KERO Ukatili Shalom Center, Kisongo - Arusha

KERO Ukatili Shalom Center, Kisongo - Arusha

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Napenda kuwasilisha malalamiko rasmi kuhusu hali ya watoto wanaolelewa katika kituo cha watoto yatima kinachojulikana kama Shalom Center, kilichopo Kisongo, Arusha.

Kwa masikitiko makubwa, kuna taarifa zinazoonyesha kuwa watoto katika kituo hicho wanakumbana na vitendo vya ukatili na unyanyasaji wa hali ya juu, ikiwemo:

  • Kukosa lishe bora na mlo kamili, hali inayosababisha baadhi ya watoto, hususan walio chini ya umri wa miaka 5, kuonyesha dalili za utapiamlo.
  • Adhabu kali na za kikatili kutoka kwa walezi, ikiwa ni pamoja na kupigwa kwa kutumia fimbo, mwiko, mateke na vipigo vinavyosababisha majeraha na makovu ya kudumu.
  • Watoto kutumikishwa kazi zisizowafaa, ikiwemo kufanya kazi za ndani (house girls) katika familia za baadhi ya wafanyakazi.
  • Baadhi ya watoto kupelekwa kufanya kazi katika biashara za mkurugenzi (ikiwemo duka lililopo Iringa), pamoja na madai ya unyanyasaji wa kingono unaofanywa na baadhi ya ndugu wa mmiliki wa kituo.
  • Wafanyakazi wa kituo kutishwa kufukuzwa kazi endapo watajaribu kuripoti au kupinga vitendo hivi.
  • Misaada inayotolewa na wafadhili kutowafikia watoto kama ilivyokusudiwa.
Aidha, wageni wanaotembelea kituo hicho wamekuwa wakipokea malalamiko ya moja kwa moja kutoka kwa watoto kuhusu mateso wanayopitia.

Kutokana na uzito wa tuhuma hizi, naomba mamlaka husika zichukue hatua za haraka kufanya uchunguzi wa kina juu ya kituo hiki, kulinda usalama wa watoto waliopo hapo, na kuwawajibisha wote watakaobainika kuhusika na vitendo hivi vya ukatili.

Afya, usalama, na haki za watoto lazima zilindwe kwa gharama yoyote.
 
Mh waziri yupo ngangari hili atalifanyia kazi akilisoma , LAKINI pia Kuna ifisi ya ustawi WA jamii wilaya au manispaaa ungekufikisha hapo
 
Inabidi iwe kweli

Ila watoto wanaolelewa kwenye vituo kama hivyo baadhi yao wanakuwaga watukutu sana so mnapowaripoti hao waendesha kituo inabidi muwe na ushahidi

So kutokana na utukutu wao inabidi wawekewe adhabu rafiki ziwafunze

Haiwezekani umlee mtoto hata haumuelekezi kwa kumkemea hata kidogo

Nimeshawahi ishi karibu na kituo cha watoto kama hao aisee ni watundu hatar yaani
 
Kwa aliyekaa Arusha anaelewa vizuri kuhusu ma-zengwe ya mji huo. Wenye jukumu wafuatilie ili tujue ukweli.
 
Back
Top Bottom