamoja na ubovu wa meli lakini manahodha wasaidizi wabovu. Hapo sijamzungumzia nahodha..
Hata chombo kinapoelekea nako siko.
 
Inashangaza sana pale mtu anaposema eti Magufuli hana shida ila tatizo ni mfumo wakati mtu anayempigia debe eti ataleta mabadiliko aliomba ridhaa ya kuwa nahodha kwenye mfumo huo huo. Je kama kweli mfumo ni mbovu mbona aliomba kua unahodha? hii inanifanya niamini kua mfumo sio mbovu ila ni kujitetea tuu
 
Afadhali ukawa nahodha anaweza akawa si mzuri. Ila huko meli mbovu, ukawa kuna manahodha wasaidizi wasaidizi wazuri.. Uko unapopatetea pamoja na ubovu wa meli lakini manahodha wasaidizi wabovu. Hapo sijamzungumzia nahodha..
Hata chombo kinapoelekea nako siko.
lakini naomba utambue nguvu alizonazo nahodha (kifedha na kimamlaka kulingana na katiba) kwenye chombo hiki je wasaidizi wake wanaweza kumbana zaidi ya kumshauri tuu
 
Afadhali ukawa nahodha anaweza akawa si mzuri. Ila huko meli mbovu, ukawa kuna manahodha wasaidizi wasaidizi wazuri.. Uko unapopatetea pamoja na ubovu wa meli lakini manahodha wasaidizi wabovu. Hapo sijamzungumzia nahodha..
Hata chombo kinapoelekea nako siko.
panga vzuri hoja zko ndipo uongee
 
inashangaza sana pale mtu anaposema eti magufuli hana shida ila tatizo ni mfumo wakati mtu anayempigia debe eti ataleta mabadiliko aliomba ridhaa ya kuwa nahodha kwenye mfumo huo huo. Je kama kweli mfumo ni mbovu mbona aliomba kua unahodha? Hii inanifanya niamini kua mfumo sio mbovu ila ni kujitetea tuu
mimi ndio maana sioni mkapa alipokosea kuwaita hawa jamaa pumbafu
 
Nitazungumzia vitu viwili;-
1- Katika nukuu za mwalimu aliwahi kusema kua "muogopeni sana mtu anayetaka kwenda ikulu kwa gharama yoyote" na pia alisema kua "ikulu hamna biashara ikulu ni mzigo ni lawama" hivyo mtu anaeng'ang'ania kwenda kule lazima atuambie kuna nini huko, mbona anatumia nguvu nyingi sana kwendAa huko?? Sikatai kua Magufuli anataka kwenda ikulu kama mgombea mwingine yoyote lakini njia, utapeli, ujanja, ulaghai, gharama, zinazotumiaka na wagombea hawa wakubwa wawili ndizo zinazowatutofautisha na kutufanya tumjue nani mwenye tamaa ya ikulu na nani anania ya kwenda ikulu kuwatumikia wananchi. Lowasa alipochukua fomu ya Urais CCM alijua dhahiri kua kuna wagombea wengi na hivyo anaweza kukosa au kupata. Ila alipoona amekosa kwa vile anabiashara yake yeye na kundi lake wanataka wakaifanye ikulu akaamua kuhama na kuzinunua taasisi nyingine 4 kwa usiku mmoja kwa sababu tu aliahidiwa kua atapewa nafasi ya kutimiza nia yake ya kufanya biashara yake ikulu. Kila mtanzania ni shahidi kua ni kias gani Lowasa ametumia cha fedha tangu akiwa CCM hadi sasa ili tu apate nafasi ya kuingia ikulu. Swali la kujiuliza ni 1) anatumia fedha zote ili aende ikulu kwa maslahi ya nani?? 2) fedha zote kazipata wapi?? basi tufanye marafiki zake ndio waliomchangi sawa, ila wamemchangia yeye ili aende ikulu wao watafaidikaje?? Kila mtazania anataka mabadiliko ila mabadiliko gani hapo ndo wengi tunatofautiana. Magufuli kila mmoja anaujua utendaji kazi wake, Hakuna wakupinga kua ni mchapakazi, mfuatiliaji na mtu makini. Mabadiliko ninayoyataka mimi ni kumchagua kiangozi mchapakazi, amabae kila mmoja anajua na ameshuhudia. Mtanzania tafakari kura yako ni ya dhamani sana, usiipoteze. [URL=https://www.jamiiforums.com/usertag.php?do=list&action=hash&hash=hapakazitu]#hapakazitu .[/URL]

