meningitis
JF-Expert Member
- Nov 17, 2010
- 8,464
- 4,828
Najitambulisha kama mkatoliki kindakindaki...na sio mara ya kwanza kufanya hivi.niliwahi kufanya hivi hapo awali na nilimtuhumu Askofu Pengo kwa tamko lake kuhusiana na mashambulizi dhidi ya mapadre wetu.inawezekana kipindi kile sikumuelewa Kadinali Pengo...nilikurupuka kumtuhumu kama alivyokurupuka Gwajima.
Nilimtuhumu kwa kupingana na msimamo wa wengi dhidi ya nani muhusika wa mashambulizi yale.nilimtuhumu kwa kutoelekeza wakatoliki tufanye nini dhidi ya ufirauni waliofanyiwa mapadre na waumini wa Kanisa katoliki,nilikasirika na kumuona ni msaliti na anasimama na serikali inayotuudhi!
Mambo yalivyoendelea nilijikuta naanza kuelewa zaidi kauli za kadinali Pengo na kuziona ni sahihi na zinazingatia ukweli au uchunguzi wa mambo.
Ndio maana kwa kauli hii ya juzi sikutaka kukurupuka.
Nimeanzisha thread zipatazo mbili kuhusu sakata na kauli ya hivi karibuni ya kadinali Pengo lengo ni kujua uhalisia na ukweli wa kile alichokisema Askofu Pengo..zote zimeishia kapuni.
madhumuni ya uzi huu ni kuwatahadharisha Ukawa juu ya kukurupuka!
Nawasihi na kuwatahadharisha Ukawa juu ya kumdharau Pengo kisa porojo na matusi ya Gwajima.
Nawatahadharisha Ukawa kutojifungamanisha na Gwajima mtu ambaye amewakosea adabu wakatoliki ...hakuna mkatoliki anayefurahishwa na matusi dhidi ya Kadinali Pengo na haitatokea kamwe hata kama angeshikwa ugoni!
Ukawa jihadharini sana!hapa ndipo mtakapopoteza!
Nawasilisha kwa uchungu!
Nilimtuhumu kwa kupingana na msimamo wa wengi dhidi ya nani muhusika wa mashambulizi yale.nilimtuhumu kwa kutoelekeza wakatoliki tufanye nini dhidi ya ufirauni waliofanyiwa mapadre na waumini wa Kanisa katoliki,nilikasirika na kumuona ni msaliti na anasimama na serikali inayotuudhi!
Mambo yalivyoendelea nilijikuta naanza kuelewa zaidi kauli za kadinali Pengo na kuziona ni sahihi na zinazingatia ukweli au uchunguzi wa mambo.
Ndio maana kwa kauli hii ya juzi sikutaka kukurupuka.
Nimeanzisha thread zipatazo mbili kuhusu sakata na kauli ya hivi karibuni ya kadinali Pengo lengo ni kujua uhalisia na ukweli wa kile alichokisema Askofu Pengo..zote zimeishia kapuni.
madhumuni ya uzi huu ni kuwatahadharisha Ukawa juu ya kukurupuka!
Nawasihi na kuwatahadharisha Ukawa juu ya kumdharau Pengo kisa porojo na matusi ya Gwajima.
Nawatahadharisha Ukawa kutojifungamanisha na Gwajima mtu ambaye amewakosea adabu wakatoliki ...hakuna mkatoliki anayefurahishwa na matusi dhidi ya Kadinali Pengo na haitatokea kamwe hata kama angeshikwa ugoni!
Ukawa jihadharini sana!hapa ndipo mtakapopoteza!
Nawasilisha kwa uchungu!