UKAWA na dharau kwa wateule wa Rais

UKAWA na dharau kwa wateule wa Rais

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
40,017
Reaction score
51,134
Tumeona kwa Kubenea na Makonda; kesi ipo mahakamani kwa sasa.

Baada ya muda kidogo; akaja Msigwa na Kasesera.

Sasa tena Meya wa Kinondoni anamwamkia tena DC wake. Kuna nini kwa hawa viongozi wa Ukawa dhidi ya wateule wa Rais?

Wanasahau kwamba kupingana na hawa ni sawa na kushindana na rais mwenyewe?

Kwanini viongozi wa Ukawa mnakosa adabu kwa mamlaka za nchi?

Sidhani kama ni sifa au ndio mtaonekana wapinzani bora kwa kufanya vituko kama hivyo. Mjiheshimu na nyie pia mtaheshimiwa kwa nafasi zenu.

Inasikitisha sana kuona wawakilishi wa wananchi wakikosa staha mbele ya kadamnasi.
 
Tumeona kwa kubenea na Makonda; kesi ipo mahakamani kwa sasa.

Baada ya muda kidogo; akaja msigwa na kasesera.

Sasa tena meya wa kinondoni anamwamkia tena dc wake.

kuna nini kwa hawa viongozi wa ukawa dhidi ya wateule wa Rais.

wanasahau kwamba kupingana na hawa ni sawa na kushindana na rais mwenyewe.

Kwanini viongozi wa ukawa mnakosa adabu kwa mamlaka za nchi.

sidhani kama ni sifa au ndio mtaonekana wapinzani bora kwa kufanya vituko kama hivyo.

Mjiheshimu na nyie pia mtaheshimiwa kwa nafasi zenu.

Inasikitisha sana kuona wawakilishi wa wananchi wakikosa staha mbele ya kadamnasi.
Hata hao ulio wataja nao niviongozi waliochaguliwa na Wananchi wa Tanzania
 
Tumeona kwa Kubenea na Makonda; kesi ipo mahakamani kwa sasa.

Baada ya muda kidogo; akaja Msigwa na Kasesera.

Sasa tena Meya wa Kinondoni anamwamkia tena DC wake. Kuna nini kwa hawa viongozi wa Ukawa dhidi ya wateule wa Rais?

Wanasahau kwamba kupingana na hawa ni sawa na kushindana na rais mwenyewe?

Kwanini viongozi wa Ukawa mnakosa adabu kwa mamlaka za nchi?

Sidhani kama ni sifa au ndio mtaonekana wapinzani bora kwa kufanya vituko kama hivyo. Mjiheshimu na nyie pia mtaheshimiwa kwa nafasi zenu.

Inasikitisha sana kuona wawakilishi wa wananchi wakikosa staha mbele ya kadamnasi.
Ungeelezea kwanza ni sababu zipi zinazochangia hiyo migogoro,ili tuipime na kujua ni yupi anayeenda kinyume na utaratibu.
 
Uhuru wa kuongea unaiharibu Tanzania, kila mtu anajiona ana haki ya kumkoromea mtu fulani mwenye cheo. Nchi inaharibiwa na siasa za bei rahisi, yule anayemkoromea mteule wa rais anajidanganya kwa zile sms anazotumiwa na mashabiki wake, na yeye anazidisha kiburi. Lakini kuna wateule wa rais ambao ni jeuri kama vile Paul Makonda. Huyu mheshimiwa amewawezesha watu wengi kujua kuwa mkuu wa wilaya na mkoa ni watu wenye vyeo muhimu sana.

Siasa zinatupeleka pabaya, uhuru wa kujieleza ambao umepitiliza na wenyewe ni tatizo kwetu. Lakini taratibu jamii itanyooka tu.
 
Ungeelezea kwanza ni sababu zipi zinazochangia hiyo migogoro,ili tuipime na kujua ni yupi anayeenda kinyume na utaratibu.
Hakuna cha mgogoro zaidi ya ukawa kupenda kuona madc wakilala ili ukawa wapate kick mjini. Nawashaur wachangamke la sivyo tutasema madc wanatosha.
 
Tatizo la UKAWA si dharau bali hawajui roles na responsibilities zao! Hawajui kuwa DC yuko kisheria! Mbaya zaidi hawajui Mipaka yao. Wanahitaji Semina Elekezi!
povu.jaji warioba kwenye rasim ya katiba alitaka hicho cheo cha DC kifutwe na kibaki cheo cha Ubunge kwasababu ndio aliyechaguliwa na watu.sio DC kateuliwa na mtu mmoja kwa sababu zao binafsi jiongeze dada yangu.hujui hata katiba ya nchi.


swissme
 
DC anatafuta kick kwa Rais na Meya anatafuta kick kwa wananchi sasa huoni ipi ni nzuri hapo
MZuri ni aliye active kuhudumia wananchi bila kujali anatafuta kick wapi. Nawashaur wanaojiita wawakilishi wetu nao wachangamke kutafuta kick.
 
