Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,169
- 48,451
Hapa siwazungumzia wana UKAWA ambao ni watu wa kawaida mitaani wasio na nyadhifa kwenye vyama vinavyounda UKAWA. Hapa nawalenga viongozi wa vyama hivyo kuanzia wenyeviti wao hadi maofisa wa Makao Makuu kwenye vyama hivyo.
Kuna suala linaendelea la kuwa na Rais bila ya kuwa na Baraza la Mawaziri, hivi msimamo wa UKAWA ni nini hasa. Wao wanaona kuwa ni sawa au si sawa? Kwa maana nyingine kama wao ndiyo wangekuwa wamepewa serikali mpaka leo wangekuwa pia hawajatangaza baraza lao la mawaziri?
Hili jambo la Bandari UKAWA wana taarifa gani kuhusu sakata zima? Kwa maana watu wafahamu kuwa Bandari ya Dar es salaam ina uwezo wa kutunza kwa wakati mmoja Makontena zaid ya milioni 4. kwa maana nyingine hayo zaidi ya 2000 yanayotajwa na Waziri Mkuu Majaliwa ni tone tu katika makontena yanayopitia Dar es salaam. Maana yangu ni kwamba inawezekana kuna watu wameachwa kutokana na maslahi ya kisiasa waliyonayo Waziri Mkuu na wenzake ndani ya CCM.
Ada elekezi kwa shule binafsi UKAWA wao msimamo wao ni upi? Maana wenye shule zao wameahidi kutozifungua msimu wa kufungua ukifika. Je UKAWA wanandhani hatua za Serikali ni sahihi au si sahihi na wao msimamo wao ni upi? Wanaona hiyo njia wanayotumia Serikali ndiyo itakuwa inajenga uwezo wa shule za Umma na kuboresha elimu au ndiyo Elimu inashushwa kiwango chake?
Halafu kuna hili la CCM kufanyia vikao vyake kwenye ofisi kuu ya Umma Tanzania, Ikulu. Kama sheria inazuia siasa kwenye majengo ya umma kama mashule na kadhalika inakuwaje chama cha siasa kitumie Ikulu ambayo ni ofisi kuu ya Umma kufanyia vikao vyake? Je UKAWA na wao wangeshika madaraka wangetumia Ikulu kufanyia vikao vyao vya kisiasa.
UKAWA ni wazembe sana, kila inapotokea nafasi ya kujijenga kisiasa wao huwa wako Bize na harakati zisizo na mashiko!
Kuna suala linaendelea la kuwa na Rais bila ya kuwa na Baraza la Mawaziri, hivi msimamo wa UKAWA ni nini hasa. Wao wanaona kuwa ni sawa au si sawa? Kwa maana nyingine kama wao ndiyo wangekuwa wamepewa serikali mpaka leo wangekuwa pia hawajatangaza baraza lao la mawaziri?
Hili jambo la Bandari UKAWA wana taarifa gani kuhusu sakata zima? Kwa maana watu wafahamu kuwa Bandari ya Dar es salaam ina uwezo wa kutunza kwa wakati mmoja Makontena zaid ya milioni 4. kwa maana nyingine hayo zaidi ya 2000 yanayotajwa na Waziri Mkuu Majaliwa ni tone tu katika makontena yanayopitia Dar es salaam. Maana yangu ni kwamba inawezekana kuna watu wameachwa kutokana na maslahi ya kisiasa waliyonayo Waziri Mkuu na wenzake ndani ya CCM.
Ada elekezi kwa shule binafsi UKAWA wao msimamo wao ni upi? Maana wenye shule zao wameahidi kutozifungua msimu wa kufungua ukifika. Je UKAWA wanandhani hatua za Serikali ni sahihi au si sahihi na wao msimamo wao ni upi? Wanaona hiyo njia wanayotumia Serikali ndiyo itakuwa inajenga uwezo wa shule za Umma na kuboresha elimu au ndiyo Elimu inashushwa kiwango chake?
Halafu kuna hili la CCM kufanyia vikao vyake kwenye ofisi kuu ya Umma Tanzania, Ikulu. Kama sheria inazuia siasa kwenye majengo ya umma kama mashule na kadhalika inakuwaje chama cha siasa kitumie Ikulu ambayo ni ofisi kuu ya Umma kufanyia vikao vyake? Je UKAWA na wao wangeshika madaraka wangetumia Ikulu kufanyia vikao vyao vya kisiasa.
UKAWA ni wazembe sana, kila inapotokea nafasi ya kujijenga kisiasa wao huwa wako Bize na harakati zisizo na mashiko!