imekuwa ni jadi sasa kwa watanzania kuwa na tatizo la kusahau namna siasa za ccm zilivyo hapa nchini. Mwaka 2005 rais wa sasa kupitia c cm kikwete alionekana kuwa chaguo sahihi na baadhi ya watu na viongozi wa kidini walisema alikuwa ni chaguo la mungu!
Lakini utendaji wake na hasa katika kushughulikia matatizo ya wananchi ya moja kwa moja haukuwaridhisha wananchi wengi na baadhi wanasema kheri aondoke mapema. Leo naona amekuja dr. Magufuli
ghafla watanzania naona wamesahau taabu na suluba zilizosababishwa na uongozi wa chama kile kile cha ccm. Sasa watu wameanza tena kuweka matumaini ya ukombozi mpya wa kiuchumi na tofauti za kitabaka utakaoletwa na dr.magufuli.
Ni muhimu tukajiuliza ni njia zipi mpya ambazo dr.magufuli atatokea ambazo wenzake hawakuzipitia? Wakati wananchi tukiendelea kupigika ndani ya utawala wa ccm, dr.magufuli alikuwa ni sehemu ya uongozi uliotufikisha hapa. Ccm ina sera ambazo kwa sasa wanahitaji mfumo mpya wa uongozi na lazima wajifunze wakiwa nje ya uongozi ndipo wanaweza kuelewa haya tunayoyazungumza.
Ni vema watanzania tukawa na fikra za kimapinduzi ili kifanya maamuzi magumu dhidi utawala wa kimazoea na kuingiza utawala wa kisasa unaojali mahitaji na mawazo ya wananchi wa hali ya chini kuliko ilivyo sasa!