benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,503
- 2,980
Wakati maadhimisho ya miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yakisubiriwa hapo Aprili 26 mwaka huu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameahirisha sherehe za gwaride na badala ameelekeza kufanyika kwa shughuli za maendeleo katika ngazi za mikoa.
Hii ni mara ya pili tangu Rais Samia aingie madarakani kufuta sherehe hizo na kuelelekeza zifanyike shughuli za kijamii ikiwemo usafi wa mazingira.
Taarifa ya kufutwa kwa sherehe hizo ilitolewa na Waziri Mkuu, Kassim Maialiwa alipokuwa akizindua ripoti ya pili ya machapisho ya sensa ya mgawanyo wa idadi ya watu kwa maeneo ya kiutawala na umri, katika ukumbi wa Dk Mohammed Shein, Mkoa wa Kusini Unguja.
Hata hivyo, Majaliwa hakutaja kiasi cha fedha kilichokuwa kimetengwa kwa ajili ya maadhimisho hayo wala mahali Kitakakoelekezwa.
"Maelekezo ya Rais ya maadhimisho ya sherehe hizo za Muungano mwaka huu, zitafanyika katika ngazi ya mikoa kwa kufanya shughuli za kijamii, kiuchumi na kaulimbiu itakuwa,
"Umoja na mshikamano ndiyo nguzo ya kukuza uchumi wetu uchumi wetu."
Alisema maadhimisho hayo yataanza kufanyika Aprili 17, hadi siku ya kilele Aprili 26 mwaka huu. Waziri Mkuu alisema katika kipindi hicho, taasisi na mikoa ziendelee na uzinduzi wa miradi va maendeleo sambamba na shughuli za kijamii, hasa upandaji wa miti, uchangiai wa damu hospitali na vituo vya afya, usafi wa mazingira na mashindano ya michezo na uandishi wa insha kwa shule za msingi na sekondari nchini.
Pia, katika kipindi hicho, ifanyike kampeni ya kupiga vita unyanyasaji na ukatili wa kijinsia na kampeni ya kupambana na wanaotaka kumomonyoa maadili ya taifa.
Hii ni mara ya pili tangu Rais Samia aingie madarakani kufuta sherehe hizo na kuelelekeza zifanyike shughuli za kijamii ikiwemo usafi wa mazingira.
Taarifa ya kufutwa kwa sherehe hizo ilitolewa na Waziri Mkuu, Kassim Maialiwa alipokuwa akizindua ripoti ya pili ya machapisho ya sensa ya mgawanyo wa idadi ya watu kwa maeneo ya kiutawala na umri, katika ukumbi wa Dk Mohammed Shein, Mkoa wa Kusini Unguja.
Hata hivyo, Majaliwa hakutaja kiasi cha fedha kilichokuwa kimetengwa kwa ajili ya maadhimisho hayo wala mahali Kitakakoelekezwa.
"Maelekezo ya Rais ya maadhimisho ya sherehe hizo za Muungano mwaka huu, zitafanyika katika ngazi ya mikoa kwa kufanya shughuli za kijamii, kiuchumi na kaulimbiu itakuwa,
"Umoja na mshikamano ndiyo nguzo ya kukuza uchumi wetu uchumi wetu."
Alisema maadhimisho hayo yataanza kufanyika Aprili 17, hadi siku ya kilele Aprili 26 mwaka huu. Waziri Mkuu alisema katika kipindi hicho, taasisi na mikoa ziendelee na uzinduzi wa miradi va maendeleo sambamba na shughuli za kijamii, hasa upandaji wa miti, uchangiai wa damu hospitali na vituo vya afya, usafi wa mazingira na mashindano ya michezo na uandishi wa insha kwa shule za msingi na sekondari nchini.
Pia, katika kipindi hicho, ifanyike kampeni ya kupiga vita unyanyasaji na ukatili wa kijinsia na kampeni ya kupambana na wanaotaka kumomonyoa maadili ya taifa.