2- Suala la mfumo. Huwa nashangaa sana chadema wanapopiga kelele juu ya mfumo wa ccm na hua najiuliza swali moja dogo, je! kama wao mfumo wa kupata viongozi wa chama mpaka karne hii ni wakuruthishana, kama wao wanachukia mifumo mibovu, kwanini wasirekebise mfumo wa chama chao ili uwe mfano na tuweze kuwaamini kua hata wakija kwenye nchi wataweka mfumo mzuri. Kama mtu jambo dogo limekushinda utaniaminishaje kua kubwa utaliweza?? Pia angalia mfumo wao wanaotumia kupata mgombea. Ni mfumo uliojaaa usiri wa hali ya juu. Alafu mnadhubutu kujiita chama cha demokrasia, Demokrasia ganai ya kujifungia chumbani na kuja na mgombea?? Demokrasia gani ya kupuuza mawazo ya mtu aliekipandisha chama toka chini hadi juu alafu leo mnamleta mtu mwingine kuja kuchukua nafasi ya huyo mpiganaji?? Kama nyie wenyewe mnasalitiana, kwanini tuwaamini kua hamtatusaliti sisi wananchi tukiwapa nafasi. Mnakua wanafki mpaka kwa nafsi zenu wenyewe. Uroho na njaa zitawamaliza na hii dhambhi ya usaliti itawatafuna hata muende wapi. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki CCM, Mungu mbariki Magufuli. #hapakazitu
 
Afadhali ukawa nahodha anaweza akawa si mzuri. Ila huko meli mbovu, ukawa kuna manahodha wasaidizi wasaidizi wazuri.. Uko unapopatetea pamoja na ubovu wa meli lakini manahodha wasaidizi wabovu. Hapo sijamzungumzia nahodha..
Hata chombo kinapoelekea nako siko.
Hauwezi kumzungumzia Nahodha kwasababu ni dhahiri ana historia ya kuzamisha meli alizowahi kuziongoza, na Meli bila nahodha haiendi
 
Nitazungumzia vitu viwili;-
1- Katika nukuu za mwalimu aliwahi kusema kua "muogopeni sana mtu anayetaka kwenda ikulu kwa gharama yoyote" na pia alisema kua "ikulu hamna biashara ikulu ni mzigo ni lawama" hivyo mtu anaeng'ang'ania kwenda kule lazima atuambie kuna nini huko, mbona anatumia nguvu nyingi sana kwendAa huko?? Sikatai kua Magufuli anataka kwenda ikulu kama mgombea mwingine yoyote lakini njia, utapeli, ujanja, ulaghai, gharama, zinazotumiaka na wagombea hawa wakubwa wawili ndizo zinazowatutofautisha na kutufanya tumjue nani mwenye tamaa ya ikulu na nani anania ya kwenda ikulu kuwatumikia wananchi. Lowasa alipochukua fomu ya Urais CCM alijua dhahiri kua kuna wagombea wengi na hivyo anaweza kukosa au kupata. Ila alipoona amekosa kwa vile anabiashara yake yeye na kundi lake wanataka wakaifanye ikulu akaamua kuhama na kuzinunua taasisi nyingine 4 kwa usiku mmoja kwa sababu tu aliahidiwa kua atapewa nafasi ya kutimiza nia yake ya kufanya biashara yake ikulu. Kila mtanzania ni shahidi kua ni kias gani Lowasa ametumia cha fedha tangu akiwa CCM hadi sasa ili tu apate nafasi ya kuingia ikulu. Swali la kujiuliza ni 1) anatumia fedha zote ili aende ikulu kwa maslahi ya nani?? 2) fedha zote kazipata wapi?? basi tufanye marafiki zake ndio waliomchangi sawa, ila wamemchangia yeye ili aende ikulu wao watafaidikaje?? Kila mtazania anataka mabadiliko ila mabadiliko gani hapo ndo wengi tunatofautiana. Magufuli kila mmoja anaujua utendaji kazi wake, Hakuna wakupinga kua ni mchapakazi, mfuatiliaji na mtu makini. Mabadiliko ninayoyataka mimi ni kumchagua kiangozi mchapakazi, amabae kila mmoja anajua na ameshuhudia. Mtanzania tafakari kura yako ni ya dhamani sana, usiipoteze. #hapakazitu .

