king ndeshi
Senior Member
- Oct 31, 2010
- 135
- 7
Ndugu watanzania,
amani iwe kwenu,awali ya yote napenda kuwashukuru kwa uvumilivu wenu kwa kipindi chote hichi cha uchaguzi,sababu kuvumilia kwenu ndo msingi wa amani hii inayotamalaki sasa. Kuna msemo unasemaga "amani haiji kwa ncha ya upanga''
ndugu zangu tumeshampata kiongozi wetu wa nchi hata kama sio yule tulie mchagua, bado tunaowajibu wa kumpa ushirikiano ili kwa pamoja tujenge taifa letu. Ni kweli yapo mapungufu kadha wa kadha lakini hayabadilishi hali ya kisiasa tuliyo nayo sasa,mpaka yatakaporekebishwa ndipo tutabadilisha mazingira ya kisiasa.
Kila mtu wa upande wa pili pengine anamengi yakusema kuhusiana na uchaguzi,hata mimi kama kijana niliechagua mabadiliko ninayo mengi nina na uchungu pia na kwakweli nimesha lalamika sana,lakini nitakuwa kama mtu ayetaka kwenda lindi kutoka dar kwa mguu wakati kuna magari kama nitatumia kila fursa inayotokea kulalamika.
Ndugu wananchi sio kwasababu hajashinda tuliemtaka basi hatutapiga hatua hata kidogo,siamini hivyo. Inawezekana tusipate elimu bure mpaka chuo kikuu lakini tukapata elimu bure mpaka form four!
Inawezekana tusipate katiba mpya lakini katiba iliyopo ikarekebishwa tukapata tume huru ya uchaguzi
inawezekana january makamba asichaguliwe naibu waziri wa mawasiliano, lakini tukapata waziri atakae pigana mpaka vifurushi vya data na internet vikapungua bei.
Sio hayo tu,sidhani kama raisi pombe akijenga daraja litakuwa la wanachama wa ccm peke yao, kimsingi tutapita wote.
Sidhani kama raisi pombe akijenga hospitali, watatibiwa watu wa ccm peke yao,tutatibiwa wote.
Na nazani kama ikitokea tumeisoma namba, hatutaisoma wanaukawa peke yetu,tutaisoma wote,tena tutaisomea kwa mbali.
Nnachotaka kusema tusimpe raisi stress hata akashindwa kufanya aliyopanga kuyafanya...SABABU Kosa la kumsonga sana kwa maneno na vijembe vya hapa na pale ndo mwanzo wa sisi kuisoma namba.
Tumuombee kiongozi wetu,tumpe moyo na tushirikiane kujenga nchi wote ukawa na ccm,kama tunavyoshirikiana kuisoma namba.
By the way nimefurahi kumuona dada lucy magereli,amabye kura zake hazikotosha jimbo la kigamboni ambamo ninariside. kwenye list ya wabunge watakao kwenda bungeni kwa tiketi ya chadema bendera ya ukawa viti maalumu.
Mungu ibariki tanzania,mungu mbariki raisi magufuli.
wote tuseme amina..
amani iwe kwenu,awali ya yote napenda kuwashukuru kwa uvumilivu wenu kwa kipindi chote hichi cha uchaguzi,sababu kuvumilia kwenu ndo msingi wa amani hii inayotamalaki sasa. Kuna msemo unasemaga "amani haiji kwa ncha ya upanga''
ndugu zangu tumeshampata kiongozi wetu wa nchi hata kama sio yule tulie mchagua, bado tunaowajibu wa kumpa ushirikiano ili kwa pamoja tujenge taifa letu. Ni kweli yapo mapungufu kadha wa kadha lakini hayabadilishi hali ya kisiasa tuliyo nayo sasa,mpaka yatakaporekebishwa ndipo tutabadilisha mazingira ya kisiasa.
Kila mtu wa upande wa pili pengine anamengi yakusema kuhusiana na uchaguzi,hata mimi kama kijana niliechagua mabadiliko ninayo mengi nina na uchungu pia na kwakweli nimesha lalamika sana,lakini nitakuwa kama mtu ayetaka kwenda lindi kutoka dar kwa mguu wakati kuna magari kama nitatumia kila fursa inayotokea kulalamika.
Ndugu wananchi sio kwasababu hajashinda tuliemtaka basi hatutapiga hatua hata kidogo,siamini hivyo. Inawezekana tusipate elimu bure mpaka chuo kikuu lakini tukapata elimu bure mpaka form four!
Inawezekana tusipate katiba mpya lakini katiba iliyopo ikarekebishwa tukapata tume huru ya uchaguzi
inawezekana january makamba asichaguliwe naibu waziri wa mawasiliano, lakini tukapata waziri atakae pigana mpaka vifurushi vya data na internet vikapungua bei.
Sio hayo tu,sidhani kama raisi pombe akijenga daraja litakuwa la wanachama wa ccm peke yao, kimsingi tutapita wote.
Sidhani kama raisi pombe akijenga hospitali, watatibiwa watu wa ccm peke yao,tutatibiwa wote.
Na nazani kama ikitokea tumeisoma namba, hatutaisoma wanaukawa peke yetu,tutaisoma wote,tena tutaisomea kwa mbali.
Nnachotaka kusema tusimpe raisi stress hata akashindwa kufanya aliyopanga kuyafanya...SABABU Kosa la kumsonga sana kwa maneno na vijembe vya hapa na pale ndo mwanzo wa sisi kuisoma namba.
Tumuombee kiongozi wetu,tumpe moyo na tushirikiane kujenga nchi wote ukawa na ccm,kama tunavyoshirikiana kuisoma namba.
By the way nimefurahi kumuona dada lucy magereli,amabye kura zake hazikotosha jimbo la kigamboni ambamo ninariside. kwenye list ya wabunge watakao kwenda bungeni kwa tiketi ya chadema bendera ya ukawa viti maalumu.
Mungu ibariki tanzania,mungu mbariki raisi magufuli.
wote tuseme amina..