Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 5,897
- 10,358
MTOTO Grace Mwita mwenye umri wa miaka mitano, mkazi wa mtaa wa Starehe wilayani Tarime mkoani Mara amechomwa mikono kwa moto na baba yake mzazi Mwita Abdala na kumsababishia majeraha na maumivu makali akimtuhumu kudokoa mboga aina ya dagaa iliyokuwa imepikwa na baba huyo kwa ajili ya chakula cha mchana.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo, Novemba 28, 2023 ambapo baba wa mtoto huyo, amekiri kufanya tukio hilo la kumchoma moto mikono mtoto wake kisa alidokoa mboga.
Chanzo: Nipashe