2- Suala la mfumo. Huwa nashangaa sana chadema wanapopiga kelele juu ya mfumo wa ccm na hua najiuliza swali moja dogo, je! kama wao mfumo wa kupata viongozi wa chama mpaka karne hii ni wakuruthishana, kama wao wanachukia mifumo mibovu, kwanini wasirekebise mfumo wa chama chao ili uwe mfano na tuweze kuwaamini kua hata wakija kwenye nchi wataweka mfumo mzuri. Kama mtu jambo dogo limekushinda utaniaminishaje kua kubwa utaliweza?? Pia angalia mfumo wao wanaotumia kupata mgombea. Ni mfumo uliojaaa usiri wa hali ya juu. Alafu mnadhubutu kujiita chama cha demokrasia, Demokrasia ganai ya kujifungia chumbani na kuja na mgombea?? Demokrasia gani ya kupuuza mawazo ya mtu aliekipandisha chama toka chini hadi juu alafu leo mnamleta mtu mwingine kuja kuchukua nafasi ya huyo mpiganaji?? Kama nyie wenyewe mnasalitiana, kwanini tuwaamini kua hamtatusaliti sisi wananchi tukiwapa nafasi. Mnakua wanafki mpaka kwa nafsi zenu wenyewe. Uroho na njaa zitawamaliza na hii dhambhi ya usaliti itawatafuna hata muende wapi. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki CCM, Mungu mbariki Magufuli. #hapakazitu
Well said Mkuu
 
UKAWAZZZ.jpg
 
Alifanya ukaguzi? Hahahaha hata hujitambui. ..mtu kakurupuka kuchukua form, hakujipanga, nakuhakikishia Kama Magufuli atapita basi atatumiki mabwana walio mshawishi kuchukua form, upo hapo?
 
Nitazungumzia vitu viwili;-
1- Katika nukuu za mwalimu aliwahi kusema kua "muogopeni sana mtu anayetaka kwenda ikulu kwa gharama yoyote" na pia alisema kua "ikulu hamna biashara ikulu ni mzigo ni lawama" hivyo mtu anaeng'ang'ania kwenda kule lazima atuambie kuna nini huko, mbona anatumia nguvu nyingi sana kwendAa huko?? Sikatai kua Magufuli anataka kwenda ikulu kama mgombea mwingine yoyote lakini njia, utapeli, ujanja, ulaghai, gharama, zinazotumiaka na wagombea hawa wakubwa wawili ndizo zinazowatutofautisha na kutufanya tumjue nani mwenye tamaa ya ikulu na nani anania ya kwenda ikulu kuwatumikia wananchi. Lowasa alipochukua fomu ya Urais CCM alijua dhahiri kua kuna wagombea wengi na hivyo anaweza kukosa au kupata. Ila alipoona amekosa kwa vile anabiashara yake yeye na kundi lake wanataka wakaifanye ikulu akaamua kuhama na kuzinunua taasisi nyingine 4 kwa usiku mmoja kwa sababu tu aliahidiwa kua atapewa nafasi ya kutimiza nia yake ya kufanya biashara yake ikulu. Kila mtanzania ni shahidi kua ni kias gani Lowasa ametumia cha fedha tangu akiwa CCM hadi sasa ili tu apate nafasi ya kuingia ikulu. Swali la kujiuliza ni 1) anatumia fedha zote ili aende ikulu kwa maslahi ya nani?? 2) fedha zote kazipata wapi?? basi tufanye marafiki zake ndio waliomchangi sawa, ila wamemchangia yeye ili aende ikulu wao watafaidikaje?? Kila mtazania anataka mabadiliko ila mabadiliko gani hapo ndo wengi tunatofautiana. Magufuli kila mmoja anaujua utendaji kazi wake, Hakuna wakupinga kua ni mchapakazi, mfuatiliaji na mtu makini. Mabadiliko ninayoyataka mimi ni kumchagua kiangozi mchapakazi, amabae kila mmoja anajua na ameshuhudia. Mtanzania tafakari kura yako ni ya dhamani sana, usiipoteze. #hapakazitu .

