Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,176
- 48,460
- Thread starter
- #21
Jana walikuwa na Kikao cha Kamati Kuu ya chama chao CCM!kikao gani cha CCM kilichofanyikia ikulu
Jana walikuwa na Kikao cha Kamati Kuu ya chama chao CCM!kikao gani cha CCM kilichofanyikia ikulu
Mkuu hili unalijua leo? unatakiwa ukapimwe akili kama alivyowahi kushauri mchungaji Msigwa! UKAWA hawajali maslahi mapana ya wananchi....LENGO la UKAWA ni Kutwaa MADARAKA hata kama Kiongozi wao ni JIWE ....
Jana walikuwa na Kikao cha Kamati Kuu ya chama chao CCM!
Wewe umerukia kama wale watoto wa kike JK aliosema wanapata mimba kwa viherehere vyao. Kwanza napenda nimjulishe mtoa mada kwamba, hilo la upinzani kupigia kelele vikao vya chama kufanyikia ikulu sio geni. Na kwa hali ilivyo kwa Tanzania na nchi nyingi za kiafrika unapokuwa madarakani unaamua sheria gani utii na zipi usitiii. Kwa maneno marahisi chama chako kinapokuwa madarakani unakuwa juu ya sheria. Hilo la makontena kwa mazingira yalivyo hata wapinzani wakienda kutaka taarifa za kina sio rahisi kupewa maana wataambiwa wanataka kuleta siasa waache serekali ifanye kazi. Kumbuka hicho kinachoendelea hapo bandarini ni uozo wa muda mrefu na wapinzani wameshapigia kelele sana na mapendekezo wakatoa bungeni, ila utashi wa kutekeleza ndio ulikosekana. Hilo la ada elekezi ni yaleyale itaonekana wakipigia kelele au kutoa pendekezo siku hizi kuna kichaka cha kujifichia kwamba wanapenda siasa za matukio. Kuhusu baraza la mawaziri, katiba iko kimya kuhusu eneo hili. Hivyo utashi wa kiongozi husika ndio utaamua.
CC: Allen Kilewella
Mtoa mada , nakupa pole na kukushangaa sana, niliposoma uzi wako nikawaza mengi sana, kwanza nilifikili ni miongoni mwa waliotumbuliwa jibu na maumivu ni makali ,sasa unaomba angalau mawaziri wawepo ili waendelee na uzembe wao wa siku zote na majipu ya situmbuliwe. Pili nikaona unayohoja ya msingi isipo kuwa umekosea kwa kuielekeza, kuwatupia lawama UKAWA juu ya hili sio shihi kabisa. UKAWA haipo kumsaidia magufuli kufanya kazi yake vizuri, bali ipo kwaajili ya kukosoa utendaji wake na kueleza kwa wananchi namna sahihi ya utendaji. Uwezi jua katika hilo wameona nini na watakuja na jambo gani.
Unapo amua kukosoa utendaji wa mtu lazima ufanye utafiti kwanza