WanaJF,
Kiongozi wa kikundi kilichoundwa ndani ya bunge maalumu la katiba (UKAWA), mhe Mbowe, ameonyesha masikitiko yake kutokana na serikali kuwanyima mwaliko wa kuhudhuria sherehe za muungano.
Mhe. Mbowe akiwa katika hali ya majonzi amesema kwamba sherehe hizo ambazo zimetokea kuwa kivutio kikubwa kwa wananchi zilipaswa kuhudhuriwa na UKAWA kwa kuwa na wao ni sehemu ya wadau wa muungano wetu.
Aidha, mhe.Mbowe amekiri kuwa yeye pamoja na wenzake wanaounda kikundi hicho cha UKAWA walitamani sana kujumuika na viongozi wa kitaifa katika sherehe hizo kwa kuwa zimefanywa kiustadi mkubwa na hakika zinaweza kuwabadili msimamo juu ya muungano wetu.
Kiongozi wa kikundi kilichoundwa ndani ya bunge maalumu la katiba (UKAWA), mhe Mbowe, ameonyesha masikitiko yake kutokana na serikali kuwanyima mwaliko wa kuhudhuria sherehe za muungano.
Mhe. Mbowe akiwa katika hali ya majonzi amesema kwamba sherehe hizo ambazo zimetokea kuwa kivutio kikubwa kwa wananchi zilipaswa kuhudhuriwa na UKAWA kwa kuwa na wao ni sehemu ya wadau wa muungano wetu.
Aidha, mhe.Mbowe amekiri kuwa yeye pamoja na wenzake wanaounda kikundi hicho cha UKAWA walitamani sana kujumuika na viongozi wa kitaifa katika sherehe hizo kwa kuwa zimefanywa kiustadi mkubwa na hakika zinaweza kuwabadili msimamo juu ya muungano wetu.