2- Suala la mfumo. Huwa nashangaa sana chadema wanapopiga kelele juu ya mfumo wa ccm na hua najiuliza swali moja dogo, je! kama wao mfumo wa kupata viongozi wa chama mpaka karne hii ni wakuruthishana, kama wao wanachukia mifumo mibovu, kwanini wasirekebise mfumo wa chama chao ili uwe mfano na tuweze kuwaamini kua hata wakija kwenye nchi wataweka mfumo mzuri. Kama mtu jambo dogo limekushinda utaniaminishaje kua kubwa utaliweza?? Pia angalia mfumo wao wanaotumia kupata mgombea. Ni mfumo uliojaaa usiri wa hali ya juu. Alafu mnadhubutu kujiita chama cha demokrasia, Demokrasia ganai ya kujifungia chumbani na kuja na mgombea?? Demokrasia gani ya kupuuza mawazo ya mtu aliekipandisha chama toka chini hadi juu alafu leo mnamleta mtu mwingine kuja kuchukua nafasi ya huyo mpiganaji?? Kama nyie wenyewe mnasalitiana, kwanini tuwaamini kua hamtatusaliti sisi wananchi tukiwapa nafasi. Mnakua wanafki mpaka kwa nafsi zenu wenyewe. Uroho na njaa zitawamaliza na hii dhambhi ya usaliti itawatafuna hata muende wapi. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki CCM, Mungu mbariki Magufuli. #hapakazitu
Watanzania wenye akili kichwani mpo wengi sana. Nakupongeza sana mkuu, Big up sana! Nafurahi sana kuona kuna watu wenye akili za kuhoji na sio bendera fuata upepo. Binadamu lazima uwe tofauti na nyumbu. #hapakazitu.
 
Alifanya ukaguzi? Hahahaha hata hujitambui. ..mtu kakurupuka kuchukua form, hakujipanga, nakuhakikishia Kama Magufuli atapita basi atatumiki mabwana walio mshawishi kuchukua form, upo hapo?
Magufuli hakukurupuka kuchukua form au ulitaka aweke maigizo kama mzee wenu yeye alishasema maigizo kwake hawezi yeye ni #HapaKaziTu maigizo waachie wengine.
 
Afadhali ukawa nahodha anaweza akawa si mzuri. Ila huko meli mbovu, ukawa kuna manahodha wasaidizi wasaidizi wazuri.. Uko unapopatetea pamoja na ubovu wa meli lakini manahodha wasaidizi wabovu. Hapo sijamzungumzia nahodha..
Hata chombo kinapoelekea nako siko.
Mfano mzuri ni sisi ambao tunaishi mijini, tunapanda daladala mbovu, lakini tunafika tunapoenda, ukweli ni kwamba nahodha ndiye muhimu sana, awe phsically fit
 
Inashangaza sana pale mtu anaposema eti Magufuli hana shida ila tatizo ni mfumo wakati mtu anayempigia debe eti ataleta mabadiliko aliomba ridhaa ya kuwa nahodha kwenye mfumo huo huo. Je kama kweli mfumo ni mbovu mbona aliomba kua unahodha? hii inanifanya niamini kua mfumo sio mbovu ila ni kujitetea tuu

Tatizo la watanzania wengi ni hili hatuwezi kujua lililo mbele, tupo kama vipofu, hivi mtu mgonjwa ni wa kumuamini? Maana muda wowote linaweza kumtokea lolote
 
Umenena ki utu uzima, MAGUFULI ndio nahodha
 
Suala la mfumo mbovu CHADEMA mimi nimeliona kabla hujalisema hili mkuu, ni wazi wazi kwamba CHADEMA kuna mfumo wa undugu, ukabila na ukaskazini.
 
Back
Top Bottom