Wewe una
Uhuru wa kuongea unaiharibu Tanzania, kila mtu anajiona ana haki ya kumkoromea mtu fulani mwenye cheo. Nchi inaharibiwa na siasa za bei rahisi, yule anayemkoromea mteule wa rais anajidanganya kwa zile sms anazotumiwa na mashabiki wake, na yeye anazidisha kiburi. Lakini kuna wateule wa rais ambao ni jeuri kama vile Paul Makonda. Huyu mheshimiwa amewawezesha watu wengi kujua kuwa mkuu wa wilaya na mkoa ni watu wenye vyeo muhimu sana.

Siasa zinatupeleka pabaya, uhuru wa kujieleza ambao umepitiliza na wenyewe ni tatizo kwetu. Lakini taratibu jamii itanyooka tu.
wewe unataka Uhuru wa kuongea ufutwe? Sasa hapo si itakuwa ni Udikteta?
 
MZuri ni aliye active kuhudumia wananchi bila kujali anatafuta kick wapi. Nawashaur wanaojiita wawakilishi wetu nao wachangamke kutafuta kick.
OK, hizo si ndiyo mnaita changamoto.
Mwambieni dogo atulie kama anavyoelekezwa asilewe sifa za Rais otherwise ataishia kwenye simu
 
povu.jaji warioba kwenye rasim ya katiba alitaka hicho cheo cha DC kifutwe na kibaki cheo cha Ubunge kwasababu ndio aliyechaguliwa na watu.sio DC kateuliwa na mtu mmoja kwa sababu zao binafsi jiongeze dada yangu.hujui hata katiba ya nchi.


swissme
Makonda alimpiga mzee Warioba, alimfutia viatu Riz sanjari na kumnyenyua juu kwa kumbeba, pia aliajiriwa na Membe kwa ajili ya kumtukana Lowasa leo hii eti naye ni mkuu wa wilaya ! ! Kutwa huwa anashinda na kamati za Ufundi akiamini atakuwa mkuu wa mkoa wa Dsm.
 
Wewe una

wewe unataka Uhuru wa kuongea ufutwe? Sasa hapo si itakuwa ni Udikteta?
Ujumbe wangu ni kwamba uhuru huu ukizidi sana unakuwa unashindwa kutofautishwa na dharau kwa mamlaka zilizopo. Tunabakia kuwa wapiga domo ambao ni masikini wenye kuzijua sana haki zao. Kila mtu anaye mtu fulani wa kumnyooshea kidole, kila mtu anaye mtu fulani ambaye kama isingelikuwa mtu huyo basi leo hii yeye na nyumba yake, wangekuwa wanaishi vizuri kabisa. Culture of blaming others for our own poverty and misfortunes.
 
Si kazi ya meya kumwelekeza DC, ye afanye yanayomuhusu. Atuambie ataleta madawat mangapi huku kitaa. Changamoto yetu si makonda.
Makonda Safari hii lazima Akonde sana licha ya kushinda kwa Sangoma kila siku.
 
Makonda Safari hii lazima Akonde sana licha ya kushinda kwa Sangoma kila siku.
Mtakonda nyie mnaokesha humu kumuhofia wakat yeye katulia na wife mida hii tayari kutumikia wana kino kesho😉
 
Tumeona kwa Kubenea na Makonda; kesi ipo mahakamani kwa sasa.

Baada ya muda kidogo; akaja Msigwa na Kasesera.

Sasa tena Meya wa Kinondoni anamwamkia tena DC wake. Kuna nini kwa hawa viongozi wa Ukawa dhidi ya wateule wa Rais?

Wanasahau kwamba kupingana na hawa ni sawa na kushindana na rais mwenyewe?

Kwanini viongozi wa Ukawa mnakosa adabu kwa mamlaka za nchi?

Sidhani kama ni sifa au ndio mtaonekana wapinzani bora kwa kufanya vituko kama hivyo. Mjiheshimu na nyie pia mtaheshimiwa kwa nafasi zenu.

Inasikitisha sana kuona wawakilishi wa wananchi wakikosa staha mbele ya kadamnasi.
Mbona ile ya Makonda kumchapa Kofi mzee Warioba umeiruka? Na ile ya Job Ndugai kumchapa mwenzake bakora kwenye kampeni je? Je, na ile ya Werema kumuita Kafulila tumbili bungeni? Hayo yote nayo hayakutokea mbele ya kadamnasi? Au kunya ni kuku tu?
 
Back
Top Bottom