UKAWA haikujiandaa kwa mafuriko haya

UKAWA haikujiandaa kwa mafuriko haya

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,866
Reaction score
4,252
SIo kwamba haikujiandaa kwa kimakosa bali pengine haikutarajia haya yanayoendelea. Pamoja na Mbowe kusema wengi watahamia Ukawa na chadema, alisema kimhemko na kihisia kulingana na wakati ule. Lowasa aliwahi kuema wakati bado yuko CCM akiwa Dodoma kuwa mtu hawezi kuzuai mafuriko kwa mikono. Kauli hiyo nayo ilijibiwa kishabiki na Nape ambapo sas anaona wazi jinsi mafuriko hayo yalivyo na madhara. Wako viongozi wengi pamoja na wanachama wengi wa ccm watafurikia Ukawa na hasa chadema. Mbowe aliwahi kusema kuwa mwanachama wa siku moja na wa miaka 20 wote wana haki sawa. Kiuhalisia hii si kweli.

Juzi Arusha tumeshuhudia aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani akihamia chadema mbele ya mkutano wa kumtambulisha Lowassa. Masha si mtu mdogo tu. ana ushawishi kwa vijana hasa wa kanda ya ziwa. Ushawiwi wake utakua baada ya wananchi kuona kahamia ukawa. Hili la Masha kuhamia ukawa nililiona kwa sura mbili; kwanza yeye ni kundi la Friends of Lowassa. Pili hakuwania ubunge jimbo la Nyamagana (jimbo la chadema chini ya Wenje) na badala yake kawania Sengerema kwa aliyekuwa mwanaccm mwenzake, Ngeleja. Hiki ni kizazi cha uongozi na kuja kwao ukawa ina maana kuna utafutaji wa madaraka na si uanachama wa kawaida tu.

Bado tutawaona wanaccm wengi tu ambao ni kizazi cha viongozi wakihamia ukawa na chadema. Hawa watu ukawa wanawapokeaje? Watakuwa wanachama tu au watapewa uongozi kama ukawa wakishika Dola? Kama Prof Kitila alivyomnukuu Nkrumah kwamba 'utafuteni kwanza ufalme wa kisiasa na mengine yatafuata'. Baada ya Oktoba ukawa watajipangaje?

Maono yangu ni kuwa miaka mitano ya ukawa madarakani itakuwa ya mkanganyiko sana maana serikali itakuwa na mseto wa hali ya juu ambao haujawahi kutokea katika Taifa hili. Vipaumbele vitawekwa upande gani?

Kwa upande wa ccm wanaweza kukubali kushindwa na wakakaza moyo na kujikunyata pamoja wakijiuliza ni nini kimetokea. Kisha wakaanza kujianga tena taratibu na baada ya miaka mitano wakawa tishio tena kwa ukawa. Kitakachotokea sasa ni kizazi cha viongozi wa ccm 'wanaokatwa' huko kuhamia ukawa kwa shinikizo na upepo wa mabadiliko. Bado tunawasubiri kina Nchimbi, Kingunge, na tetesi kuwa kuna kina Sumaye na wengine.

Napenda tujadili hili. UKAWA imejiandaaje kwa mabadiliko na mapokezi haya?
 
Ogopa sana umasikini usiogope mabadiliko-tazama shule zetu,tazama hospitali ,tazama uchafu wa miji,tazama watoto wamedumaa, tazama uchawi bado unaaminika tazama utajiri wa watoto wa maccm
 
Wengi wanaoshindwa kwenye kura za maoni majimbon mwao, ndio wanaohamia Ukawa.. Wakijua kbsa Ukawa inaweza ikashinda na wenyew hawataachwa.. Hasara watapata pale Ukawa itaposhindwa, cjui wataelekea wap tn! maana wanahama kwa mbwembwe hao, kurud kwao itakuwa aibu kubwa..
 
Wengi wanaoshindwa kwenye kura za maoni majimbon mwao, ndio wanaohamia Ukawa.. Wakijua kbsa Ukawa inaweza ikashinda na wenyew hawataachwa.. Hasara watapata pale Ukawa itaposhindwa, cjui wataelekea wap tn! maana wanahama kwa mbwembwe hao, kurud kwao itakuwa aibu kubwa..

Naomba uondoe dhana ya kushindwa kwenye kichwa chako,UKAWA wanachukua nchi asbh.
 
Wengi wanaoshindwa kwenye kura za maoni majimbon mwao, ndio wanaohamia Ukawa.. Wakijua kbsa Ukawa inaweza ikashinda na wenyew hawataachwa.. Hasara watapata pale Ukawa itaposhindwa, cjui wataelekea wap tn! maana wanahama kwa mbwembwe hao, kurud kwao itakuwa aibu kubwa..

Kushindwa mwiko. Mkwere akizingua kukabizi gongo, mafuriko yanamuhusu
 
Lengo lako ni nini na huu uzi wako!? Unawataka UKAWA wasipokee wageni kama Dr. Slaa alivyofanya. Ubinafsi ni maradhi makubwa sana,hongera sana Mbowe.
Kupokea wageni rukha, tatizo ni pale tayari una wageni kwako. Wengine hawajui wamefikaje ila nao wanahitaji nafasi. Ukawa imejipangaje kupanga na kupangua bila madhara mengine?
 
Hata tsunami hutulia yenyewe haihitaji mtu kuizuwia.

Binadam anaefata mafuriko huyo hajielewi, anakwenda na maji.

Red: Asante. Tuamini kuwa mambo ndani ya ukawa yatatulia.

Blue: Tsunami inafuata na haifuatwi
 
UKAWA itajali maslahi ya Taifa... Watu wa Vatican wanaangalia maslahi yao Zaidi ...
 
Kupokea wageni rukha, tatizo ni pale tayari una wageni kwako. Wengine hawajui wamefikaje ila nao wanahitaji nafasi. Ukawa imejipangaje kupanga na kupangua bila madhara mengine?

Hao wanaopokelewa ni Warundi,Wakenya ama Waganda? Kuweni wakweli anayekiuwa chama chenu CCM ni mwenyekiti wenu,tatizo la wana CCM mna nidhamu ya woga na kutanguliza matumbo mbele. Leo chama mmemwachia Nape mtoto wa mama je mtafika?
 
Wengi wanaoshindwa kwenye kura za maoni majimbon mwao, ndio wanaohamia Ukawa.. Wakijua kbsa Ukawa inaweza ikashinda na wenyew hawataachwa.. Hasara watapata pale Ukawa itaposhindwa, cjui wataelekea wap tn! maana wanahama kwa mbwembwe hao, kurud kwao itakuwa aibu kubwa..

Ndio! lakini kuna ubaya gani ukiamini kuwa Mungu yupo ukaishi kwa uadilifu kama matakwa yake na siku ya mwisho ukakuta hayupo? Unataka uamini kuwa hayupo ikitokea ukafika kule ukakuta yupo huoni kuwa itakuwa imekula kwako!
 
Hao wanaopokelewa ni Warundi,Wakenya ama Waganda? Kuweni wakweli anayekiuwa chama chenu CCM ni mwenyekiti wenu,tatizo la wana CCM mna nidhamu ya woga na kutanguliza matumbo mbele. Leo chama mmemwachia Nape mtoto wa mama je mtafika?

leo hii hata wewe hapo kama una familia yako halafu akatokea mtoto anayesadikiwa ni wako ulimzaa nje ya taratibu ni wazi kwa kiasi fulani ataigharimu familia yako. kadhalika sio kila anayeikosoa au kuizungumZia ukawa si lazima awe ccm
 
Back
Top Bottom